Crocodiletooth
JF-Expert Member
- Oct 28, 2012
- 18,611
- 20,936
KAZI SASA IMEANZA AFRICA
~~~~~~~
Mamlaka za Gambia zimetangaza kuizuia kutua nchini humo ndege ya Rais Ellen Sirleaf Johnson ambaye pia ni Mwenyekiti wa hivi sasa wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Magharibi mwa Afrika ECOWAS.
Rais wa Liberia alitarajiwa kuwasili nchini Gambia leo kwa ajili ya kufanya juhudi za kuikoa nchi hiyo isitumbukie katika mgogoro wa kisiasa baada ya Rais Yahya Jammeh kutangaza kuyapinga matokeo ya uchaguzi wa Rais ambapo mpinzani wake Adama Barrow aliibuka na ushindi.
Nabkeur Ndiaye, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Senegal ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba, Rais wa Liberia ambaye ni Mwenyekiti wa hivi sasa wa Jumuiya ya ECOWAS alikuwa aelekee Gambia leo lakini ndege yake ilizuiwa kutua mjini Banjul.
Ripoti zaidi zinasema kwamba, Yahya Jammeh alitangaza kwamba, hatamruhusu mwenyekiti huyo wa Ecowas kutua nchini Gambia.
Hayo yanajiri katika hali ambayo, Rais Yahya Jammeh wa Gambia ametangaza kuwa hatambui matokeo ya uchaguzi wa Rais uliofanyika nchini humo Disemba Mosi.
Jammeh ametangaza msimamo huo ikiwa imepita karibu wiki moja tangu uchaguzi huo ufanyike na mgombea wa muungano wa upinzani kuibuka mshindi. Yahya Jammeh ametaka ufanyike uchaguzi mwingine mpya wa rais.
[HASHTAG]#THIS[/HASHTAG] AFRICA BANA.
;>>RECOLONISATION MATTERS.
~~~~~~~
Mamlaka za Gambia zimetangaza kuizuia kutua nchini humo ndege ya Rais Ellen Sirleaf Johnson ambaye pia ni Mwenyekiti wa hivi sasa wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Magharibi mwa Afrika ECOWAS.
Rais wa Liberia alitarajiwa kuwasili nchini Gambia leo kwa ajili ya kufanya juhudi za kuikoa nchi hiyo isitumbukie katika mgogoro wa kisiasa baada ya Rais Yahya Jammeh kutangaza kuyapinga matokeo ya uchaguzi wa Rais ambapo mpinzani wake Adama Barrow aliibuka na ushindi.
Nabkeur Ndiaye, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Senegal ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba, Rais wa Liberia ambaye ni Mwenyekiti wa hivi sasa wa Jumuiya ya ECOWAS alikuwa aelekee Gambia leo lakini ndege yake ilizuiwa kutua mjini Banjul.
Ripoti zaidi zinasema kwamba, Yahya Jammeh alitangaza kwamba, hatamruhusu mwenyekiti huyo wa Ecowas kutua nchini Gambia.
Hayo yanajiri katika hali ambayo, Rais Yahya Jammeh wa Gambia ametangaza kuwa hatambui matokeo ya uchaguzi wa Rais uliofanyika nchini humo Disemba Mosi.
Jammeh ametangaza msimamo huo ikiwa imepita karibu wiki moja tangu uchaguzi huo ufanyike na mgombea wa muungano wa upinzani kuibuka mshindi. Yahya Jammeh ametaka ufanyike uchaguzi mwingine mpya wa rais.
[HASHTAG]#THIS[/HASHTAG] AFRICA BANA.
;>>RECOLONISATION MATTERS.