Adui wa Dereva barabarani ni Dereva mwenzie, sio Trafiki wala Polisi

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Adui zetu wakubwa barabarani sio Polisi bali ni Madereva wenzetu.

Kusema kweli adui zetu wakubwa barabarani ni madereva wenzetu kuliko hata hao Polisi tunaowaona maadui. Dereva anatumia nguvu nyingi kuchukua tahadhari dhidi ya Polisi kuliko hata dereva mwenzake. Kwa nini Polisi baadhi yetu tunawachukuliaga kama maadui na kimsingi si maadui zetu?

Polisi hata akikusimamisha:
1. Haumizi mguu wako na kukufanya mlemavu.
2. Haondoi uhai wako na kukufanya mfu.

Atakushughulikia kwa taratibu tu au hata kama atachukua chochote bado viungo vyako unabaki navyo na uhai wako unabaki nao. Sasa tuje kwa hawa wenzetu. Kwa nini tunasema maadui ni wenzetu tena tunaowaamimini?

Dereva mwenzio:
1. Hakawii kukuletea gari upande wako akakugonga ukapoteza mwelekeo.
2. Hakawii kuingilia nafasi yako barabarani kwa kuovateki bila umakini.
3. Hakawii kukugonga kwa nyuma kwa kufuata kwa karibu sana.
4. Hakawii kukuuzia tela uhangaike nalo.
5. Hakawii kuyumba na kuangusha mzigo ukaangukia gari lako kutokana na uzembe wa uendeshaji au kufunga mzigo.
6. Hakawii kukubania ili ukutane na kicheche.
7. Akimaliza kutengeneza gari haondoi mawe au miti ya tahadhari aliyoweka.
8. Gari lake limeharibika haweki tahadhari yoyote njiani.
9. Anakupiga na mwanga mkali wa taa na usione kabisaa.
10. Wakiongozana kama ni malori 5 hawaachi nafasi kabisa ya kuingia kati yao pale dereva mwingine anapo ovateki.
11. Ni dereva mwenzio ndiye anayekuchomekea kwa pupa zake barabarani.

Matokeo ya matendo hayo ni kukusababishia ulemavu au kifo. Mwogope dereva mwenzio, Usimwamini sana, jiamini wewe tu, chukua tahadhari dhidi yake.

Usalama Barabarani ni Jukumu Letu Sote.
 
Adui zetu wakubwa barabarani sio Polisi bali ni Madereva wenzetu.

Kusema kweli adui zetu wakubwa barabarani ni madereva wenzetu kuliko hata hao Polisi tunaowaona maadui. Dereva anatumia nguvu nyingi kuchukua tahadhari dhidi ya Polisi kuliko hata dereva mwenzake. Kwa nini Polisi baadhi yetu

Tofautisha dereva mjinga na dereva aliyeelimika.

Ajali: Tuambiane ukweli dhahama hili lituepuke

Ukimaliza hapo tambua polisi na jukumu la polisi:

"Atakushughulikia kwa taratibu tu au hata kama atachukua chochote bado viungo vyako unabaki navyo na uhai wako unabaki nao."

Hapa kama nawaona walivyokenua.

Unasomeka kuwa polisi traffic hatakushughulukia kwa mujibu wa jukumu lake kama polisi bali taratibu huku akichukua chochote.

Hawa ni kero sana kwa kuwageuza wananchi miradi yao huku wakiwabambikizia kesi Ili wapate zaidi.

Unaweza kujipanga kujiepusha na madereva hawa lakini si polisi.
 
Dereva pekee mwenye akili timamu barabarani ni wewe, wengine wote ona ni wendawazimu tu! Tuwe na udereva wa kujihami!

Udereva wa kujihami ni muhimu sana
Bahati mbaya wengi kwenye nguzo ya maamuzi ndio inawagharimu
Maana yangu ni kwamba wengi bado hawajui muda sahihi wa kufanya maamuzi.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Umesema kweli. Madereva wote wangefuata sheria za barabarani ajali zingepungua sana. Sasa unakuta mtu anaendesha huku amelewa ama anasinzia siyo kuhatarisha usalama na maisha yako tu bali pia kwa wengine watumiao barabara.

Unakuta kwenye Bar watu wamepaki magari yao really that's selfishness. Hizi zinapoteza sana maisha na kuwapa watu ulemavu wa kudumu.
 
Sifa nyingi hapo umewaelezea madereva wa serikali na mabasi!

Hao jamaa hu-overtake ovyo na kuja upande wako halafu li?wanakuwashia full mchana hiyo na honi juu!

Nikisimamishwa na traffic huwa najisikia ovyo hata kama anaomba lift tu.
 
Back
Top Bottom