Afghanistan: Mamia wajitokeza ofisi ya kutoa passport baada ya Taliban kutangaza kurejesha huduma

Afghanistan wana deposit kubwa ya lithium duniani yenye thamani maelfu ya trilioni. Hao wamechukua nchi sasa hivi tu, mchina akiingia hapo soon utasikia watu wanazamia Afghanistan kutafuta maisha.
Unaweza kutuambia wapi mchina aliingia watu wakazamia kutafuta maisha, hata China kwenyewe hakuna anayeendapo na wenyewe tu wanakimbilia kwa wengine.
 
Marekakani ndiyo wamereta shida na co tareban ambayo nchi wameikuta iko na hali mbaya kiuchumi.
Lini Afghanistan ilikuwa na hali nzuri ya uchumi ukiondoa kipindi wamarekani walipokuwepo.

Hata wakati wa utawala wa kwanza wa Taliban kulikuwa na shida kibao, njaa na watu takriban milioni mbili walikuwa ni wakimbizi. Taliban ni shida.
 
Unaweza kutuambia wapi mchina aliingia watu wakazamia kutafuta maisha, hata China kwenyewe hakuna anayeendapo na wenyewe tu wanakimbilia kwa wengine.
Unafikiri nani anachimba mafuta Nchi za kiarabu? China ni major player kwenye Kampuni za uchimbaji. Ni kwamba tu hao jamaa wajanja wanajua kutumia rasilimali zao.

Hio lithium thamani yake ni matrilioni ya Dola hata kama kuna ufisadi kwa kanchi kadogo kama Afghanistan watatoboa.
 
Unafikiri nani anachimba mafuta Nchi za kiarabu? China ni major player kwenye Kampuni za uchimbaji. Ni kwamba tu hao jamaa wajanja wanajua kutumia rasilimali zao.

Hio lithium thamani yake ni matrilioni ya Dola hata kama kuna ufisadi kwa kanchi kadogo kama Afghanistan watatoboa.
Hujajibu nilicho kiongelea, uwepo wa China popote haumnufaishi mtu ni wao wenyewe kwa sababu ni watu wabinafsi sana.
 
Hujajibu nilicho kiongelea, uwepo wa China popote haumnufaishi mtu ni wao wenyewe kwa sababu ni watu wabinafsi sana.
Mkuu unaijua Trillioni dollar lakini? Trilioni kama 2300 za Kitanzania.

Tanzania budget yetu ni trilioni 30,
GDP ya Nchi kwa mwaka ni kama trilioni 150

Hivyo unaongelea budget ya Tanzania karibia miaka 70. Ni hela kubwa sana.

Wakiwa na mchimbaji muda utatuambia, watakuwa sio wenzentu.
 
Siku moja baada ya kutangazwa kuwa Hati za Kusafiria (Passport) zitaanza kutolewa, mamia ya wananchi wamejitokeza katika Ofisi hiyo

Huduma hiyo ilisitishwa baada ya Taliban kuchukua madaraka mwezi Agosti, hali ambayo ilipelekea wengi waliotaka kuondoka Nchini humo kushindwa

Kwa mujibu wa UN watu takriban 500,000 wamekimbia makazi yao miezi ya karibuni, na idadi inatazamiwa kuongezeka ikiwa huduma muhimu kama Afya zitaendelea kudorora

View attachment 1965701

View attachment 1965710

======

Hundreds of Afghans flocked to the passport office in Kabul on Wednesday, just a day after news that it would re-open this week to issue the documents, while Taliban security men had to beat back some in the crowd in efforts to maintain order.

Taliban officials have said the service will resume from Saturday, after being suspended since their takeover and the fall of the previous government in August, which stranded many of those desperate to flee the country.

"I have come to get a passport but, as you can see here, there are lots of problems, the system is not working," one applicant, Mahir Rasooli, told Reuters outside the office.

"There is no official to answer our questions here to tell us when to come. People are confused."

A spokesman for the Taliban officials running the passport department did not immediately respond to requests for comment.

Poverty and hunger have worsened since the Islamist movement took over Afghanistan, which already suffered from drought and the COVID-19 pandemic.

Half a million people have been displaced in recent months, the United Nations says, and the number will only grow if health services, schools and the economy break down.

Source: Reuters
Taliban wanaweza kuendesha nchi vizuri tu kama wataruhusu mambo ya kawaida ya maisha yaende bila kutumia ubabe.
 
Talibans kama Wana akili wangeruhusu watu kuondoka.Huenda hao diaspora wangeanza kutuma Hela nyumbani na kusaidia uchumi wa nchi.Ethiopia na Somalia zinajengwa na diasporas!
 
Mkuu unaijua Trillioni dollar lakini? Trilioni kama 2300 za Kitanzania.

Tanzania budget yetu ni trilioni 30,
GDP ya Nchi kwa mwaka ni kama trilioni 150

Hivyo unaongelea budget ya Tanzania karibia miaka 70. Ni hela kubwa sana.

Wakiwa na mchimbaji muda utatuambia, watakuwa sio wenzentu.
Amekwambia umwambie ni nchi gani China imewekeza watu ama Raia wakakimbilia kwenda kupata fursa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Amekwambia umwambie ni nchi gani China imewekeza watu ama Raia wakakimbilia kwenda kupata fursa

Sent using Jamii Forums mobile app
Swali ambalo nimemjibu middle east.

China kampuni yao ya Serikali ya Mafuta inaitwa Sinopec unaweza kui Google ipo karibia Nchi zote Za mafuta, kuanzia za Kiarabu mpaka za Asia kama Brunei.

Nafkiri unafahamu Kampuni kubwa Kabisa ya mafuta Duniani ambayo pia inachuana na makampuni kama Apple, Saudi Aramco, sasa Aramco na Sinopec Zina Muungano unaitwa Yanbu Aramco kwa ajili ya Ku refine Mafuta,

Same kwa Nchi nyengine Soma huu Uzi jinsi China anavyo dominate refiners
 
Swali ambalo nimemjibu middle east.

China kampuni yao ya Serikali ya Mafuta inaitwa Sinopec unaweza kui Google ipo karibia Nchi zote Za mafuta, kuanzia za Kiarabu mpaka za Asia kama Brunei.

Nafkiri unafahamu Kampuni kubwa Kabisa ya mafuta Duniani ambayo pia inachuana na makampuni kama Apple, Saudi Aramco, sasa Aramco na Sinopec Zina Muungano unaitwa Yanbu Aramco kwa ajili ya Ku refine Mafuta,

Same kwa Nchi nyengine Soma huu Uzi jinsi China anavyo dominate refiners
Unachanganya madesa chief. Oil refinery unaweza kufanya popote pale sio lazima iwe nchi inayotoa mafuta. Makampuni ya uchimbaji mafuta ya magharibi ndio yaliyowekeza middle east na kuzifanya zile nchi kuwa matajiri, si hivyo tu hadi leo ukanda ule makampuni ya magharibi ndio yamewekeza sana na utalii asilimia kubwa wanategemea nchi za magharibi sio China.

Ni ukweli ulio wazi maeneo mengi aliyowekeza China wenyeji huwa hawaoni faida, anza na Afrika tu hapa Namibia kuna migomo inayoendelea kwenye migodi ya uranium waliyowekeza, Congo wamefunga migodi miwili kwa kukiuka sheria za mazingira na za kazi, Zambia ndio hao na Tanzania hapa sijaona uwekezaji wowote wa maana wa mchina zaidi ya yeboyebo, Myanmar na Cambodia kuna uwekezaji mkubwa wa China lakini bado wamechoka.

Tunataka mchina awe mbadala wa nchi za magharibi lakini ni wazi China wanajirudisha nyuma wenyewe.
 
Unachanganya madesa chief. Oil refinery unaweza kufanya popote pale sio lazima iwe nchi inayotoa mafuta. Makampuni ya uchimbaji mafuta ya magharibi ndio yaliyowekeza middle east na kuzifanya zile nchi kuwa matajiri, si hivyo tu hadi leo ukanda ule makampuni ya magharibi ndio yamewekeza sana na utalii asilimia kubwa wanategemea nchi za magharibi sio China.

Ni ukweli ulio wazi maeneo mengi aliyowekeza China wenyeji huwa hawaoni faida, anza na Afrika tu hapa Namibia kuna migomo inayoendelea kwenye migodi ya uranium waliyowekeza, Congo wamefunga migodi miwili kwa kukiuka sheria za mazingira na za kazi, Zambia ndio hao na Tanzania hapa sijaona uwekezaji wowote wa maana wa mchina zaidi ya yeboyebo, Myanmar na Cambodia kuna uwekezaji mkubwa wa China lakini bado wamechoka.

Tunataka mchina awe mbadala wa nchi za magharibi lakini ni wazi China wanajirudisha nyuma wenyewe.
Najua kuna narrative unataka kuiweka hapo, kwani haiwezekani China aka invest Nchi A wakafanikiwa na Nchi B wasifanikiwe?

Personally nawafahamu watu na makampuni ya Uchimbaji Mafuta Oman ya Kichina miaka na Miaka. Na naweza ku backup kwa data kibao


Pia hata hizo kampuni za West mfano BP nazo kwa asilimia kadhaa zinamilikiwa na wachina Huko middle East.

Na ni muda sana Makampuni ya Kichina ya Petroli yame overtake hayo ya magharibi

17930.jpeg


Kama una data zinazopingana na hizi zilete, ila sio hizi za kina Zambia.
 
Najua kuna narrative unataka kuiweka hapo, kwani haiwezekani China aka invest Nchi A wakafanikiwa na Nchi B wasifanikiwe?

Personally nawafahamu watu na makampuni ya Uchimbaji Mafuta Oman ya Kichina miaka na Miaka. Na naweza ku backup kwa data kibao


Pia hata hizo kampuni za West mfano BP nazo kwa asilimia kadhaa zinamilikiwa na wachina Huko middle East.

Na ni muda sana Makampuni ya Kichina ya Petroli yame overtake hayo ya magharibi

17930.jpeg


Kama una data zinazopingana na hizi zilete, ila sio hizi za kina Zambia.
Mzee mafanikio ya Middle East hayatokani na China, hata hizo takwimu za makampuni makubwa huelezi kama hao petrochina na sinopec ndio wawekezaji wakubwa kwenye huo ukanda kwa leo. Hizo takwimu hazitaji operations za hizo kampuni ni wapi, na hiyo kampuni uliyoitaja inachimba mafuta Oman hatujui ina nguvu gani au ukubwa gani kwenye hiyo nchi. Tafuta takwimu zinazojibu maswali yaliyopo.

Labda nikukumbushe swali uliloulizwa ni kwamba utaje Nchi ambayo China amewekeza watu wakapakimbilia?

Kwanini hutaki tuizungumzie Zambia, basi tuongee kuhusu yanayoendelea Namibia.

China bado hana uwezo wa kuvutia watu wafanye kazi kwenye makampuni yao ni njaa tu ndio zinatufanya twende kwao. Tusiende mbali, taja kampuni yoyote ya kichina iliyopo Tanzania ambayo wabongo wanaikimbilia sababu ya maslahi mazuri?
 
Mzee mafanikio ya Middle East hayatokani na China, hata hizo takwimu za makampuni makubwa huelezi kama hao petrochina na sinopec ndio wawekezaji wakubwa kwenye huo ukanda kwa leo. Hizo takwimu hazitaji operations za hizo kampuni ni wapi, na hiyo kampuni uliyoitaja inachimba mafuta Oman hatujui ina nguvu gani au ukubwa gani kwenye hiyo nchi. Tafuta takwimu zinazojibu maswali yaliyopo.

Labda nikukumbushe swali uliloulizwa ni kwamba utaje Nchi ambayo China amewekeza watu wakapakimbilia?

Kwanini hutaki tuizungumzie Zambia, basi tuongee kuhusu yanayoendelea Namibia.

China bado hana uwezo wa kuvutia watu wafanye kazi kwenye makampuni yao ni njaa tu ndio zinatufanya twende kwao. Tusiende mbali, taja kampuni yoyote ya kichina iliyopo Tanzania ambayo wabongo wanaikimbilia sababu ya maslahi mazuri?
Nature ya mbongo akipenda CCM basi wanavyofanya Chadema vyote Vibaya, Akipenda Chadema basi wanavyofanya CCM vyote Vibaya. Kwetu hakuna kati na kati.

Nchi ngapi Marekani AMEZIHARIBU? Nchi ngapi Uingereza Ameziharibu, Nchi ngapi Ufaransa Ameziharibu? Sababu wameharibu je ina maanisha investment zao zote zina madhara kwa Nchi?

Link niliokupa imetaja hadi Maeneo Gani PetroChina wanachimba mafuta OMAN, ila unaipotezea na kuuliza swali hilo hilo.

Na hata ukitumia akili ya kuzaliwa huwezi kumiliki kampuni mbili kubwa zaidi za mafuta Duniani kwa kupewa Vitenda uchwara,

Hizi links za Matenda Makubwa Makubwa yenye Thamani ya Matrilioni ya Hela ambazo PetroChina na Kampuni Nyengine za China wanafanya Duniani.

-moja ya eneo kubwa la Uchimbaji mafuta Iraq kwa sasa

-Qatar block D

-UAE karibia Block 3

-saudia

Kifupi mkuu China siku nyingi wapo Middle East na wanafanya Project kubwa kubwa. Hivyo si kweli kila eneo anakokwenda China wananchi ni masikini.
 
China bado hana uwezo wa kuvutia watu wafanye kazi kwenye makampuni yao ni njaa tu ndio zinatufanya twende kwao. Tusiende mbali, taja kampuni yoyote ya kichina iliyopo Tanzania ambayo wabongo wanaikimbilia sababu ya maslahi mazuri?
Tanzania kampuni gani kubwa ya China Ime invest? Kipindi cha ujamaa kulikuwa na urafiki, Tazara na Project nyengine kubwa hazikuwa zikitoa Ajira na watu kuajiriwa?

Hawa machinga wa China ambao wamejaa siku hizi hawawezi kuwa level moja na Multi Billion corporations.

Unapoongelea projects za Matrilioni ya Hela unatakiwa ufananishe na projects nyengine kama hizo duniani, na sio kufananisha kiduka cha mchina ama viproject uchwara ambavyo kampuni hata haijulikani kimataifa.
 
Nature ya mbongo akipenda CCM basi wanavyofanya Chadema vyote Vibaya, Akipenda Chadema basi wanavyofanya CCM vyote Vibaya. Kwetu hakuna kati na kati.

Nchi ngapi Marekani AMEZIHARIBU? Nchi ngapi Uingereza Ameziharibu, Nchi ngapi Ufaransa Ameziharibu? Sababu wameharibu je ina maanisha investment zao zote zina madhara kwa Nchi?

Link niliokupa imetaja hadi Maeneo Gani PetroChina wanachimba mafuta OMAN, ila unaipotezea na kuuliza swali hilo hilo.

Na hata ukitumia akili ya kuzaliwa huwezi kumiliki kampuni mbili kubwa zaidi za mafuta Duniani kwa kupewa Vitenda uchwara,

Hizi links za Matenda Makubwa Makubwa yenye Thamani ya Matrilioni ya Hela ambazo PetroChina na Kampuni Nyengine za China wanafanya Duniani.

-moja ya eneo kubwa la Uchimbaji mafuta Iraq kwa sasa

-Qatar block D

-UAE karibia Block 3

-saudia

Kifupi mkuu China siku nyingi wapo Middle East na wanafanya Project kubwa kubwa. Hivyo si kweli kila eneo anakokwenda China wananchi ni masikini.
Unakwepa swali la msingi na unabadili taarifa kila mara. Kampuni ulizotaja kuwa zimewekeza hapo middle zina nguvu gani kuliko za magharibi au za waarabu wenyewe zilizopo hapo? Naona we umeleta tu kampuni zinazochimba huko lakini huelezi ukubwa wao kwenye hizo nchi?

Tuje kwenye mada, unataka kusema sasa hivi watu wanaenda middle East kutokana na huo uwekezaji wa mchina?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom