KBG SCORPION
Member
- Feb 25, 2022
- 23
- 21
Habari wanajukwaa,
Naomba niingie Moja Kwa moja kwenye mada.Tabia na mazoea ya afisa Elimu tajwa hapo juu haikubaliki ambapo afisa huyo pasi na aibu Wala hofu huagiza kila mkuu Wa shule kupeleka fedha kwake.
Mwezi huu kila mkuu Wa shule ya serikali katika wilaya ya Mbarali kaagizwa kupeleka Tshs.100,000/= .Madai ya fedha hizo Kwa wakuu Wa shule hayana barua isipokuwa anachokifanya ni kuwaagiza wenyeviti Wa wakuu Wa shule ngazi ya wilaya Kwa njia ya magrupu ya "Whatsapp".
Kama fedha au michango hii ya wakuu Wa shule kwenda kwake ni halali Kwa nin Haina barua inayotoa maagizo hayo?
Kwa vile fedha hiyo humfikia Kwa njia isiyo halali,je matumizi yake yatakuwa halali?
Tunaomba wahusika Kwa maana ya wateule wake na vyombo vya dola kuchukua hatua.Wakuu Wa shule hawafanyi majukumu Yao Kwa amani maana nafasi zao za madaraka zipo rehani.
Muwe na Dominika njema!
Naomba niingie Moja Kwa moja kwenye mada.Tabia na mazoea ya afisa Elimu tajwa hapo juu haikubaliki ambapo afisa huyo pasi na aibu Wala hofu huagiza kila mkuu Wa shule kupeleka fedha kwake.
Mwezi huu kila mkuu Wa shule ya serikali katika wilaya ya Mbarali kaagizwa kupeleka Tshs.100,000/= .Madai ya fedha hizo Kwa wakuu Wa shule hayana barua isipokuwa anachokifanya ni kuwaagiza wenyeviti Wa wakuu Wa shule ngazi ya wilaya Kwa njia ya magrupu ya "Whatsapp".
Kama fedha au michango hii ya wakuu Wa shule kwenda kwake ni halali Kwa nin Haina barua inayotoa maagizo hayo?
Kwa vile fedha hiyo humfikia Kwa njia isiyo halali,je matumizi yake yatakuwa halali?
Tunaomba wahusika Kwa maana ya wateule wake na vyombo vya dola kuchukua hatua.Wakuu Wa shule hawafanyi majukumu Yao Kwa amani maana nafasi zao za madaraka zipo rehani.
Muwe na Dominika njema!