Afghanistan: Marekani yamuua aliyepanga shambulizi katika Uwanja wa Kabul

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,500
9,279
Jeshi la Marekani limesema limemuua mtu anayedaiwa kupanga shambulizi kwenye uwanja wa ndege wa Kabul baada ya kufanya shambulizi la ndege isiyokuwa na rubani.

Operesheni hiyo ya usiku wa kuamkia Jumamosi ilimlenga mtuhumiwa wa kundi la wanamgambo lenye mafungamano na lile linalojiita Dola la Kiislamu, IS-K kwenye jimbo la mashariki Nangahar. Msemaji wa Kamandi Kuu ya Marekani, Bill Urban amesema dalili za awali zinaonesha kuwa wamemuua mlengwa na hakuna raia wowote waliouawa.

Shambulizi hilo limefanyika baada ya Rais Joe Biden kuapa kupambana na IS baada ya mashambulizi ya Alhamisi yaliyosababisha mauwaji ya wanajeshi 13 wa Marekani na takriban raia 79 wa Afghanistan. IS ilikiri kuhusika na shambulizi, huku kundi la Taliban likikanusha kuhusika kwa namna yoyote ile. Biden pia aliliagiza jeshi kufanya mashambulizi dhidi ya viongozi wa IS, pamoja na mali za kundi hilo.

Ama kwa upande mwingine, Marekani imesema itaendelea kuwaondoa raia wa Afghanistan kutoka uwanja wa ndege wa Kabul hadi dakika ya mwisho, licha ya kuwepo wasiwasi kuhusu mashambulizi zaidi ya kundi la IS.


DW
 
Jeshi la Marekani limesema limemuua mtu anayedaiwa kupanga shambulizi kwenye uwanja wa ndege wa Kabul baada ya kufanya shambulizi la ndege isiyokuwa na rubani.

Operesheni hiyo ya usiku wa kuamkia Jumamosi ilimlenga mtuhumiwa wa kundi la wanamgambo lenye mafungamano na lile linalojiita Dola la Kiislamu, IS-K kwenye jimbo la mashariki Nangahar. Msemaji wa Kamandi Kuu ya Marekani, Bill Urban amesema dalili za awali zinaonesha kuwa wamemuua mlengwa na hakuna raia wowote waliouawa.

Shambulizi hilo limefanyika baada ya Rais Joe Biden kuapa kupambana na IS baada ya mashambulizi ya Alhamisi yaliyosababisha mauwaji ya wanajeshi 13 wa Marekani na takriban raia 79 wa Afghanistan. IS ilikiri kuhusika na shambulizi, huku kundi la Taliban likikanusha kuhusika kwa namna yoyote ile. Biden pia aliliagiza jeshi kufanya mashambulizi dhidi ya viongozi wa IS, pamoja na mali za kundi hilo.

Ama kwa upande mwingine, Marekani imesema itaendelea kuwaondoa raia wa Afghanistan kutoka uwanja wa ndege wa Kabul hadi dakika ya mwisho, licha ya kuwepo wasiwasi kuhusu mashambulizi zaidi ya kundi la IS.


DW

ni nani anaewafadhili IS
 
ni nani anaewafadhili IS
Zaidi ni waislamu wenye imani kali kwa kile kinachoitwa "The Global Jihad" na wanalenga kufanya kila mmoja duniani awe muislamu kwa nguvu na pia wanadai ndivyo alivyoamuru mtume wao katika kitabu chao kinachoitwa Korani.
 
US kaishiwa mbinu
sasa anacheza michezo ya KITOTO
kwa hiyo now ataunga muungano na TALIBAN kuwapiga magaidi wa IS ama !!

huku TALIBAN anataka ikifika SEPTEMBER
majeshi ya kigeni yasepe ha ha ha
ngoja tuone hii SERIEZ itakuwa na EPISODE ngapi
 
US si inasemaga yenyewe inafuata rule of law?Kwanini haijamfikisha huyo gaidi mahakamani?Wale wa wazee wa haki za binadamu mko wapi?
 
Zaidi ni waislamu wenye imani kali kwa kile kinachoitwa "The Global Jihad" na wanalenga kufanya kila mmoja duniani awe muislamu kwa nguvu na pia wanadai ndivyo alivyoamuru mtume wao katika kitabu chao kinachoitwa Korani.
Kwa nini watumie bunduki na mabomu kueneza uislam?
 
Yaani Marekani kwa miaka 20 ilishindwa kufahamu kuwa Waafghanistan wataungana na Taliban kuchukua nchi pindi wakiondoka, ila ndani ya Masaa 24 wameweza wameweza kimtambua aliyelipua bomu. Interesting!
 
Kwa nini watumie bunduki na mabomu kueneza uislam?
Read this letter!
20210828_173225.jpg
20210828_173227.jpg
20210828_173229.jpg
 
IS ni kikundi kilichotumia mgongo wa dini ili kutaka kujiweka uhuru na dini zingine.

unaweza kushangaa taliban mwaka kesho kupigana na IS au mujahidini
Ukijadili hizi mambo usimsahau Mmarekani. Huyo ndiye aliyeunda/aliyaendeleza makundi yote hayo mawili, IS na Taliban. Kila mmoja akiwa rafiki,kisha adui kulingana na maslahi anayoyajua yeye. Unamuona USA kwa sasa ni kama hana ukali kwa Taliban. Na amewaachia nchi. Si kwamba US kashindwa kihivyo, kuna kitu hapo. Tuhesabu siku.
 
Jeshi la Marekani limesema limemuua mtu anayedaiwa kupanga shambulizi kwenye uwanja wa ndege wa Kabul baada ya kufanya shambulizi la ndege isiyokuwa na rubani.

Operesheni hiyo ya usiku wa kuamkia Jumamosi ilimlenga mtuhumiwa wa kundi la wanamgambo lenye mafungamano na lile linalojiita Dola la Kiislamu, IS-K kwenye jimbo la mashariki Nangahar. Msemaji wa Kamandi Kuu ya Marekani, Bill Urban amesema dalili za awali zinaonesha kuwa wamemuua mlengwa na hakuna raia wowote waliouawa.

Shambulizi hilo limefanyika baada ya Rais Joe Biden kuapa kupambana na IS baada ya mashambulizi ya Alhamisi yaliyosababisha mauwaji ya wanajeshi 13 wa Marekani na takriban raia 79 wa Afghanistan. IS ilikiri kuhusika na shambulizi, huku kundi la Taliban likikanusha kuhusika kwa namna yoyote ile. Biden pia aliliagiza jeshi kufanya mashambulizi dhidi ya viongozi wa IS, pamoja na mali za kundi hilo.

Ama kwa upande mwingine, Marekani imesema itaendelea kuwaondoa raia wa Afghanistan kutoka uwanja wa ndege wa Kabul hadi dakika ya mwisho, licha ya kuwepo wasiwasi kuhusu mashambulizi zaidi ya kundi la IS.


DW

Yaani USA auwe hasitaje hata jina, yaani drama zinazofanywa na USA afghanistan ni nyingi mno. Mtenegeneza matatizo yeye , mtafuta mtuhumiwa yeye, na mtafuta suluhu yeye. USA uwa akiua watu alio watengeneza uwa anawataja majina. Yaani kwa sasa huko afghanistan anacheza movie tu. Sasa amesha tengeneza kundi la kuadhibu Taliban kwa sababu ameona yeye hawawezi.
 
Back
Top Bottom