Mtz kwanza
Member
- Sep 5, 2021
- 7
- 2
Afisa Mtendaji kata ya Lulembela, wilaya ya Mbogwe, mkoa wa Geita amekuwa Mungu mtu kwa kutisha na kulazimisha wananchi na watumishi kutoa mchango wa maendeleo bila staha na kuzingatia utu wa mtu.
Anamtumia balozi wa nyumba kumi anayeitwa Benard Gwanguru ambaye amekuwa akiambatana na mgambo muda wote
kuwatisha na kuwalazimisha wananchi na watumishi kuchangia mchango kiasi cha elfu kumi na mbili (12000/=) kwa lazima.
Kinachosikitisha ni kwamba hakuna maelezo yanayojitosheleza, wala kikao kilichoitishwa na afisa mtendaji huyu na balozi huyu kuwaeleza wananchi na watumishi katika vituo vyao vya kazi kuhusu mchango huo, zaidi afisa mtendaji huyo na balozi huyo wakiulizwa wanasema ni agizo linalohitaji wananchi na watumishi wachangie mchango huo bila kufafanua agizo hilo limetoka wapi.
Pia mchango unaolazimishwa unabagua watumishi ambapo watumishi wanaoishi katika nyumba za serikali (quaters) hawapaswi kuchangia wakati watumishi wanaoishi uraiani wanalazimishwa kuchangia mchango huo, swali ambalo ukiwauliza kwa nini watumishi wengine wachangie na wengine wasichangie afisa mtendaji huyo na balozi huyo hawana majibu.
Watumishi wanaohoji mchango huo huandikiwa wito "Summons" na afisa mtendaji huyo akiwataka kuhudhuria katika ofisi ya kata ya Lulembela kwa kosa linaloandikwa "KUPINGA MAENDELEO" ambapo kwa waliowahi kuitika wito huo hulazimishwa kuchanga mchango huo kwa kufungiwa na kuteswa katika ofisi ya afisa mtendaji huyo.
Kwa upande wa watumishi hali hii inaathiri molali yao ya utendaji kazi ikiwemo kupunguza mahudhurio ya watumishi katika vituo vyao vya kazi kwa kuhofia kukamatwa.
Dhamira ya Serikali ya Mheshimiwa Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan imejikita katika kuwapunguzia wananchi na watumishi mzigo kwa kutengeneza mazingira rafiki ya ulipaji kodi bila vitisho na kuathiri utendaji kazi wa wananchi na watumishi. Lakini kwa huyu afisa mtendaji kata ya Lulembela ni tofauti kabisa.
Mheshimiwa Ummy Mwalimu Waziri wa Tamisemi alitoa ufafanuzi juu ya uchangishaji michango ya maendeleo alipotembelea wilaya ya Sengerema August mwaka huu lakini kinachoonekana kwa afisa mtendaji na huyu balozi wa nyumba kumi hawakuelewa alichosema mheshimiwa waziri kutowalazimisha wananchi kuchangia michango ya maendeleo.
Wananchi na watumishi wa kata ya Lulembela tunaomba mamlaka zinazohusika zifuatilie suala hili la afisa mtendaji kata ya Lulembela na balozi wa nyumba kumi aliyetajwa kulazimisha wananchi na watumishi kuchangia mchango bila kuwaelewesha ili kuondoa usumbufu na taharuki kwa wananchi na watumishi wa kata hii.
Anamtumia balozi wa nyumba kumi anayeitwa Benard Gwanguru ambaye amekuwa akiambatana na mgambo muda wote
kuwatisha na kuwalazimisha wananchi na watumishi kuchangia mchango kiasi cha elfu kumi na mbili (12000/=) kwa lazima.
Kinachosikitisha ni kwamba hakuna maelezo yanayojitosheleza, wala kikao kilichoitishwa na afisa mtendaji huyu na balozi huyu kuwaeleza wananchi na watumishi katika vituo vyao vya kazi kuhusu mchango huo, zaidi afisa mtendaji huyo na balozi huyo wakiulizwa wanasema ni agizo linalohitaji wananchi na watumishi wachangie mchango huo bila kufafanua agizo hilo limetoka wapi.
Pia mchango unaolazimishwa unabagua watumishi ambapo watumishi wanaoishi katika nyumba za serikali (quaters) hawapaswi kuchangia wakati watumishi wanaoishi uraiani wanalazimishwa kuchangia mchango huo, swali ambalo ukiwauliza kwa nini watumishi wengine wachangie na wengine wasichangie afisa mtendaji huyo na balozi huyo hawana majibu.
Watumishi wanaohoji mchango huo huandikiwa wito "Summons" na afisa mtendaji huyo akiwataka kuhudhuria katika ofisi ya kata ya Lulembela kwa kosa linaloandikwa "KUPINGA MAENDELEO" ambapo kwa waliowahi kuitika wito huo hulazimishwa kuchanga mchango huo kwa kufungiwa na kuteswa katika ofisi ya afisa mtendaji huyo.
Kwa upande wa watumishi hali hii inaathiri molali yao ya utendaji kazi ikiwemo kupunguza mahudhurio ya watumishi katika vituo vyao vya kazi kwa kuhofia kukamatwa.
Dhamira ya Serikali ya Mheshimiwa Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan imejikita katika kuwapunguzia wananchi na watumishi mzigo kwa kutengeneza mazingira rafiki ya ulipaji kodi bila vitisho na kuathiri utendaji kazi wa wananchi na watumishi. Lakini kwa huyu afisa mtendaji kata ya Lulembela ni tofauti kabisa.
Mheshimiwa Ummy Mwalimu Waziri wa Tamisemi alitoa ufafanuzi juu ya uchangishaji michango ya maendeleo alipotembelea wilaya ya Sengerema August mwaka huu lakini kinachoonekana kwa afisa mtendaji na huyu balozi wa nyumba kumi hawakuelewa alichosema mheshimiwa waziri kutowalazimisha wananchi kuchangia michango ya maendeleo.
Wananchi na watumishi wa kata ya Lulembela tunaomba mamlaka zinazohusika zifuatilie suala hili la afisa mtendaji kata ya Lulembela na balozi wa nyumba kumi aliyetajwa kulazimisha wananchi na watumishi kuchangia mchango bila kuwaelewesha ili kuondoa usumbufu na taharuki kwa wananchi na watumishi wa kata hii.