Shark
JF-Expert Member
- Jan 25, 2010
- 29,459
- 29,153
Habari za Asubuhi Kamanda Kova,
Ni matumaini yangu hua unapitaga pitaga humu kwenye hili Jukwaa, au kama sio wewe basi vijana wako wanapitaga na kukuletea taarifa. Maana hata mara nyingi nakusikiaga ukilitaja hili Jukwaa.
Sasa mimi nina swali dogo tu kwako Afande wangu Kova, ni kuhusu wale vijana waliokamatwa Jana wakiandamana kutokea maeneo mbalimbali kuelekea zilipo ofisi za Makao Makuu ya Chama Cha Demokrasiana Maendeleo (CHADEMA). Wale waliokua wakidai eti wao ni wana-Chadema na eti kua wamehuzunika na kukasirika sana kwa Dkt Slaa kujitoa CHADEMA. NI kwamba tu nlikua naomba kujua kama wameshafikishwa mahakamani au bado maana ukweli hata mimi wale vijana walinisikitisha sana kuamua kuandamana bila kibali.
Swali au ombi langu hili linachagizwa zaidi na wale vijana wa 4U MOVEMENT ambao walikua wamekusanyika (inasemekana bila kibali) kukamatwa na kufikishwa Polisi kisha mahakamani kwa haraka sana. Sasa niliomba tu kujua kama na hawa pia watapitia mkondo uleule wa vijana wale.
Afande wangu Kova naomba nieleweke tu sina nia ya kuingilia utendaji wa Jeshi lako la Polisi, bali ni ile tu sintofahamu niliyokumbana nayo juu ya vijana hawa, kwani kwa uelewa wangu mdogo naona kama hawa wana makosa makubwa zaidi kuliko wale wa kwanza. Wale walikutwa wamekusanyika tu, lakini hawa walikusanyika na wakaanza kutembea/kuandamaba.
Zaidi ya yote nakutakia utendaji mwema wa Jeshi lako la Polisi Kamanda wangu.
Wako,
Shark wa JamiiForums
Ni matumaini yangu hua unapitaga pitaga humu kwenye hili Jukwaa, au kama sio wewe basi vijana wako wanapitaga na kukuletea taarifa. Maana hata mara nyingi nakusikiaga ukilitaja hili Jukwaa.
Sasa mimi nina swali dogo tu kwako Afande wangu Kova, ni kuhusu wale vijana waliokamatwa Jana wakiandamana kutokea maeneo mbalimbali kuelekea zilipo ofisi za Makao Makuu ya Chama Cha Demokrasiana Maendeleo (CHADEMA). Wale waliokua wakidai eti wao ni wana-Chadema na eti kua wamehuzunika na kukasirika sana kwa Dkt Slaa kujitoa CHADEMA. NI kwamba tu nlikua naomba kujua kama wameshafikishwa mahakamani au bado maana ukweli hata mimi wale vijana walinisikitisha sana kuamua kuandamana bila kibali.
Swali au ombi langu hili linachagizwa zaidi na wale vijana wa 4U MOVEMENT ambao walikua wamekusanyika (inasemekana bila kibali) kukamatwa na kufikishwa Polisi kisha mahakamani kwa haraka sana. Sasa niliomba tu kujua kama na hawa pia watapitia mkondo uleule wa vijana wale.
Afande wangu Kova naomba nieleweke tu sina nia ya kuingilia utendaji wa Jeshi lako la Polisi, bali ni ile tu sintofahamu niliyokumbana nayo juu ya vijana hawa, kwani kwa uelewa wangu mdogo naona kama hawa wana makosa makubwa zaidi kuliko wale wa kwanza. Wale walikutwa wamekusanyika tu, lakini hawa walikusanyika na wakaanza kutembea/kuandamaba.
Zaidi ya yote nakutakia utendaji mwema wa Jeshi lako la Polisi Kamanda wangu.
Wako,
Shark wa JamiiForums
Last edited by a moderator: