Afrika bado sana, tusichekane, kule Tanzania wanafunzi kusoma kwa zamu kisa uhaba wa madarasa

MK254

JF-Expert Member
May 11, 2013
31,746
48,385
Yaani wanafunzi wanasubirishwa nje ili kundi la kwanza likamilishe somo kwenye ratiba yao, hii Afrika tumechelewa kweli maana siamini mambo kama haya yanatendeka kwenye karne hii miaka mingi sana tangu mkoloni aondoke. Vipau mbele hamna, utakuta wakulu wanasafiri kwa magari ya kifahari kwenye misafara hadi raha.

========

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge jana Jumanne Januari 6 amesema wanafunzi waliofaulu kuingia kidato cha kwanza mwaka huu watasoma kwa zamu kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa katika mkoa huo.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya shule kwa ajili ya wanafunzi hao, Kunenge amesema wamefikia hatua,ili wengine wasibaki nyumbani na itakapofika Februari 28,2021 wataendelea na utaratibu wa kawaida.

Kunenge amebainisha kuwa Tayari uongozi wa Mkoa umeomba kibali wanafunzi wote kuanza kwenda shule japo kwa zamu kutokana na uhaba wa madarasa ambapo wataanza Januari 11, 2021.

 
Hahahahaaa, njoo hapa usaidie Wakenya wenzako wamechapwa vibaya kwenye battle ya shule za Govt

 
Kama hapa Kenya,wanafunzi wote wako ndani ya darasa

kenya.JPG
 
Hahahahaaa, njoo hapa usaidie Wakenya wenzako wamechapwa vibaya kwenye battle ya shule za Govt

kichapo mlikipata mkaanza kulia mapema eti si shule za serikali tukawaacha mjienjoy, watanzania kwa propaganda na kutopenda facts khaaa...the fact remains tanzania education sector ipo nyuma sana ndo maana unaona haya wanafunzi kusoma kwa zamu na wengine kukosa nafasi kwenye shule za upili.

Kenya ambapo pana 100% transition from primary to secondary school hamna kitu kama kusoma kwa zamu na kila mwanafunzi anapata nafasi kwenye public school. Infact it's a criminal offense kumzuia mwanafunzi kujiunga na shule ya upili anapo maliza primary
 
Halafu kinachohuzunisha zaidi, ni taarifa za Dar, yaani mkuu wa mkoa wa Dar, mji ambao huwa kidogo kama tegemezi lenu kwa kuona mataa. Ina maana kule mikoani ni choka mbaya...
Kila mkoa Tanzania ina uhaba wa shule na madarasa..huku ni kigoma.mkoa mmoja tu wanafunzi zaidi ya elfu tano kutojiunga na shule ya upili

FB_IMG_16100014795647001.jpeg
 
kila mkoa tanzania ina uhaba wa shule na madarasa..huku ni kigoma.mkoa mmoja tu wanafunzi zaidi ya elfu tano kutojiunga na shule ya upiliView attachment 1670672

Yaani inatia huruma ukizingatia kwao huko kumaliza shule ya msingi ni bado sana ni kama aliyeishia kwenye darasa la pili huku, sasa hao maelfu wanamaliza la saba na kuingia kitaa.
 
Yaani inatia huruma ukizingatia kwao huko kumaliza shule ya msingi ni bado sana ni kama aliyeishia kwenye darasa la pili huku, sasa hao maelfu wanamaliza la saba na kuishia kitaa.
Yn we jamaa huwa unanichekesha sn comments zako, ila njoo kule usaidie wenzako kutuonesha huo wingi wa shule zenu unaozidi zetu mana wenzako wamesusia uzi
 
Hapa vp mkuu..Tanzania tunasoma kwa zamu Kenya hakuna kabisa madarasa..watoto wanakaa chini..nua lao, mvua yaoView attachment 1670730

Kinachoshangaza, yaani mji wenu wa Dar ambao ndio wenye mataa na ndio Tanzania, huko kuna mapungufu ya madarasa, sasa kule kwingine ndio kuna kero za kufa mtu, halafu mkuu wa mkoa mwenyewe ndiye kakiri hata sio mipicha ya asasi za kijamii ambazo hutia chumvi na kukoleza taarifa, hapo ni kiongozi mkuu serikalini, jameni shughuli sana kwa kweli.

Mnanikumbusha yale mapicha yalipigwa na mwanafunzi wa chuo kikuu namna kuta za vyuo vyenu zilivyo na nyufa, yaani mpaka chuo kikuu ni kero, poleni sana kwa kweli.
 
Halafu naona walimu ni mwendo wa kufungua nyuzi tu....

 
Yn we jamaa huwa unanichekesha sn comments zako, ila njoo kule usaidie wenzako kutuonesha huo wingi wa shule zenu unaozidi zetu mana wenzako wamesusia uzi
Sasa unataka tuonyeshe picha za shule zote zilizopo Kenya ama? There are over 9,000 secondary schools alone in Kenya. Hapo hujaweka za msingi which are even way more. How do you want us to post all those? Kuna vitu zingine common sense should apply. Not everything calls for stupid battles and arguments
 
Back
Top Bottom