joto la jiwe
JF-Expert Member
- Sep 4, 2017
- 26,117
- 46,613
Baada ya Kenya kushindwa katika lengo lake la kumpigia debe Balozi Amina Mohammed ili kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Africa miaka miwili iliyopita pamoja na kuweka juhudi kubwa na kutumia pesa nyingi ili kufanikisha lengo hilo, kwa Mara nyingine tena, nchi za Africa zimeonyesha kutokua na imani na Kenya baada ya kuichagua Ghana iwe ndio makao makuu ya sekretarieti ya Africa kuhusu biashara huru barani Africa.
Kenya imekua Mara kwa Mara ikijaribu kugombea nafasi mbalimbali za Africa bila mafanikio, hii ni dalili wazi kwamba nchi za Africa hazina imani na Kenya, hii ni tofauti na mashirika mbalimbali ya nje ya Africa ambayo hupendelea kufungua ofisi zao Nairobi. Je hii ni kusema kwamba Kenya inakubalika zaidi nje ya Africa kuliko ndani ya Africa?, kama jibu ni ndio, sababu gani inayosababisha Kenya isikubalike Africa?
Kenya imekua Mara kwa Mara ikijaribu kugombea nafasi mbalimbali za Africa bila mafanikio, hii ni dalili wazi kwamba nchi za Africa hazina imani na Kenya, hii ni tofauti na mashirika mbalimbali ya nje ya Africa ambayo hupendelea kufungua ofisi zao Nairobi. Je hii ni kusema kwamba Kenya inakubalika zaidi nje ya Africa kuliko ndani ya Africa?, kama jibu ni ndio, sababu gani inayosababisha Kenya isikubalike Africa?