Afisa wa TRA Mwanza Bi. Mary Moyo akamatwa na TAKUKURU kwa kuomba na kupokea rushwa ya Tsh.milioni 8

Countrywide

JF-Expert Member
Mar 2, 2015
18,173
27,223
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Jijini Mwanza imemkamata Afisa wa TRA, Bi. Mary Moyo akipokea rushwa kutoka kwa Mfanyabiashara.

Naibu Mkuu wa TAKUKURU mkoani humo, DAUD NDYAMUKAMA amesema mtuhumiwa Moyo aliomba rushwa ya tsh Milion 8 (8,000,000) kutoka kwa Mfanyabiashara huyo hili apunguzie malipo ya kodi.

Mtuhumiwa amefikishwa Mahakamani kwa ajili ya kusomemwa kesi yake.

--------

Afisa wa TRA Bi. Mary hatimaye amekamatwa, waliosema za mwizi ni arobaini hawakukosea kabisa.

Niwe muwazi moja ya kitu ambacho niliwahi kukata nacho tamaa ni TRA mkoa wa mwanza, nimeenda mara nyingi kwenye shughuli zangu nikitokea dar ili kuweza kuweka mambo sawa lakini nilikutana na kila aina ya usumbufu na dharau.

Mtu anataka umpatie pesa ila dharau anayokuonyesha sio ya kawaida, mimi bado siamini kama serikali inawatuma kufanya hivyo ila tu ni tabia zao ambazo wameamua kwa makusudi wawe nazo.

Pole sana Bi. mary, hii ni fundisho kwako na kwa wenzako hapo mwanza, za mwizi ni arobaini.

Nawapongeza sana Takukuru kwa hiki mlichofanya mwanza kwa kumuwekea mtego mtu huyu na pia nampongeza sana mfanyabiashara huyo kwa kwenda kutoa taarifa takukuru ili kukomesha hii tabia.

Kuna wakati niliwahi kuwaambia kuwa nitawashitaki takukuru na nilitaka kwenda kuwaambia takukuru ili tuwaekee mtego, lakini huruma iliniingia sana.

TRA jirekebisheni sio kila mtu ana huruma kama sisi wengine.
 
Sababu ya mshahara mzuri (wa juu) wanaolipwa wafanyakazi wa tra ni ati, kuwaepusha na vishawishi vya rushwa. Haya ndio hao wanaowekewa mitego, sijui wangapi wanapokea rushwa bila ya mitego yoyote.
 
Sababu ya mshahara mzuri (wa juu) wanaolipwa wafanyakazi wa tra ni ati, kuwaepusha na vishawishi vya rushwa. Haya ndio hao wanaowekewa mitego, sijui wangapi wanapokea rushwa bila ya mitego yoyote.
Kulipa mshahata mkubwa sio sababu ya watu kukwepa rushwa
 
Rushwa ipo sana tu,kuna ofisi ya ardhi nimeenda juzi yaani jamaa bila hata uoga cos hatufahamiani kabisa,ila akaniambia direct Laki moja ilikufanikisha jambo langu,nilimuonea huruma sana maana kuna siku atakutana na nyoka.....hata amini.....anyway nikamtoa 20 ,faster nikapata huduma nikasepa
 
Rushwa ipo sana tu,kuna ofisi ya ardhi nimeenda juzi yaani jamaa bila hata uoga cos hatufahamiani kabisa,ila akaniambia direct Laki moja ilikufanikisha jambo langu,nilimuonea huruma sana maana kuna siku atakutana na nyoka.....hata amini.....anyway nikamtoa 20 ,faster nikapata huduma nikasepa
Rushwa kila idara, uhamiaji, ardhi, tra nida. Ni shida.
 
Wengi hukamatwa na rushwa hawa TRA na Takukuru Ila mwisho wao hatuusikii naona huwa wanayamaliza juuu kwa juuuu
 
1. Hivi Kuna mtu kafungwa jela baada ya kuwekewa mtego na TAKUKURU?
2. Hivi katika magereza yetu Kuna mfungwa hata mmoja aliyetokea TRA au NIDA au BRELA?
3. TAKUKURU mnakwama wapi? Mnaweka mitego halafu kirahisi tu watu wa TRA wanategua? Au wanawapa hela ya kiwi?
 
Kwani kutoa na kupokea rushwa ni kosa kisheria hapa nchini?, wajumbe naomba mnijibu.
 
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Jijini Mwanza imemkamata Afisa wa TRA, Bi. Mary Moyo akipokea rushwa kutoka kwa Mfanyabiashara.

Naibu Mkuu wa TAKUKURU mkoani humo, DAUD NDYAMUKAMA amesema mtuhumiwa Moyo aliomba rushwa ya tsh Milion 8 (8,000,000) kutoka kwa Mfanyabiashara huyo hili apunguzie malipo ya kodi.

Mtuhumiwa amefikishwa Mahakamani kwa ajili ya kusomemwa kesi yake.

--------

Afisa wa TRA Bi. Mary hatimaye amekamatwa, waliosema za mwizi ni arobaini hawakukosea kabisa.

Niwe muwazi moja ya kitu ambacho niliwahi kukata nacho tamaa ni TRA mkoa wa mwanza, nimeenda mara nyingi kwenye shughuli zangu nikitokea dar ili kuweza kuweka mambo sawa lakini nilikutana na kila aina ya usumbufu na dharau.

Mtu anataka umpatie pesa ila dharau anayokuonyesha sio ya kawaida, mimi bado siamini kama serikali inawatuma kufanya hivyo ila tu ni tabia zao ambazo wameamua kwa makusudi wawe nazo.

Pole sana Bi. mary, hii ni fundisho kwako na kwa wenzako hapo mwanza, za mwizi ni arobaini.

Nawapongeza sana Takukuru kwa hiki mlichofanya mwanza kwa kumuwekea mtego mtu huyu na pia nampongeza sana mfanyabiashara huyo kwa kwenda kutoa taarifa takukuru ili kukomesha hii tabia.

Kuna wakati niliwahi kuwaambia kuwa nitawashitaki takukuru na nilitaka kwenda kuwaambia takukuru ili tuwaekee mtego, lakini huruma iliniingia sana.

TRA jirekebisheni sio kila mtu ana huruma kama sisi wengine.
Ana kesi za kujibu kutengeneza mazingira ya rushwa, kupokea rushwa na rushwa ni adui wa haki, kuikwepesha serikali mapato, pia kuwakandamiza walipa kodi, acha awekwe ndani hata Mungu hapendi rushwa
 
Rushwa ipo sana tu,kuna ofisi ya ardhi nimeenda juzi yaani jamaa bila hata uoga cos hatufahamiani kabisa,ila akaniambia direct Laki moja ilikufanikisha jambo langu,nilimuonea huruma sana maana kuna siku atakutana na nyoka.....hata amini.....anyway nikamtoa 20 ,faster nikapata huduma nikasepa
Yani mtu yupo tayari ku risk mshahara wake wa mwezi, marupurupu nk kwa laki 1 huyo nae ni amekaukiwa hela mpaka anatia huruma, hata kumuekea mtego unamuonea huruma unajiuliza una umasikini wa kiasi gani au akili zimemruka
 
1. Hivi Kuna mtu kafungwa jela baada ya kuwekewa mtego na TAKUKURU?
2. Hivi katika magereza yetu Kuna mfungwa hata mmoja aliyetokea TRA au NIDA au BRELA?
3. TAKUKURU mnakwama wapi? Mnaweka mitego halafu kirahisi tu watu wa TRA wanategua? Au wanawapa hela ya kiwi?
Sio kila mtego unaweza kukunasa
 
Back
Top Bottom