kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Mwanaume mmoja wa nchini Marekani mwenye rekodi ya kufikishwa mahakamani kwa makosa ya ubakaji, ameiaga dunia wakati akimbaka mwanamke mwenye umri wa miaka 77. |
Isabel Chavelo Gutierrez mwenye umri wa miaka 53 wa Tivoli, Texas nchini Marekani alisafiri umbali wa kilomita tatu kwa kutumia baiskeli na kwenda kumvamia nyumbani kwake na kumbaka bibi mwenye umri wa miaka 77 baada ya kumtishia kumuua kwa kutumia kisu. Taarifa ya polisi ilisema kuwa mbakaji huyo wakati akiendelea kumuingilia kinguvu bibi huyo alisimama kwa muda na kusema hajisikiii vizuri na aliamua kupumzika kwa muda. Baada ya dakika chache alisimama tena na kuendelea kumbaka bibi huyo na ghafla alidondoka chini na kuiga dunia. Taarifa ya polisi ilisema kuwa inaaminika mbakaji huyo alifariki dunia kutokana na shambulio la moyo baada ya kuendesha baiskeli umbali wa kilomita tatu kwenda kumbaka bibi huyo. Baada ya kuona mbakaji wake amedondoka chini amefariki dunia, bibi huyo alitoka nje na kukimbilia nyumbani kwa binti ambaye alipopewa taarifa hizo aliwaita polisi. Mwili wa Gutierrez ulichukuliwa na kupelekwa hospitali kwa uchunguzi zaidi. NIFAHAMISHE Tanzania news portal .: Habari za Tanzania :. |