Afisa wa TRA amenikera, anadai serikali haitambui biashara na mtu wa Congo

mandella

JF-Expert Member
Oct 29, 2011
3,048
3,227
Huyu afisa wa TRA anaongea kama vile ana lengo la kukomoa Watu wa clearing badala ya kutengeneza mazingira rafiki either ya watu kuelewa kuhusu VAT iliyoweka kwnye port charges na Shiping line kwa Transit .

Namnukuu "serikali haitambui biashara na mtu wa congo ''

Hii kauli imenikera saana .. kuongea hivyo anamaa hii bandari sasa ni kwa ajili ya local tu ..Kwann anaongea kwa kukomoa badala ya kutengeneza mazingira rafiki ya hii biashara ?

Kwann anaongea kama anabishana instead ya kuongea in a neutral way kwa ajili ya ku facilitate maswala yakae sawa ....Anaendelea kuongea ..msikilizeni ..asipiporekebisha kauli zake ataendele kuharibu hii biashara .
 
Huyu afisawa TRA anaongea kama vile ana lengo la kukomoa Watu wa clearing badala ya kutengeneza mazingira rafiki either ya watu kuelewa kuhusu VAT iliyoweka kwnye port charges na Shiping line kwa Transit .

Namnukuu "serikali haitambui biashara na mtu wa congo ''

Hii kauli imenikera saana .. kuongea hivyo anamaa hii bandari sasa ni kwa ajili ya local tu ..

Kwann anaongea kwa kukomoa badala ya kutengeneza mazingira rafiki ya hii biashara ?

Kwann anaongea kama anabishana instead ya kuongea in a nutral way kwa ajili ya ku facilitate maswala yakae sawa .

Anaendelea kuongea ..msikilizeni ..asipiporekebisha kauli zake ataendele kuharibu hii biashara .

Ila pia huyo Rais wa TAFA kajichanganya na kujikuta anatetea utozaji wa VAT kwenye hizo huduma bila kujijua. Pale alipotoa mfano wa mfanyabiashara aliyetoka Congo akilala hotelini, akila chakula akitumia huduma ya kuhamisha fedha ni sahihi kutozwa kodi kwa kuwa ametumia hapa...ina maana basi anaungana na huyo jamaa wa TRA kuwa hata hiyo huduma aliyopata ya kuhudumia mizigo hapa basi ni shurti itozwe VAT kwa kuwa huduma imepatikana hapa. Na ikumbukwe hizo gharama zote kuanzia kulala, kula, money transfer charges na PIA huduma za kufikisha mzigo Congo ZOTE HIZI huenda kutozwa kwa mlaji wa mwisho. Hivyo hakuna mantiki kwa nini huduma nyingine ziwe sawa kutozwa VAT na nyingine zisiwe sawa.
 
Ila pia huyo Rais wa TAFA kajichanganya na kujikuta anatetea utozaji wa VAT kwenye hizo huduma bila kujijua. Pale alipotoa mfano wa mfanyabiashara aliyetoka Congo akilala hotelini, akila chakula akitumia huduma ya kuhamisha fedha ni sahihi kutozwa kodi kwa kuwa ametumia hapa...ina maana basi anaungana na huyo jamaa wa TRA kuwa hata hiyo huduma aliyopata ya kuhudumia mizigo hapa basi ni shurti itozwe VAT kwa kuwa huduma imepatikana hapa. Na ikumbukwe hizo gharama zote kuanzia kulala, kula, money transfer charges na PIA huduma za kufikisha mzigo Congo ZOTE HIZI huenda kutozwa kwa mlaji wa mwisho. Hivyo hakuna mantiki kwa nini huduma nyingine ziwe sawa kutozwa VAT na nyingine zisiwe sawa.
Hapana ulimuelewa vibaya .

Huyu mgeni wa congo Final destnation ya yeye kulala ni hapa , akila anamaliza hapa .
Lakini akitoa mzigo final destanation ni Huko kwao Congo ...not here . no need of tht VAT .
 
Halafu hata kama wanapaawa kulipa hiyo VAT .. na hapo nyuma walikosea kutoiweka , hawapaswi kabisa kufanya hili jambo kama wanakomoa ,wangetafuta namna ya kuliingiza taratibu ., ina maana hawaoni kuna kuyumba kwa uchumi duniani kwa sasa , bandari ziliseez hata kabla ya VAT , stil tena wanaweka Chumvi kwnye kidonda kibichi . , hawaoni S.A wanalainisha sheria zao ?
 
Hakuna jinsi VAT on transit goods inamuathiri muagizaji. Kama mtu wa clearing atatozwa VAT, huduma za Bandari zitatozwa VAT mwisho wa siku gharama hizo lazima zifidiwe na Muagizaji ambaye atapelekewa mzigo wake nje ya nchi. Hili halina mjadala kwa maoni yangu.

Kama hivyo ndivyo value ya mzigo itaongezeka kwa kiwango cha VAT atakachotozwa Clearing Agent na VAT kwenye huduma nyinginezo za Bandari.
 
Kwa namna huyu Rais wa TAFA anavyojieleza hapa kwenye nafasi yake pia inabidi waweke Mnyarwanda
 
Hakuna jinsi VAT on transit goods inamuathiri muagizaji. Kama mtu wa clearing atatozwa VAT, huduma za Bandari zitatozwa VAT mwisho wa siku gharama hizo lazima zifidiwe na Muagizaji ambaye atapelekewa mzigo wake nje ya nchi. Hili halina mjadala kwa maoni yangu.

Kama hivyo ndivyo value ya mzigo itaongezeka kwa kiwango cha VAT atakachotozwa Clearing Agent na VAT kwenye huduma nyinginezo za Bandari.
Unaposema haina adhari unakosea .
Mfano gharama za kutoa gari ni dola 250 .. kama kampuni baada ya kulipa Charges zote nabaki na Dola 100.

Leo umeweka VAT . Unataka mm mfanyabiashara niendelee kumtoza th same price huyo mteja .
Na nikimzidishia ili niweze kulipa hiyo VAT unadhani anakubali ? Au ndio anakimbia ..dont say haina impact .
 
Hili swala lilikua ni lakupelekwa bungeni na Waziri Mkuu alishasema,kwa ubabe wa TRA waligoma kulipeleka na kuliingiza direct kwenye bajeti.
 
Hii radio leo imenisaidia kujua ni kiasi gani hizi taasisi zetu zimejaa watu wenye uelewa mdogo wa mambo wanayoyafanyia kazi.

Yaani mtu hata kabla ya kuja kuongea radioni hawezi kufanya japo utafiti mdogo ni kwa nini nchi zote duniani mizigo inayoitwa ya 'transit' hailipiwi hizi VAT. Na taasisi hizi zinajaza watu kama hawa bila kujua kuwa Tanzania ni miongozi mwa nchi ambazo ziko strategically positioned kwa ajili ya mizigo ya aina hii. Ndio maana katika nchi ya Misri/Egypt kuna chuo kikuu kimoja kinatoa MBA on logistics for East Africa.

Atakayenielea hapa afuatilie matrillion wanayopata Kenya kupitia bandari wakati tungelikuwa na kiwango sawa kiutendaji Kenya hawatakiwi kufikia hata robo yetu!
Cha kuchekesha zaidi huyo ofisa atakuwa anaongea na Kipanya na kumuona kama muuni fulani lakini hajui kuwa ni mtu mwelewa sana na mzalendo.
 
Hakuna jinsi VAT on transit goods inamuathiri muagizaji. Kama mtu wa clearing atatozwa VAT, huduma za Bandari zitatozwa VAT mwisho wa siku gharama hizo lazima zifidiwe na Muagizaji ambaye atapelekewa mzigo wake nje ya nchi. Hili halina mjadala kwa maoni yangu.

Kama hivyo ndivyo value ya mzigo itaongezeka kwa kiwango cha VAT atakachotozwa Clearing Agent na VAT kwenye huduma nyinginezo za Bandari.
Inaelekea akili yako inawaza kwa kiwango cha '....bora mkono uingie kinywani' na ndio maana unafikiria clearance ya gari lakini mizigo wanayoongelea hapa ni ya matajiri wenye viwanda huko Rwanda, Burundi, Congo, Zambia nk. Hawa wanaleta wastani wa meli mbili za mbolea, makontena 200 kwa mwezi na kupeleka nje mizigo kwa speed ile ile. Meli ambayo labda thamani ya mzigo wake ni USD $15 million ukipiga VAT yake unajua ni pungufu ya gharama za matruck ya kutoka tuseme Beira kwenda Zambia!?
Wenye uelewa ndio wanajua mahesabu haya na sio allowance za maofisa wa TRA na wenzao wa bandarini.
 
TRA wameanzisha VAT kwa transit goods sababu hapo awali kuna watanzania wasiowahaminifu walikuwa wanaingiza mizigo nchini kama transit goods, wakishafika njiani kabla ya kuvuka border wanaifungua na kuuza ndani ya nchi kama local goods hiyo ndio sababu ya serikali kutaka kuanzisha VAT kwa transit goods ili kuzuia ukwepaji wa kodi wa namna hiyo.
Upande wa pili naona hii sheria ipo kinyume na sheria za kimataifa zinazohusu kodi ya ongezeko la thamani VAT.
Ushauri wangu kwa serikali ni kuweka mfumo mzuri wa kuzuia ukwepaji wa kodi kwa wafanyabiashara wasio waaminifu ambao wanaingiza local goods kwa njia ya transit goods.
 
Huyu afisawa TRA anaongea kama vile ana lengo la kukomoa Watu wa clearing badala ya kutengeneza mazingira rafiki either ya watu kuelewa kuhusu VAT iliyoweka kwnye port charges na Shiping line kwa Transit .

Namnukuu "serikali haitambui biashara na mtu wa congo ''

Hii kauli imenikera saana .. kuongea hivyo anamaa hii bandari sasa ni kwa ajili ya local tu ..

Kwann anaongea kwa kukomoa badala ya kutengeneza mazingira rafiki ya hii biashara ?

Kwann anaongea kama anabishana instead ya kuongea in a neutral way kwa ajili ya ku facilitate maswala yakae sawa .

Anaendelea kuongea ..msikilizeni ..asipiporekebisha kauli zake ataendele kuharibu hii biashara .
Sasa serikal inamtambuaje huyo mtu wa congo au burundi serikal mteja wake ni yule aliepewa tenda ya clerearing na shiping hzo goods kwahyo hyo VAT lazima huyu wa shiping na clearing lazima alipe VAT mbona mataifa mengine wanalipa tatizo tumezoea kufanya kaz kwa mazoea sana hilo ndio shida kubwa inayotukumba kwa waafrika weng sana
 
Sasa serikal inamtambuaje huyo mtu wa congo au burundi serikal mteja wake ni yule aliepewa tenda ya clerearing na shiping hzo goods kwahyo hyo VAT lazima huyu wa shiping na clearing lazima alipe VAT mbona mataifa mengine wanalipa tatizo tumezoea kufanya kaz kwa mazoea sana hilo ndio shida kubwa inayotukumba kwa waafrika weng sana
Leo nimecheka TAFA wamebanwa hawana hoja...mtu anaulizwa kama unasema kodi anatozwa muagiza mzigo twambie wewe wakala unafanya shughuli gani anabaki kujing'ata! Ngatwanga kapwaya mno..!
 
Ambacho serikali haisemi: Ni kwa nini mwanzo huduma hizo zilikuwa hazitozwi kodi (VAT)? Nini ilikuwa mantiki ya kutokutoza kodi? Je, sababu hizo hazipo tena? Ni kitu gani kimebadilika?

Kuna umuhimu mkubwa kwa sera zetu za kodi kuzingatia athari za kiuchumi za muda mrefu badala ya kuangalia mapato ya kodi katika muda mfupi (5-10yrs ya utawala wa kisiasa!).
 
Leo nimecheka TAFA wamebanwa hawana hoja...mtu anaulizwa kama unasema kodi anatozwa muagiza mzigo twambie wewe wakala unafanya shughuli gani anabaki kujing'ata! Ngatwanga kapwaya mno..!
TAFA wanahoja ya kupinga hiyo VAT ila hawana point za kuishawishi serikali isianzishe VAT kwa transit goods, pia TRA wanahoja ya kutaka kuanzisha VAT kwa transit goods ila hawana hoja za kuwashawishi TAFA waelewe na mwisho ndio kilichokuwa kinatokea kwenye mjadala kutokuwepo maelewano baina ya TRA na TAFA.
Serikali inatakiwa iangalie pia sheria za kimataifa zinasemaje kuhusu VAT kwa transit goods sababu wanachotaka kufanya TRA ni kama ubabe ambao naona mwisho wa siku utaleta tatizo pale bandarini kuhusu idadi ya watakaoingiza transit goods
 
Transit ni transit tu. Ina maana ukismama Dubai airport au Kenya ukiwa on transit kwa ndege ulipe mi vat yao?
 
TAFA wanahoja ya kupinga hiyo VAT ila hawana point za kuishawishi serikali isianzishe VAT kwa transit goods, pia TRA wanahoja ya kutaka kuanzisha VAT kwa transit goods ila hawana hoja za kuwashawishi TAFA waelewe na mwisho ndio kilichokuwa kinatokea kwenye mjadala kutokuwepo maelewano baina ya TRA na TAFA.
Serikali inatakiwa iangalie pia sheria za kimataifa zinasemaje kuhusu VAT kwa transit goods sababu wanachotaka kufanya TRA ni kama ubabe ambao naona mwisho wa siku utaleta tatizo pale bandarini kuhusu idadi ya watakaoingiza transit goods
Ulisikiliza huu mjadala utagundua kuwa Wafanya biashara hawataki kulipa kodi hata wanao piga simu wao ni kulalama tui!
Hivi Agent kwanini asitozwe kodi kwenye huduma?
Halafu wengi wamekuwa wakisema ni mizigo ya nje halafu wakifika kati wanaishusha ...!
 
Sasa serikal inamtambuaje huyo mtu wa congo au burundi serikal mteja wake ni yule aliepewa tenda ya clerearing na shiping hzo goods kwahyo hyo VAT lazima huyu wa shiping na clearing lazima alipe VAT mbona mataifa mengine wanalipa tatizo tumezoea kufanya kaz kwa mazoea sana hilo ndio shida kubwa inayotukumba kwa waafrika weng sana
Document ya mzigo na shipping line ndio utambulisho tosha mkuu.
 
Back
Top Bottom