Analyse
JF-Expert Member
- Jan 19, 2014
- 16,384
- 41,394
Unajua mahusiano yanachangamoto nyingi sana, na hazifanani. Kila mmoja kwa sehemu yake anapitia changamoto katika mahusiano. Sasa inapotokea umefanyiwa mabaya na mtu uliyenae kwenye mahusiano, sio jambo zuri kuyaweka wazi mabaya yake hasa kwa ndugu zako au watu wako wa karibu sana.
Unajua mapenzi yana nguvu sana, kuna baadhi ya scenarios zinatokea kwa watu hadi unajisemea kwamba "its over between these two" lakini unakuja kuwa surprised after awhile unakuta wako pamoja as if nothing happened.
Nina jamaa yangu ashawahi mkuta mpenz wake amebananishwa uchochoroni na jamaa, ilikuwa usiku tunatoka kuangalia mpira, na kama tungechelewa kidogo tungekuta wanafanya mapenzi. Jamaa alikuwa disappointed sana kiasi kwamba nikajua ndo mwisho wa penzi lao, ila after siku kadhaa naona wako pamoja as if nothing happened. Sikumshangaa jamaa,japo yule Shem wangu Wala simchangamkii kama ilivyokuwa zamani.
Point ya kuandika huu uzi ni kwamba, ikitokea umegombana na mtu ambae uko nae katika serious relationship, tena ikiwa amekufanyia Yale mambo ambayo hayavumiliki, nakusihi hutakiwi kuyaanika mabaya yake Kila sehemu, maana kesho ni fumbo.
Ikitokea unahitaji msaada wa kiushauri, mawazo na counseling, jitahidi kuwa mchaguzi wa watu wa kuwaambia, sio Kila anayekuuliza kulikoni? Basi wewe unammwagia file Zima la mtu wako alichofanya. Kuna watu wanabeba matatizo yetu kwa uzito sana.
Kuna wale watu ambao kipindi upo kwenye mapito ndio waliokuwa faraja Yako, ndio waliokuwa wanahakikisha hujidhuru, wanahakikisha furaha yako inarudi, so ikitokea wewe umemsamehe, wao wanaweza wasimsamehe. Na kutomsamehe kwao kunatokana na kumbukumbu zao jinsi ulivyokuwa unapitia hali ngumu sababu ya huyo mtu wako. Au jinsi wao walivyokuwa hawafanyi mambo yao kwa uhuru ilimradi kuhakikisha wanakufariji wewe.
Wewe utampa second chance,ila wao hawatakaa wampe hiyo nafasi. Na inawezekana wasimpe tena ule uzito waliokuwa wanampa awali.
That's All (Ni hayo Tu).
Analyse
Unajua mapenzi yana nguvu sana, kuna baadhi ya scenarios zinatokea kwa watu hadi unajisemea kwamba "its over between these two" lakini unakuja kuwa surprised after awhile unakuta wako pamoja as if nothing happened.
Nina jamaa yangu ashawahi mkuta mpenz wake amebananishwa uchochoroni na jamaa, ilikuwa usiku tunatoka kuangalia mpira, na kama tungechelewa kidogo tungekuta wanafanya mapenzi. Jamaa alikuwa disappointed sana kiasi kwamba nikajua ndo mwisho wa penzi lao, ila after siku kadhaa naona wako pamoja as if nothing happened. Sikumshangaa jamaa,japo yule Shem wangu Wala simchangamkii kama ilivyokuwa zamani.
Point ya kuandika huu uzi ni kwamba, ikitokea umegombana na mtu ambae uko nae katika serious relationship, tena ikiwa amekufanyia Yale mambo ambayo hayavumiliki, nakusihi hutakiwi kuyaanika mabaya yake Kila sehemu, maana kesho ni fumbo.
Ikitokea unahitaji msaada wa kiushauri, mawazo na counseling, jitahidi kuwa mchaguzi wa watu wa kuwaambia, sio Kila anayekuuliza kulikoni? Basi wewe unammwagia file Zima la mtu wako alichofanya. Kuna watu wanabeba matatizo yetu kwa uzito sana.
Kuna wale watu ambao kipindi upo kwenye mapito ndio waliokuwa faraja Yako, ndio waliokuwa wanahakikisha hujidhuru, wanahakikisha furaha yako inarudi, so ikitokea wewe umemsamehe, wao wanaweza wasimsamehe. Na kutomsamehe kwao kunatokana na kumbukumbu zao jinsi ulivyokuwa unapitia hali ngumu sababu ya huyo mtu wako. Au jinsi wao walivyokuwa hawafanyi mambo yao kwa uhuru ilimradi kuhakikisha wanakufariji wewe.
Wewe utampa second chance,ila wao hawatakaa wampe hiyo nafasi. Na inawezekana wasimpe tena ule uzito waliokuwa wanampa awali.
That's All (Ni hayo Tu).
Analyse