Afisa wa TRA amenikera, anadai serikali haitambui biashara na mtu wa Congo

This solution is the best.
Kama tatizo ni wafanyabiashara kushusha mizigo njiani, watafute jinsi ya kuzuia hilo tatizo. Kuweka VAT kama suluhu ya tatizo sio sawa.
Wakumbuke hiyo VAT imesababisha mizigo kushuka bandarini, kuna watu wameajiriwa kwenye kusafirisha hiyo mizigo. Hao watu hawana ajira tena.
Ni kweli mdau, na matokeo ya VAT kwenye transit goods ni kuongezeka kwa gharama za uingizaji wa mizigo hali itakayopelekea wafanyabiashara wa Congo, Zambia, Rwanda, Burundi n.k kutumia bandari za Mombasa, Beira Msumbiji au hata South Africa kwani nao wanafanya marekebisho kwenye sheria zao za transit.
TRA wanatumia vibaya matamko anayotoa Rais JPM kuhusu kodi hivyo wanataka kufanya mambo kwa nguvu bila kuzingatia hali halisi na sheria za kimataifa kuhusu VAT kwenye transit goods.
 
TRA wameanzisha VAT kwa transit goods sababu hapo awali kuna watanzania wasiowahaminifu walikuwa wanaingiza mizigo nchini kama transit goods, wakishafika njiani kabla ya kuvuka border wanaifungua na kuuza ndani ya nchi kama local goods hiyo ndio sababu ya serikali kutaka kuanzisha VAT kwa transit goods ili kuzuia ukwepaji wa kodi wa namna hiyo.
Upande wa pili naona hii sheria ipo kinyume na sheria za kimataifa zinazohusu kodi ya ongezeko la thamani VAT.
Ushauri wangu kwa serikali ni kuweka mfumo mzuri wa kuzuia ukwepaji wa kodi kwa wafanyabiashara wasio waaminifu ambao wanaingiza local goods kwa njia ya transit goods.
Mbona nimesikia hiyo VAT ukifika border inarudishwa?
 
Huyu afisa wa TRA anaongea kama vile ana lengo la kukomoa Watu wa clearing badala ya kutengeneza mazingira rafiki either ya watu kuelewa kuhusu VAT iliyoweka kwnye port charges na Shiping line kwa Transit .

Namnukuu "serikali haitambui biashara na mtu wa congo ''

Hii kauli imenikera saana .. kuongea hivyo anamaa hii bandari sasa ni kwa ajili ya local tu ..Kwann anaongea kwa kukomoa badala ya kutengeneza mazingira rafiki ya hii biashara ?

Kwann anaongea kama anabishana instead ya kuongea in a neutral way kwa ajili ya ku facilitate maswala yakae sawa ....Anaendelea kuongea ..msikilizeni ..asipiporekebisha kauli zake ataendele kuharibu hii biashara .


Sasa kwa nini haukumtumia sms kama lengo lako lilikuwa ni kumsuta? Kwa maana hapa haueleweki!
 
Sasa serikal inamtambuaje huyo mtu wa congo au burundi serikal mteja wake ni yule aliepewa tenda ya clerearing na shiping hzo goods kwahyo hyo VAT lazima huyu wa shiping na clearing lazima alipe VAT mbona mataifa mengine wanalipa tatizo tumezoea kufanya kaz kwa mazoea sana hilo ndio shida kubwa inayotukumba kwa waafrika weng sana
siku nyingine soma mada uelewe na uchangie kama mwenye akili timamu sio kimihemko sasa kama ni kwa ajili ya clearing agent kwa nini wateja wakimbie?hivi unajua maana ya VAT kweli ?hii sishangai maana ni sawa na yale yaliyotokea ktk mabenk sijui nani hapa anakomolewa.
 
Mbona nimesikia hiyo VAT ukifika border inarudishwa?
Kinachorudishwa border ni bond sio VAT, bond ni kiasi cha pesa chenye samani sawa na mzigo wa transit ambacho wakala wa forodha analipa Kitengo cha Custom-TRA, kama security ya mzigo wa transit aliochukua dhamana ya kuusafirisha. Na mzigo ukifika salama border basi kampuni ya uwakala wa forodha hurudishiwa bond yake na mzigo usipofika salama border basi TRA huendelea kushikilia hiyo bond
 
Leo nimecheka TAFA wamebanwa hawana hoja...mtu anaulizwa kama unasema kodi anatozwa muagiza mzigo twambie wewe wakala unafanya shughuli gani anabaki kujing'ata! Ngatwanga kapwaya mno..!
pye unadhani mnawakomoa maajent wakati ndo imekula kwenu wateja iko kimbia nyie na bandari yenu hamkawii kusema ni bandari pekee afrika na watakuja tu..:D:D:D:D:D:D
 
Ulisikiliza huu mjadala utagundua kuwa Wafanya biashara hawataki kulipa kodi hata wanao piga simu wao ni kulalama tui!
Hivi Agent kwanini asitozwe kodi kwenye huduma?
Halafu wengi wamekuwa wakisema ni mizigo ya nje halafu wakifika kati wanaishusha ...!
jamani si nimesikia kuna track system za kuangalia hiyo mizigo ama ilikua ni mbwembwe tu sasa kama hii ni kwa wafanya biashara kulipa kodi kwa nini mizigo ipungue ama watu wakimbilie kwengine au kwa nini situation isibaki kama zamani na mizigo ileile kama hiyo vat haitawahusu waagizao mizigo hapa lazima muwaze mara mbili hata kama tunataka fedha lakini tuangalie ni jinsi gani tutakavo shindana na wenzetu wengine ili tusipoteze yale mapato ya kuvunja rekodi .Na ninawaomba yale mapato ya kuvunja rekodi waendelee kuyataja kila mwezi tuone basi nani mkweli.Pia waangalie wapinzani wao wanavotoa huduma jamani mbona vitu simple tu tamaa mbaya mtakuja kutafutana ubaya hapa baadae kila mtu ajitoe oho haya.Biashara ushindani.
 
Ni kweli mdau hawa maafisa wa TRA pamoja na TAFA kwenye ule mjadala hawakuwa nakujielewa fulani, ni kama walienda kwenye ule mjadala kwa ajili ya mabishano tu na kutunishiana misuli kwa TRA kutaka kulazimisha kuanzisha hiyo VAT kwa transit goods na TAFA kupinga uanzishwaji wa VAT kwa transit.
Kwa undani ukifatilia point zao TRA na TAFA ni dhaifu kuweza kushawishi upande wowote kati yao kukubali hoja ya mwenzie.
nashindwa kuwaelewa mnaotetea TRA nadhani mliona picha juzi ya mabenk na sijui imeishia wapi huyu anasema hivi huyu vile hivi mpk hapo tu huwezi kuwaprove failure tax si kitu cha kukurupuka ni kukaa pamoja na kujadili sio kufanya mtakavyo kwa vile wana hiyo power lakini wakumbuke hizo biashara zikifungwa pia watakosa hata hiyo elfu kumi waliokua wanaipata na sijui watamnyonya nani from there maana wanasema makampuni mengi hayajasajiliwa vat that means mtaji wao mdogo haohao unataka kuwaondoa badala ya kukaa na kujadiliana kusaidia halafu mnataka uchumi wakati kwa stail hii ya ubabe?tusije tukawa zimbabwe kwa ubabe usio na matunda.Hii nchi ni yetu wote si ya kina fulani lazima kila mtu ainjoy matunda ya kazi anayofanya sio kuifanyia kazi serikali tu na yenyewe ifanye biashara basi si kuumiza wananchi.Maana akiumia huyu wa kipato cha kati cha chini si ndo kwishe.Hekima ni bora kuliko..........
 
Kodi Zote za nchi hii hupitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano, Hawa jamaa wa mapato wao wanasimama just for tax laws enforcement na TAFFA(customs), Wafanyabiashara(kwa upande wa domestic revenue) wanasimama kama Agency ktk Collection ya Revenue. Sasa Mwenye Mamlaka ya kutoa ufafanuzi wa hili Jambo ni Waziri wa Fedha, Maana TRA ipo chini ya wizara ya fedha, imekaa kama kitengo cha makusanyo, so usishangae ukamwuliza mfanyakazi wa Mapato au Agent asiwe na Majibu sahihi, Mnakumbuka ile issue ya VAT ktk Mabanks na M-Pesa? Kiufupi, Bado kuna haja ya kila Mwananchi kuwa na Uelewa na Kila Kodi ya serikali, iwe PAYE, SDL, au tuite tu Direct and Indirect Taxes, Pia kujua Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hivi Vitu natamani Vingefundishwa Toka Secondary Kabisa au Primary, Viwepo Vilabu vya Taxes na Mengineyo. Halafu Serikali pia inapaswa kutanua wigo wa kodi baada ya kufanya tafiti, Kwa sababu VAT na Kodi zingine, Mara nyingi Mwananchi ndiye anayelipa.
 
jamani si nimesikia kuna track system za kuangalia hiyo mizigo ama ilikua ni mbwembwe tu sasa kama hii ni kwa wafanya biashara kulipa kodi kwa nini mizigo ipungue ama watu wakimbilie kwengine au kwa nini situation isibaki kama zamani na mizigo ileile kama hiyo vat haitawahusu waagizao mizigo hapa lazima muwaze mara mbili hata kama tunataka fedha lakini tuangalie ni jinsi gani tutakavo shindana na wenzetu wengine ili tusipoteze yale mapato ya kuvunja rekodi .Na ninawaomba yale mapato ya kuvunja rekodi waendelee kuyataja kila mwezi tuone basi nani mkweli.Pia waangalie wapinzani wao wanavotoa huduma jamani mbona vitu simple tu tamaa mbaya mtakuja kutafutana ubaya hapa baadae kila mtu ajitoe oho haya.Biashara ushindani.
Track system ilianzishwa ila ilikuwa ni kwa majaribio tu tena ilikuwa ni kwa border moja tu ya kasumulu mpaka wa Tanzania na Malawi kwa kuwa ile border haiko bize sana kama zilivyo border kama Tunduma, Mtukula, Namanga, Rusumo, Kabanga n.k ila sijajua ule mpango wa transit tracking system uliishia wapi kwani ni njia nzuri sana ya kusimamia transit goods na unatumika katika nchi chache zilizoendelea kama South Africa ingawa nasikia ule mfumo wa transit tracking system ulifeli kenya
 
nashindwa kuwaelewa mnaotetea TRA nadhani mliona picha juzi ya mabenk na sijui imeishia wapi huyu anasema hivi huyu vile hivi mpk hapo tu huwezi kuwaprove failure tax si kitu cha kukurupuka ni kukaa pamoja na kujadili sio kufanya mtakavyo kwa vile wana hiyo power lakini wakumbuke hizo biashara zikifungwa pia watakosa hata hiyo elfu kumi waliokua wanaipata na sijui watamnyonya nani from there maana wanasema makampuni mengi hayajasajiliwa vat that means mtaji wao mdogo haohao unataka kuwaondoa badala ya kukaa na kujadiliana kusaidia halafu mnataka uchumi wakati kwa stail hii ya ubabe?tusije tukawa zimbabwe kwa ubabe usio na matunda.Hii nchi ni yetu wote si ya kina fulani lazima kila mtu ainjoy matunda ya kazi anayofanya sio kuifanyia kazi serikali tu na yenyewe ifanye biashara basi si kuumiza wananchi.Maana akiumia huyu wa kipato cha kati cha chini si ndo kwishe.Hekima ni bora kuliko..........
Umeni quote vibaya mdau, napenda sana wafanyabiashara walipe kodi ila sio kwa mtindo huo wanaotaka kuanza TRA kuweka VAT kwenye transit goods,
Kwani hakuna sheria ya kodi kama hiyo duniani.
Na ndio mana nikatoa angalizo kwamba TRA wanatakiwa watumie vizur matamko anayotoa Raisi JPM kuhusu kukusanya kodi
 
Mimi ninachojua kama ni mzigo wa transit documents zinaonyesha clear, kwamba mpokeaji wa mwisho ni nani na mtumaji ni nani,
Nchi zote transit goods uwa hakuna kodi kabisa, ata ukisafiri nje ukanunua vitu kama camera au simu ukatunza risiti siku ya kuondoka airport unarudishiwa kodi yote.
Trucks zote zinazokwenda nje kwa sasa zina car trucking, kwa hiyo kushusha mzigo njiani kwa sasa naona ni ngumu.
Clearing Agent anatakiwa kulipa labda agency fee sababu ni mapato yake, lakini ata hiyo wakati mwingine ni ngumu sababu huo mzigo unatwishwa mtu wa nje.
Mimi naona mizigo ya nje wangeacha kutoza kodi kabisa maana uko bandarini mpaka mzigo utoke kuna tozo chungu nzima,
 
Msemaji wa TRA Richard Kayombo ameshaweka sawa hii taarifa kuhusu TRA kuweka VAT kwenye transit goods kwani amesema hiyo taarifa haina ukweli, na pia amesema wananchi wanatakiwa waelewe kwamba VAT imeongezwa kwenye huduma wanayotoa wakala wa forodha kwa maana ya TAFFA na TATTOA bali haijawekwa katika transit goods kama watu walivyoamini awali. Hivyo ule mjadala mkubwa uliokuwa asubuh ni mabishano kati ya TRA na mawakala wa forodha TAFFA wakipinga kuongezewa kodi ya ongezeko la thamani na TRA kwa huduma wanazotoa za clearing and forwarding kwa transit goods.
 
Msemaji wa TRA Richard Kayombo ameshaweka sawa hii taarifa kuhusu TRA kuweka VAT kwenye transit goods kwani amesema hiyo taarifa haina ukweli, na pia amesema wananchi wanatakiwa waelewe kwamba VAT imeongezwa kwenye huduma wanayotoa wakala wa forodha kwa maana ya TAFFA na TATTOA bali haijawekwa katika transit goods kama watu walivyoamini awali. Hivyo ule mjadala mkubwa uliokuwa asubuh ni mabishano kati ya TRA na mawakala wa forodha TAFFA wakipinga kuongezewa kodi ya ongezeko la thamani na TRA kwa huduma wanazotoa za clearing and forwarding kwa transit goods.
Hapa naona aliyoongea Kayombo na wewe uelewa wenu uko sawa na ndio maana mnaelewana. Sasa ni kwa nini hii kitu inasumbua vichwa vya hata maprofesa nguli wa vyuo vikuu!? Hivi hii kodi on transit inatozwa hivi katika nchi zingine!?
Mwanzoni sikumuelewa JPM alivyokuja na wazo la outsourcing ya nguvukazi kutoka Rwanda lakini sasa naanza kuelewa na punde wengi tutaelewa mantiki yake.
 
Hapa naona aliyoongea Kayombo na wewe uelewa wenu uko sawa na ndio maana mnaelewana. Sasa ni kwa nini hii kitu inasumbua vichwa vya hata maprofesa nguli wa vyuo vikuu!? Hivi hii kodi on transit inatozwa hivi katika nchi zingine!?
Mwanzoni sikumuelewa JPM alivyokuja na wazo la outsourcing ya nguvukazi kutoka Rwanda lakini sasa naanza kuelewa na punde wengi tutaelewa mantiki yake.
Acha kukalili mambo kuhusu maproffesor wa vyuo vikuu,
Alichosema Kayombo ni kwamba VAT imewekwa kwa watu wanaotoa huduma ya transit goods yani mawakala wa forodha na sio mizigo ya transit.
Unatakiwa utofautishe kati ya VAT kwenye huduma za transit goods na VAT kwenye mizigo transits
Kila la kheri.
 
Acha kukalili mambo kuhusu maproffesor wa vyuo vikuu,
Alichosema Kayombo ni kwamba VAT imewekwa kwa watu wanaotoa huduma ya transit goods yani mawakala wa forodha na sio mizigo ya transit.
Unatakiwa utofautishe kati ya VAT kwenye huduma za transit goods na VAT kwenye mizigo transits
Kila la kheri.
Kwa hiyo ukipewa ankara za bandarini na kuwekewa VAT ni gharama ya agent au mwenye mzigo!?
Kujifunza ni kuzuri, tumuulize aliyeko Beira, Mombasa, Durban nk ...kwenye ankara zao za bandari wanaweka VAT?, wakisema 'ndiyo' basi huyo Ngatunga akalale lakini wakisema 'hapana' basi tukubaliane na JPM kuleta wataalamu wa kuiendesha TRA kutoka Rwanda.
 
Kwa hiyo ukipewa ankara za bandarini na kuwekewa VAT ni gharama ya agent au mwenye mzigo!?
Kujifunza ni kuzuri, tumuulize aliyeko Beira, Mombasa, Durban nk ...kwenye ankara zao za bandari wanaweka VAT?, wakisema 'ndiyo' basi huyo Ngatunga akalale lakini wakisema 'hapana' basi tukubaliane na JPM kuleta wataalamu wa kuiendesha TRA kutoka Rwanda.
Acha kukalili mdau, mda mwingine penda kujifunza usichokijua kwamba kilichoongezwa VAT ni huduma wanayotoa wakala wa forodha kwa shughuli zao za clearing and forwarding na sio VAT kuongezwa kwenye transit goods.
Nafikiri lengo la serikali kuongeza VAT kwenye kampuni zinazotoa huduma za forodha ni kupunguza idadi ya kampuni nyingi ndogo za forodha ili kuweza kupunguza mianya ya ukwepaji kodi bandarini.
 
Acha kukalili mdau, mda mwingine penda kujifunza usichokijua kwamba kilichoongezwa VAT ni huduma wanayotoa wakala wa forodha kwa shughuli zao za clearing and forwarding na sio VAT kuongezwa kwenye transit goods.
Nafikiri lengo la serikali kuongeza VAT kwenye kampuni zinazotoa huduma za forodha ni kupunguza idadi ya kampuni nyingi ndogo za forodha ili kuweza kupunguza mianya ya ukwepaji kodi bandarini.
haya bwana mkuu nimekubali. Usisahau kwamba huu uelewa wako ndio wengi wanautegemea katika kujenga Tanzania ya viwanda!
Nakukumbusha tu kuwa makampuni mengi yaliyotuhumiwa na serikali hii hii ya JPM kukwepa kodi na kuiba makontena bandarini hakukuwa hata na kampuni moja ndogo.
 
Back
Top Bottom