Shabdullah
Member
- Feb 17, 2020
- 65
- 52
Habari zenu wana jamii forum.
Pili poleni kwa msiba wa kitaifa.
Nimekuja kwenu kuiongelea ishu ilotokea juzikati kama kichwa cha habari kinavosomeka. Bila ya shaka ishu hii inamuhusu afande sele na mungu na sheikh nurdeen kishki na mungu wake (allah)
Nimefanikiwa kuzisikiliza pande zote mbili, na pia nimesikiliza watoa maoni wa pande zote mbili na nilichogundua ni kuwa watu wanachanganya kati ya uhuru wa kuabudu na kuheshimu dini , na pia baadhi ya watu kukurupuka kutoa maono yao binafsi na kusahau kuwa kila dini ina muongozo wake.
Kwanza nivyema kabla ya kuchangia chochote kwa upande wowote ni lazima ujue afande sele dini yake ni ipi na sheikh dini yake ni ipi?. Yaani usiitolee maoni dini ambayo huijui na huelewi sheria zake., Pili ujue afande sele amemtukana mungu yupi?
Afande sele alimtukana mungu , mungu ambe hajamtaja jina lake haswa ila alongea maneno kama
"mungu",
"god",
"jitu lisilo ona",
na mengineyo.
Pia alitaja sifa za mungu huyo ni:
Haonekani
Hasikii
Hatendi
Anauwa watu tu
Lipo lipo tu.
Muungu wa wazungu
Pia alitaja miungu yake anayoiamini nayo ni:-
Jua
Ng'ombe
Bange
Ila pia alitoa matusi makubwa sana japo kuwa matusi hayo baadhi ya watu hutukanana kawaida na hakuna reaction yyte ile.
Pia afande sele aliomba ushuhuda kuwa anaeamini kama mungu yupo basi apige magoti aombe kuwa yeye (afande sele) afe kama kweli atakufa.
Lakini pia akamalizia kwa kutoa sababu ya kusema aliyoyasema kuwa ni kwasababu ya kifo cha raisi.
Masuala hayo yote ni mazito kwa wale wanaoamini uwepo wa mungu, afande sele hakutaja jina la mungu kwahio kila dini inapaswa kutafakari juu ya kauli ile na matusi yale kwa mungu wake.
Seikh kishki aliongea kulingana na dini yake na kwa jina la mungu wake, so kama huamini uwepo wa mungu ni vyema usichangie kwenye hilo pia kama huamini dini ya uislam ni vyema uongee kulingana na dini yako tu na wala sio kumtoa makosa sheikh ambae itikadi yake haiendani na yako.
Ni kweli nurdiin kishki aliongea kwa jazba na yeye mwenyewe aliliongelea hilo na alimuomba mungu kutokana na jazba hizo.
Nurdiin kishki alimuombea afande sele kifo kma alivoomba mwenyewe kuwa "anaeamini kama mungu yupo basi apige magoti aombe kuwa yeye (afande sele) afe kama kweli atakufa"
Pia sheikh nurdeen alimuomba mungu amuuwe kabla ya ramadhani na amuue kifo kibaya sana na amuangamize. Maneno haya ameyaongea akiwa na jazba na ni kutokana na uzito wa maneno aliyoyasikia kutoka kwenye clip ya afande sele kulingana na imani yake.
Pia sheikh huyu akasema kuwa "sisi tumeudhika tumeumia kutokana na matusi ya huyu jamaa" na akasema kuwa "hatuumii hakika {kwasababu} sisi tunakupenda" aliongezea kwa kusema "yaarabbi tuma jeshi lako kumteketeza huyo mja wako" pia akaomba kwa mungu wake kuwa "nasisi atusamehe kama tumekosea kumuombea dua ya kumteketeza na kumlaani vikali huyu mja wako",
Na alisema kuwa raisi magufuli alikua ni kimbe tu kma viumbe wengine na isiwe sababu ya mipasuko katika taifa hili.
Kiukweli sheikh aliomba dua kwa mungu wake , sheikh huyu hakumuhukumu afande sele sheikh huyu aliomba dua kwa mungu wake ili amuhukumu kiumbe huyu kwa jinsi alivyomtukana mungu,
Kufa kila mtu ata kufa na ni dua aliyomuombea na ndo clip ambayo inatawala kwenye social media na watu kumkisia vikali sheikh kwa kusema kuwa sheikh amekosea zaidi kuliko afande sele, wakasahau kuwa afande sele ndo kasema aombewe afe na sio takwa la sheikh, hilo ni ushuhuda wa afande sele ambao anataaka kuona na kuamini kuwa kweli mungu yupo.
Inashangaza kuona watu wakimkosoa vikali sheikh na wakiacha imani zao zinasemaje na wengine kukosoa kulingana na imani zao lakini wakisahau kuwa wapo na imani tofauti na sheikh.
Watanzania tunapenda kupokea clip fupi fupi ambazo zinaleta maana ya lile tunalolitaka sisi tu na hapo tunatoa comment zetu bila kujua mbeleni kunaongelewa nini au nyuma kumeongelewa nini.
Tujue kuwa kuna uhuru wa kuabudu lakini pia kuna haki ya kuabudu
Pili poleni kwa msiba wa kitaifa.
Nimekuja kwenu kuiongelea ishu ilotokea juzikati kama kichwa cha habari kinavosomeka. Bila ya shaka ishu hii inamuhusu afande sele na mungu na sheikh nurdeen kishki na mungu wake (allah)
Nimefanikiwa kuzisikiliza pande zote mbili, na pia nimesikiliza watoa maoni wa pande zote mbili na nilichogundua ni kuwa watu wanachanganya kati ya uhuru wa kuabudu na kuheshimu dini , na pia baadhi ya watu kukurupuka kutoa maono yao binafsi na kusahau kuwa kila dini ina muongozo wake.
Kwanza nivyema kabla ya kuchangia chochote kwa upande wowote ni lazima ujue afande sele dini yake ni ipi na sheikh dini yake ni ipi?. Yaani usiitolee maoni dini ambayo huijui na huelewi sheria zake., Pili ujue afande sele amemtukana mungu yupi?
Afande sele alimtukana mungu , mungu ambe hajamtaja jina lake haswa ila alongea maneno kama
"mungu",
"god",
"jitu lisilo ona",
na mengineyo.
Pia alitaja sifa za mungu huyo ni:
Haonekani
Hasikii
Hatendi
Anauwa watu tu
Lipo lipo tu.
Muungu wa wazungu
Pia alitaja miungu yake anayoiamini nayo ni:-
Jua
Ng'ombe
Bange
Ila pia alitoa matusi makubwa sana japo kuwa matusi hayo baadhi ya watu hutukanana kawaida na hakuna reaction yyte ile.
Pia afande sele aliomba ushuhuda kuwa anaeamini kama mungu yupo basi apige magoti aombe kuwa yeye (afande sele) afe kama kweli atakufa.
Lakini pia akamalizia kwa kutoa sababu ya kusema aliyoyasema kuwa ni kwasababu ya kifo cha raisi.
Masuala hayo yote ni mazito kwa wale wanaoamini uwepo wa mungu, afande sele hakutaja jina la mungu kwahio kila dini inapaswa kutafakari juu ya kauli ile na matusi yale kwa mungu wake.
Seikh kishki aliongea kulingana na dini yake na kwa jina la mungu wake, so kama huamini uwepo wa mungu ni vyema usichangie kwenye hilo pia kama huamini dini ya uislam ni vyema uongee kulingana na dini yako tu na wala sio kumtoa makosa sheikh ambae itikadi yake haiendani na yako.
Ni kweli nurdiin kishki aliongea kwa jazba na yeye mwenyewe aliliongelea hilo na alimuomba mungu kutokana na jazba hizo.
Nurdiin kishki alimuombea afande sele kifo kma alivoomba mwenyewe kuwa "anaeamini kama mungu yupo basi apige magoti aombe kuwa yeye (afande sele) afe kama kweli atakufa"
Pia sheikh nurdeen alimuomba mungu amuuwe kabla ya ramadhani na amuue kifo kibaya sana na amuangamize. Maneno haya ameyaongea akiwa na jazba na ni kutokana na uzito wa maneno aliyoyasikia kutoka kwenye clip ya afande sele kulingana na imani yake.
Pia sheikh huyu akasema kuwa "sisi tumeudhika tumeumia kutokana na matusi ya huyu jamaa" na akasema kuwa "hatuumii hakika {kwasababu} sisi tunakupenda" aliongezea kwa kusema "yaarabbi tuma jeshi lako kumteketeza huyo mja wako" pia akaomba kwa mungu wake kuwa "nasisi atusamehe kama tumekosea kumuombea dua ya kumteketeza na kumlaani vikali huyu mja wako",
Na alisema kuwa raisi magufuli alikua ni kimbe tu kma viumbe wengine na isiwe sababu ya mipasuko katika taifa hili.
Kiukweli sheikh aliomba dua kwa mungu wake , sheikh huyu hakumuhukumu afande sele sheikh huyu aliomba dua kwa mungu wake ili amuhukumu kiumbe huyu kwa jinsi alivyomtukana mungu,
Kufa kila mtu ata kufa na ni dua aliyomuombea na ndo clip ambayo inatawala kwenye social media na watu kumkisia vikali sheikh kwa kusema kuwa sheikh amekosea zaidi kuliko afande sele, wakasahau kuwa afande sele ndo kasema aombewe afe na sio takwa la sheikh, hilo ni ushuhuda wa afande sele ambao anataaka kuona na kuamini kuwa kweli mungu yupo.
Inashangaza kuona watu wakimkosoa vikali sheikh na wakiacha imani zao zinasemaje na wengine kukosoa kulingana na imani zao lakini wakisahau kuwa wapo na imani tofauti na sheikh.
Watanzania tunapenda kupokea clip fupi fupi ambazo zinaleta maana ya lile tunalolitaka sisi tu na hapo tunatoa comment zetu bila kujua mbeleni kunaongelewa nini au nyuma kumeongelewa nini.
Tujue kuwa kuna uhuru wa kuabudu lakini pia kuna haki ya kuabudu