Africaoline wana matatizo gani?

Inviolata

Member
Apr 23, 2009
70
2
Jamani sisi tunaotumia mtandao wa Africaonline kwa ajili ya matumizi ya internet tumeonja joto ya jiwe toka jumamosi mpaka leo hii ninapoandika hii bado hatuna internet. Network hakuna toka jumamosi mpaka leo hii jumatatu. Tumejaribu kuwapigia simu mara kwa mara lakini tumekuwa tukijibiwa kuwa kuna tatizo ila linashughulikiwa baada ya muda litaisha. lakini cha kushangaza mpaka tunafunga ofisi leo jioni j3 hapakuwa na mabadiliko yoyote. Cha kusikitisha zaidi ni kwamba ilipofika mida ya kwenye saa 6 mchana hata simu wakawa hawapokei. Kitendo cha kutopokea simu kwa kweli kimenikera sana. Imagine clients wanakupigia simu wakilalamika kutojibiwa mail zao. Tunaomba majibu yanayoeleweka kutoka Africaonline.
 
Back
Top Bottom