Afisa Elimu Wilaya ya Uyui, Jacob Makala: Tenda haki na tatua migogoro ya uongozi mashuleni acha kufunika kombe

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Oct 29, 2019
8,520
17,426
Wanabodi habari za asubuhi,

Leo naleta malalamiko ya baadhi ya wakuu wa shule za sekondari wilaya uyui! kumhusu Jakobo Makala huyu kama Afisa elimu wa Uyui!

Malalamiko makubwa yanatoka kwa Aliekuwa Mkuu wa shule Loya sekondari Ndugu Joseph Nduba! Huyu ndiye alisimamia ujenzi wa sekondari ya loya mwaka 2007 na kuifungua mwaka huo huo. Baada ya kuhudumu kwenye cheo hicho hadi mwaka 2011 Mzee aliwekwa pembeni na kupewa Ndugu Khalifa Khamisi hadi leo.

Huyu mzee amekuwa mwalimu wa kawaida tangu kipindi hicho hadi sasa. Japo aligoma kumkabidhi shule ndugu Khalifa na kusababisha mgogoro wa uongozi ambao unafukuta hadi leo kimya kimya. Ndugu Makala ondoa kero iliopo kwa kuwaondoa wote na kumleta Mkuu mwingine kwa sababu wote hawana sifa za kuwa wakuu wa shule kwa vigezo vya sasa.

Wote wana stashahada na sio shahada au degree kwa mujibu wa viwango vya sasa vya TAMISEMI. Acha kufunika kombe mwanaharamu apite tatua tatizo sio kulifunika. Mbona shule nyingine mmewatoa wakuu wenye diploma hapo loya mnasubiri nini?

Hamuoni mnamdhalilisha huyu mzee kwa kumfanya mwalimu wa kawaida wakati yeye ndio alioifungua shule? Mna maslahi gani hasa binafsi na kubakiza Wakuu wa shule ambao hawana vigezo vya kielimu? Je, ni rushwa maarufu kama fungu la kumi hapo Halmashauri ya Uyui?

Acheni kudhalilisha taaluma za watu! wengine mmewafedhehesha kwa kuwatoa kuwa hawana sifa kielimu halafu wengine wawili mmewakumbatia!

Badilikeni tatueni hili jipu kabla Wakuu wa shule mliowatoa kwa kukosa sifa hawajaenda mahakamani kufungua shauri.

Nimatumaini yangu kuwa sinto fahamu hii mtaitatua.

nikutakie kila heri kwenye majukumu yako ya kila siku.
 
Kuna shule sita zimeanza mmeteua wakuu tena lakini yule mzee mmemuacha na ule mgogoro bado unafukuta!!wanashindana kwa waganga kila siku!mara huyu atoe laki tatu ili aendelee kubaki halafu mzee na maono yake ya kila siku!!eti suala lipo kwa jpm ili alipwe stahiki zake!!!
 
Kuna shule sita zimeanza mmeteua wakuu tena lakini yule mzee mmemuacha na ule mgogoro bado unafukuta!!wanashindana kwa waganga kila siku!mara huyu atoe laki tatu ili aendelee kubaki halafu mzee na maono yake ya kila siku!!eti suala lipo kwa jpm ili alipwe stahiki zake!!!
Mkuu hao Wazee wote wezi hivi inakuwaje mtu alilie ukuu wa shule? ambayo ni mali ya serikali kama anapata mshahara kama mwalimu inatosha haya mambo ya kun'gan'gania ukuu ni uchawi hao wote wapigwe chini wawekwe vijana wasomi hiyo mijizee ikarogane mbele huko pambaf kabisa
 
Tatizo ni elim zao!halafu mmoja anatoa vihela pale halmashauri kwa maafisa elim!!!sasa inaonekana kuna nongwa kwa wale walioondolewa halafu wengine wakaachwa!!kazi kweli kweli!!!
 
ee amekuwa mwalimu wa kawaida tangu kipindi hicho hadi sasa. Japo aligoma kumkabidhi shule ndugu Khalifa na kusababisha mgogoro wa uongozi ambao unafukuta hadi leo kimya kimya. Ndugu Makala ondoa kero iliopo kwa kuwaondoa wote na kumleta Mkuu mwingine kwa sababu wote hawana sifa za kuwa wakuu wa shule kwa vigezo vya sasa.

Wote wana stashahada na sio shahada au degree kwa mujibu wa viwango vya sasa vya TAMISEMI. Acha kufunika kombe mwanaharamu apite tatua tatizo sio kulifunika. Mbona shule nyingine mmewatoa wakuu wenye diploma hapo loya mnasubiri nini?


Walimu wa maiak hii wanashughulika na vitu ambavyo ni trivial sana sijui kama wanapata muda wa kufikiri mambo muhimu makubwa yenye kustawisha jamii wanazozitumikia
 
Mkuu maxiplus!!!Hakuna ualimu siku hizi!ni dili tu zimebaki!!rushwa na kuumizana tu!!!Wapiga kazi wa kweli wanaonekana wanafiki na viherehere wazembe wanaonekana watu kisa rushwa!!!
 
Kuna shule sita zimeanza mmeteua wakuu tena lakini yule mzee mmemuacha na ule mgogoro bado unafukuta!!wanashindana kwa waganga kila siku!mara huyu atoe laki tatu ili aendelee kubaki halafu mzee na maono yake ya kila siku!!eti suala lipo kwa jpm ili alipwe stahiki zake!!!
Hapa inawezekana mtu anajifukiza kwa Corona ila ikaonekana Ni tunguli,Ina maana mmoja wapo ameshindwa kumnyang'anya mwenzake Haki ya kuishi🤣🤣🤣🤣😂😂😂
 
Itakuwa kale ka posho wanagawana,haiwezekani stashahada awe mkuu wa shule ilihali shahada na shahada ya uzamili ikiwapo.
Hiyo ni rushwa,achunguzwe huyo Afisa Elimu.
 
Seriously dunia ya leo usawa huu bado kuna walimu wanapigania ukuu wa shule badilikeni vijana badilikeni dunia sasa imrfunguka uko mashambani ndio sehemu pekee ya fursa nendeni bank chukueni pesa muwekeze kwenye kilimo cha mboga mboga matunda, ufugaji achaneni na kugombania ukuu wa shule mnapoteza muda kwa pesa ipi unayopiga hapo

Jikiteni kwenye ujasiliamali naimani uko loya ni kijijini baada ya mda wa masomo mko free nendeni shambani vijijini nguvu kazi IPO limeni mipunga uko mda huu tafuta masoko Fanya biashara, fugeni ng'ombe, mbuzi leteni mjini muuze limeni mapapai nk leteni mjini muuze acheni gombania vyeo acheni vijana wazeni kuzalisha pesa

MY TAKE
Uyo mzee naye shule siyo Mali yake hata kama kaifungua hana haki ya kuwa MKUU milele ile Mali ya umma aache ujinga eti nimefungua miye kwaiyo kwani Mali ya familia hiyo yeye ni mtendaji tu na ndio maana alikuwa analipwa mishahara so aache utoto, afisa elimu uyo mzee mpige pini hata usecond master au uhasibu hata SMT asingie au bodies ya shule asipate iwe fundisho kwa wengine maana kuna watu wanahisi ukuu wamezaliwa nao

Yani usihamishe mtu wala kubadilisha mtu acha wakae hapo hapo uone kipi kitatokea kwani ajabu nini ooh ana diploma ajabu nini

Yani REO mkoa na katibu tawala mkoa wa Tabora msibadilishe mtu hapo acheni hivyo hivyo waone maana kuna watu wanajiona wana haki sana zaidi ya wenzao wanakuja mpaka uku kuleta majungu sasa waacheni hivyo hivyo na uyo mzee ambiwe aache ujinga mtaanza ukaguzi wa mapato na matumizi kuanzia mwaka 2017 mpaka 2011 tunaimani hatochomoka so akijifanya kihele apewe kesi ya uhujumu uchumi tunaimani kupiga alipiga na ndio maana analilia ukuu anajua upigaji bado upon

Walimu ukuu wa shule njaa stress acheni fanyeni ujasiliamali
 
Mkuu REJESHO HURU utambue tatizo maafisa walifanya Reshufle wengine wakatolewa kwa vigezo vya elimu ndogo wakawekwa wengine!!sasa wale waliotemwa wanashangaa wale wachache wawili waliobaki wana sifa zile zile !sasa waliotolewa wanahoji kwanini wao walienguliwa kama wengine wamebaki na sifa zile zile???
 
Mkuu REJESHO HURU utambue tatizo maafisa walifanya Reshufle wengine wakatolewa kwa vigezo vya elimu ndogo wakawekwa wengine!!sasa wale waliotemwa wanashangaa wale wachache wawili waliobaki wana sifa zile zile !sasa waliotolewa wanahoji kwanini wao walienguliwa kama wengine wamebaki na sifa zile zile???
Tatizo lipo wapi kwani natumai wewe mwalimu ngoja nikuulize swali tangy muongozo utoke kuwa mkuu wa shule anatakiwa kuwa na degree je kuna kipi kimebadilika katika majukumu ya ukuu wa shule ambayo mwalimu mwenye elimu ya diploma hawezi yafanya

Majukumu ni Yale Yale Tamisemi walileta hoja hiyo kwa kuondoa person conflict kama hizi Mara nyingi viwango vya elimu ni tatizo hususan kwa mtu ambaye hana exposure hilo tatizo ndio linasumbua uko maofisini na staff elimu ya ni kwa faida yako wewe usiende sumbua watu eti miye sasa na degree nataka cheo au na diploma nataka cheo my friend majukumu mengine hizi degree diploma is nothing kabisa maana ni majukumu yenye uhitaji hekima na busara si degree wala diploma
 
Seriously dunia ya leo usawa huu bado kuna walimu wanapigania ukuu wa shule badilikeni vijana badilikeni dunia sasa imrfunguka uko mashambani ndio sehemu pekee ya fursa nendeni bank chukueni pesa muwekeze kwenye kilimo cha mboga mboga matunda, ufugaji achaneni na kugombania ukuu wa shule mnapoteza muda kwa pesa ipi unayopiga hapo


Brilliant fact
 
Back
Top Bottom