EL+RA=UFISADI
Member
- Jul 4, 2010
- 56
- 6
Adui mkubwa wa CUF na NCCR ni CHADEMA, si CCM!:angry:
Imekaaje hii. Hivi hii ni kwa sababu ya njaa kali, kutokuwa na akili au wivu wa kitoto
(siblings rivalry?).
Inakuaje leo hii vyama vya siasa vya CUF na NCCR viione CHADEMA kama adui wake mkuu badala ya chama tawala CCM?
Taarifa zilio wazi zinaonesha kuwa viongozi wakuu wa CUF akiwemo Mwenyekiti wake Ibrahim Lipumba na aliyekuwa kiongozi wa upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohamed, na wengineo wana chuki kali sana na CHADEMA.
In fwact, CUF iko karibu sana na CCM na wako tayari kupokea maagizo kutoka chama tawala ili kuibomoa CHADEMA.
Angalia haya mambo:
1. Lipumba mara kadhaa amekiponda CHADEMA na alikuwa wa kwanza
kumpa mkono wa pongezi Kikwete wakati amejuwa fika kuwa aliiba
kura kwenye uchaguzi.
2. Hamad Rashid alionesha hasira, jazba na chuki binafsi dhidi ya
CHADEMA kwenye mdahalo wake na mwenyekiti wa CHADEMA Freeman
Mbowe. Pengine hii inatokana na yeye kutolewa kwenye ulaji wa kuwa kiongozi wa upinzani Bungeni baada ya ushindi wa CHADEMA kupata wabunge wengi.
3. Wabunge wa CUF walikuwa wako tayari kuona mtu wa CCM anakuwa spika wa Bunge badala ya CHADEMA. Hii imetokana na CUF kumpigia kura Anne Makinda kuwa Spika badala ya Mabere Marando wa CHADEMA. CUF walimpigia Makinda licha ya kutoa guarantee kwa maandishi kuwa CHADEMA kuwa watamuunga mkono Marando.
4. James Mbatia wa NCCR Mageuzi anakwenda mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi jimbo la ubunge Kawe ambapo Halima Mdee wa CHADEMA ameshinda. Lengo ni nini? Uchaguzi urudiwe ili CCM ishinde?
5. Siku zote CUF na NCCR wamekuwa wanazungumzia haja ya katiba mpya na tume huru ya uchaguzi. Baada ya kuona CHADEMA imessimama kidete kwenye harakati hizo, eti wao wanakaa pembeni.
Yaani huwa natamani nishike bakora niwachape hawa wasaliti wote wa demokrasia nchini kama CUF, NCCR, TLP, UDP na wengineo.
Kwa ufupi, wakati CHADEMA inapambana ili ichukue dola na kuongoza serikali, CUF na NCCR wanapambana kuwa chama kikuu cha upinzani chini ya utawala wa milele wa CCM.
Je tutafika? Kuna haja kweli ya kuwa na umoja wa vyama vya siasa wakati CUF na NCCR ziko mfukoni mwa mafisadi wa CCM?
Nadhani jawabu ni kuwa CHADEMA ndiyo chama pekee cha upinzani nchini ambacho hakijanunuliwa na CCM, suluhisho ni kwa chama hiki kiendelee jitahada zake peke yake kisipoteze muda na viongozi njaa wa CUF na NCCR Mageuzi.
Imekaaje hii. Hivi hii ni kwa sababu ya njaa kali, kutokuwa na akili au wivu wa kitoto
(siblings rivalry?).
Inakuaje leo hii vyama vya siasa vya CUF na NCCR viione CHADEMA kama adui wake mkuu badala ya chama tawala CCM?
Taarifa zilio wazi zinaonesha kuwa viongozi wakuu wa CUF akiwemo Mwenyekiti wake Ibrahim Lipumba na aliyekuwa kiongozi wa upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohamed, na wengineo wana chuki kali sana na CHADEMA.
In fwact, CUF iko karibu sana na CCM na wako tayari kupokea maagizo kutoka chama tawala ili kuibomoa CHADEMA.
Angalia haya mambo:
1. Lipumba mara kadhaa amekiponda CHADEMA na alikuwa wa kwanza
kumpa mkono wa pongezi Kikwete wakati amejuwa fika kuwa aliiba
kura kwenye uchaguzi.
2. Hamad Rashid alionesha hasira, jazba na chuki binafsi dhidi ya
CHADEMA kwenye mdahalo wake na mwenyekiti wa CHADEMA Freeman
Mbowe. Pengine hii inatokana na yeye kutolewa kwenye ulaji wa kuwa kiongozi wa upinzani Bungeni baada ya ushindi wa CHADEMA kupata wabunge wengi.
3. Wabunge wa CUF walikuwa wako tayari kuona mtu wa CCM anakuwa spika wa Bunge badala ya CHADEMA. Hii imetokana na CUF kumpigia kura Anne Makinda kuwa Spika badala ya Mabere Marando wa CHADEMA. CUF walimpigia Makinda licha ya kutoa guarantee kwa maandishi kuwa CHADEMA kuwa watamuunga mkono Marando.
4. James Mbatia wa NCCR Mageuzi anakwenda mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi jimbo la ubunge Kawe ambapo Halima Mdee wa CHADEMA ameshinda. Lengo ni nini? Uchaguzi urudiwe ili CCM ishinde?
5. Siku zote CUF na NCCR wamekuwa wanazungumzia haja ya katiba mpya na tume huru ya uchaguzi. Baada ya kuona CHADEMA imessimama kidete kwenye harakati hizo, eti wao wanakaa pembeni.
Yaani huwa natamani nishike bakora niwachape hawa wasaliti wote wa demokrasia nchini kama CUF, NCCR, TLP, UDP na wengineo.
Kwa ufupi, wakati CHADEMA inapambana ili ichukue dola na kuongoza serikali, CUF na NCCR wanapambana kuwa chama kikuu cha upinzani chini ya utawala wa milele wa CCM.
Je tutafika? Kuna haja kweli ya kuwa na umoja wa vyama vya siasa wakati CUF na NCCR ziko mfukoni mwa mafisadi wa CCM?
Nadhani jawabu ni kuwa CHADEMA ndiyo chama pekee cha upinzani nchini ambacho hakijanunuliwa na CCM, suluhisho ni kwa chama hiki kiendelee jitahada zake peke yake kisipoteze muda na viongozi njaa wa CUF na NCCR Mageuzi.