Uchaguzi 2020 Ado Shaibu: CHADEMA ni chama cha siasa. Kina haki ya kuandaa Wagombea Zanzibar

Zitto

Former MP Kigoma Urban
Mar 2, 2007
1,562
10,880
MAJIBU YA KATIBU MKUU WA ACT WAZALENDO ADO SHAIBU ALIPOULIZWA KUHUSU KAULI YA CHADEMA KUSIMAMISHA WAGOMBEA ZANZIBAR.

Kwenye Mkutano wake na waandishi wa habari, Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo Ndugu Ado Shaibu aliulizwa na waandishi wa habari kuhusu msimamo wa ACT Wazalendo baada ya CHADEMA kutangaza mchakato wa wagombea wa Urais Zanzibar.

Ado Shaibu: CHADEMA ni chama cha siasa. Kina haki ya kujiandaa na uchaguzi ikiwemo kuandaa wagombea wa ngazi zote sehemu yoyote ya nchi ikiwemo Zanzibar.

Ado Shaibu: Mara baada ya Katibu Mkuu wa CHADEMA kutangaza kufungua milango ya ushirikiano wa vyama, siku inayofuata nilimwandikia barua kupokea hatua hiyo kwa mikono miwili na kuonesha utayari wa ACT Wazalendo.

Ado Shaibu: Tunahitaji ushirikiano wa vya vyama vya upinzani na wapenda demokrasia wotr ili kuing'oa CCM madarakani 2020 na kuleta mabadiliko kwenye maisha ya wananchi.

Ado Shaibu: CCM haipendi umoja wa vyama vya upinzani. Itafanya kila njia kutugawanya. Sisi ACT Wazalendo tumetamka mara nyingi kuwa tupo tayari kwa umoja na tutasimamia hilo.

Imeandaliwa na:

Janeth Rithe, Naibu Katibu, Idara ya Habari, Uenezi na Mahusiano kwa Umma, ACT Wazalendo.
07 Juni 2020.
 
Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu. Unganeni tumtupe magufuli kando.

Hii dhana ni njema kinadharia, 2015 kulikuwa na Ukawa, yenye cdm, cuf, Nld na Nccr. Leo hii Cuf na Nccr wako wapi? Cdm ndio chama chenye nguvu kwenye upinzani ila kuna tatizo la ubinafsi, na Act wako tayari kwa umoja, ila historia yao ya 2015, na tofauti/kutokuaminiana kwa Mbowe na Zito ni tatizo la dhahiri. Ni ngumu kukataa uanzishwaji wa ACT na mkono wa ccm, tena hiyo ACT ni kama mtoto wa nje wa ccm aliyepatikana kutokana na ugomvi wa Zito na Mbowe/cdm.

Cdm na Act ndio vyama vinavyoweza kuungana ili kutoa ushindani stahiki dhidi ya CCM. Je wako tayari kuondoa tofauti zao hasa zinazoendana na historia zao? Hili ni suala litakalopata majibu kulingana na muda. Ila tatizo la msingi kwangu sio kuungana, bali tume ya uchaguzi ilivyo na matumizi mabaya ya madaraka ya Magufuli itakuwaje? Ikumbukwe sasa hivi Magufuli anachezea katiba kupata kinga, lengo ni ili kupata uhalali wa kuchezea chaguzi za nchi hii.
 
Ulikuwa wapi siku zote kukubal kuwa chadema kuna ubinafsi na kwa nini usikubari kuwa mbinafsi huyo ni mbowe. Kabali yaishe
Hii dhana ni njema kinadharia, 2015 kulikuwa na Ukawa, yenye cdm, cuf, Nld na Nccr. Leo hii Cuf na Nccr wako wapi? Cdm ndio chama chenye nguvu kwenye upinzani ila kuna tatizo la ubinafsi, na Act wako tayari kwa umoja, ila historia yao ya 2015, na tofauti/kutokuaminiana kwa Mbowe na Zito ni tatizo la dhahiri. Ni ngumu kukataa uanzishwaji wa ACT na mkono wa ccm, tena hiyo ACT ni kama mtoto wa nje wa ccm aliyepatikana kutokana na ugomvi wa Zito na Mbowe/cdm.

Cdm na Act ndio vyama vinavyoweza kuungana ili kutoa ushindani stahiki dhidi ya CCM. Je wako tayari kuondoa tofauti zao hasa zinazoendana na historia zao? Hili ni suala litakalopata majibu kulingana na muda. Ila tatizo la msingi kwangu sio kuungana, bali tume ya uchaguzi ilivyo na matumizi mabaya ya madaraka ya Magufuli itakuwaje? Ikumbukwe sasa hivi Magufuli anachezea katiba kupata kinga, lengo ni ili kupata uhalali wa kuchezea chaguzi za nchi hii.
 
Ulikuwa wapi siku zote kukubal kuwa chadema kuna ubinafsi na kwa nini usikubari kuwa mbinafsi huyo ni mbowe. Kabali yaishe

Ninajitambua vya kutosha, usidhani mimi ni bendera fuata upepo kama ww dogo.
 
Zitto mjanja sana, kasoma alama za nyakati kaogopa kugombea urais mwaka huu maana ataaibika, anataka awaunge mkono ili kipindi kijacho iwe zamu yake kuungwa mkono wakati JPM akiwa hayupo.
 
Mara ya kwanza kuusoma uzi mzima wa Zitto.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Zitto mjanja sana, kasoma alama za nyakati kaogopa kugombea urais mwaka huu maana ataaibika, anataka awaunge mkono ili kipindi kijacho iwe zamu yake kuungwa mkono wakati JPM akiwa hayupo.

Acha upotoshaji wa kijinga, kwani mpaka sasa Zito kasema ataawaunga mkono cdm kwenye mgombea urais? Hata umoja wenyewe bado unaanza kumpamba Zito, au hayo ndio matamanio yako?

Halafu hata wakiungana kwani kuna guarantee ya huo umoja kuendelea hiyo 2025? Nccr na Cuf walikuwa kwenye Ukawa 2015, leo hii wako wapi?

JPM Hana uwezo wa kushindana kisiasa kwa box la kura, pitia historia yake alipokuwa mbunge, ni mara ngapi alishinda kwa box la kura, pia upate taarifa kwa usahihi alikuwa anashinda kwa kufanya nini.
 
Nikisema nyie ni kenge kwenye msafara wa mamba nitakuwa nimewakuza sana,nyie ni mijusi tu wasindikizaji.chadema,act-wazalendo nk nj mijusi tu,mwaka huu mtabaki kubweka tu kama mbwa koko hamna sera za maana.Consistency ni zero, jana mlikuwa na lile,leo mna hili kesho mna jingine tena.
 
Nikisema nyie ni kenge kwenye msafara wa mamba nitakuwa nimewakuza sana,nyie ni mijusi tu wasindikizaji.chadema,act-wazalendo nk nj mijusi tu,mwaka huu mtabaki kubweka tu kama mbwa koko hamna sera za maana.Consistency ni zero, jana mlikuwa na lile,leo mna hili kesho mna jingine tena.
Bc ngoja na ww tukuite nyoka wa kijani...au punda mbeba mizigo wa wanaume wenzio wa ccm
 
MAJIBU YA KATIBU MKUU WA ACT WAZALENDO ADO SHAIBU ALIPOULIZWA KUHUSU KAULI YA CHADEMA KUSIMAMISHA WAGOMBEA ZANZIBAR.

Kwenye Mkutano wake na waandishi wa habari, Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo Ndugu Ado Shaibu aliulizwa na waandishi wa habari kuhusu msimamo wa ACT Wazalendo baada ya CHADEMA kutangaza mchakato wa wagombea wa Urais Zanzibar.

Ado Shaibu: CHADEMA ni chama cha siasa. Kina haki ya kujiandaa na uchaguzi ikiwemo kuandaa wagombea wa ngazi zote sehemu yoyote ya nchi ikiwemo Zanzibar.

Ado Shaibu: Mara baada ya Katibu Mkuu wa CHADEMA kutangaza kufungua milango ya ushirikiano wa vyama, siku inayofuata nilimwandikia barua kupokea hatua hiyo kwa mikono miwili na kuonesha utayari wa ACT Wazalendo.

Ado Shaibu: Tunahitaji ushirikiano wa vya vyama vya upinzani na wapenda demokrasia wotr ili kuing'oa CCM madarakani 2020 na kuleta mabadiliko kwenye maisha ya wananchi.

Ado Shaibu: CCM haipendi umoja wa vyama vya upinzani. Itafanya kila njia kutugawanya. Sisi ACT Wazalendo tumetamka mara nyingi kuwa tupo tayari kwa umoja na tutasimamia hilo.

Imeandaliwa na:

Janeth Rithe, Naibu Katibu, Idara ya Habari, Uenezi na Mahusiano kwa Umma, ACT Wazalendo.
07 Juni 2020.
TUNAOMBA MUUNGANO WA ACT NA CDM ,HAWA WENGINE NI WABABAISHAJI
 
Back
Top Bottom