Adhabu ya Spika kwa Mbunge Mnyika ni void ab initio?

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,192
25,493
Nakiri kuchelewa kuleta hoja hii hapa. Lakini, mniwie radhi na kunisoma ninachokileta hapa kwa mjadala. Kimsingi, Bunge linaoongozwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Sheria na hasa kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la mwaka 2013.

Kanuni za Bunge ndizo hasa zinazoratibu shughuli na mwenendo mzima wa Bunge kuanzia uongozi; Kamati za Bunge; vikao na kadhalika. Kila jambo linalofanyika Bungeni huratibiwa na Kanuni za Bunge. Kanuni ndiyo nyenzo muhimu kwa kila Mbunge.

Nimejipa muda wa kuzisoma Kanuni husika (nitaziambatanisha hapa) ili nione uhalali wa adhabu aliyopewa Mbunge wa Kibamba John John Mnyika ya kutohudhuria vikao vya Bunge vya juma zima. Ni adhabu iliyotamkwa na Spika Job Ndugai wakati Mnyika akitolewa nje ya Bunge.

Katika Kanuni za Bunge, sikuona mahali popote ambapo Spika au Kiti cha Spika kwa ujumla kinapewa mamlaka ya kumfanya Mbunge asihudhurie, yaani kumsimamisha, kuhudhuria vikao vya Bunge. Nimeikosa Kanuni au Fasili fulani inayompa mamlaka hayo.

Kisheria na kikanuni, suala la Mnyika lilipaswa kupelekwa kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuchunguzwa, kujadiliwa na mapendekezo kutolewa. Kumsimamisha vikao bila ya kumsikiliza ni kinyume na kanuni za haki za msingi za kusikilizwa kabla ya kuadhibiwa. Ilitosha kumtoa nje ya Bunge ili kulinda utulivu na amani Bungeni.

Katika kukosekana kwa Kanuni au Fasili inayompa madaraka Spika kumsimamisha Mbunge kuhudhuria vikao bila kusikilizwa au kujadiliwa na Kamati ya Maadili, adhabu ya Spika Ndugai ni halali? Au ndiyo batili tangu mwanzo (void ab initio)?
 

Attachments

  • 1447851651-Kanuni za Kudumu za Bunge.pdf
    282.5 KB · Views: 61
Adhabu Siyo ya Spika ni azimio la Bunge
.....Mwalimu wako wa sheria ni nani?
 
Nadhani hapa ndipo Spika wetu mtukufu sana alipopotoka Petro kama nimekosea ruksa kunisahihisha.

Uadilifu kwa Kiongozi wa Bunge

8.Kwa kuzingatia matakwa na masharti yaliyowekwa na kiapo cha kazi zake na kwa madhumuni ya utoaji wa maamuzi na
uendeshaji wa Shughuli za Bunge kwa haki na bila upendeleo, Spika:-

(a) ataendesha shughuli za Bunge na kutoa maamuzi kwa haki, uadilifu na bila chuki wala upendeleo wowote, kwa kuongozwa na Katiba,Sheria za nchi, Kanuni hizi, Kanuni nyingine zilizopo, maamuzi ya maspika wa Bunge waliotangulia na pia kwa kuzingatia uzoefu pamoja na mila na desturi za mabunge mengine yanayofuata utaratibu wa kibunge unaofanana na unaofuatwa na Bunge la Tanzania

(b) hatafungwa na msimamo utakaowekwa au makubaliano yatakayofikiwa na Kamati yoyote ya Chama cha Siasa kinachowakilishwa Bungeni.
 
Nadhani hapa ndipo Spika wetu mtukufu sana alipopotoka Petro kama nimekosea ruksa kunisahihisha.

Uadilifu kwa Kiongozi wa Bunge

8.Kwa kuzingatia matakwa na masharti yaliyowekwa na kiapo cha kazi zake na kwa madhumuni ya utoaji wa maamuzi na
uendeshaji wa Shughuli za Bunge kwa haki na bila upendeleo, Spika:-

(a) ataendesha shughuli za Bunge na kutoa maamuzi kwa haki, uadilifu na bila chuki wala upendeleo wowote, kwa kuongozwa na Katiba,Sheria za nchi, Kanuni hizi, Kanuni nyingine zilizopo, maamuzi ya maspika wa Bunge waliotangulia na pia kwa kuzingatia uzoefu pamoja na mila na desturi za mabunge mengine yanayofuata utaratibu wa kibunge unaofanana na unaofuatwa na Bunge la Tanzania

(b) hatafungwa na msimamo utakaowekwa au makubaliano yatakayofikiwa na Kamati yoyote ya Chama cha Siasa kinachowakilishwa Bungeni.
Mkuu Tetty, tumalize kwanza hilo la adhabu
 
Mi najiuliza, je Mh. Mnyika hakufanya kosa au kafanya kosa kwa kitendo chake cha kulalamika ndani ya bunge bila ya idhini ya spika. Je spika alipo simama na pia kumtaka Mh. Mnyika kukaa chini na Mnyika kutotii amri ya spika ni kosa kwa mujibu wa kanuni za bunge au si kosa? Labda tuanzie hapo.
 
Kwa namna alivyoitoa ile adhabu ilionyesha kabisa anaitoa tu kwa jazba bila kufikiria.

Ndugai ni janga lingine kwa demokrasia ya Nchi hii.
 
Nakiri kuchelewa kuleta hoja hii hapa. Lakini, mniwie radhi na kunisoma ninachokileta hapa kwa mjadala. Kimsingi, Bunge linaoongozwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Sheria na hasa kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la mwaka 2013.

Kanuni za Bunge ndizo hasa zinazoratibu shughuli na mwenendo mzima wa Bunge kuanzia uongozi; Kamati za Bunge; vikao na kadhalika. Kila jambo linalofanyika Bungeni huratibiwa na Kanuni za Bunge. Kanuni ndiyo nyenzo muhimu kwa kila Mbunge.

Nimejipa muda wa kuzisoma Kanuni husika (nitaziambatanisha hapa) ili nione uhalali wa adhabu aliyopewa Mbunge wa Kibamba John John Mnyika ya kutohudhuria vikao vya Bunge vya juma Zima. Ni adhabu iliyotamkwa na Spika Job Ndugai wakati Mnyika akitolewa nje ya Bunge.

Katika Kanuni za Bunge, sikuona mahali popote ambapo Spika au Kiti cha Spika kwa ujumla kinapewa mamlaka ya kumfanya Mbunge asihudhurie, yaani kumsimamisha, kuhudhuria vikao vya Bunge. Nimeikosa Kanuni au Fasili fulani inayompa mamlaka hayo.

Kisheria na kikanuni, suala la Mnyika lilipaswa kupelekwa kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuchinguzwa, kujadiliwa na mapendekezo kutolewa. Kumsimamisha vikao bila ya kumsikiliza ni kinyume na kanuni za haki za msingi za kusikilizwa kabla ya kuadhibiwa. Ilitosha kumtoa nje ya Bunge ili kulinda utulivu na amani Bungeni.

Katika kukosekana kwa Kanuni au Fasili inayompa madaraka Spika kumsimamisha Mbunge kuhudhuria vikao bila kusikilizwa au kujadiliwa na Kamati ya Maadili, adhabu ya Spika Ndugai ni halali? Au ndiyo batili tangu mwanzo (void ab initio)?
Petro, you are taking a wrong course! This issue should be looked at in the eye of constitutional law/administrative. Mimi siyo mtaalamu ila napenda kusoma haya mambo, formally! Najaribu kuyaelewa nyinyi wataalamu mtuongozee!
Kanuni za bunge zinampa mamlaka makubwa spika, hivyo anaweza kufanya "upuuzi" anaoutaka! LAKINI mimi nasema hivi:

Parliament is a creature of the constitution and therefore all proceed from the parliament should conform to the dictates of the constitution! Kanuni za bunge kama zinakiuka katiba zinaweza kuwa challenged. Nieleweshe, siyo mtaalamu, but we can discuss

Dragon tumekuwa na majadiliano kuhusu hilo, nakuwekea andiko lake!

Can the arbitrary actions of the SPEAKER from his absolute power be subjected to judicial review?


Kiongozi,

Swali lako nitalijibu kwa Kiswahili, na inapobidi nitachanganya na kingereza. Katika kujibu swali lako nitajikita zaidi katika kadhia iliyotokea hivi karibuni bungeni, yaani ya John Mnyika kufukuzwa bungeni na kusimamishwa kuhudhuria baadhi ya vikao vya bunge la Jamhuri wa Muungano. Pia nitajikita kwa yaliyowakuta wabunge Halima Mdee na Esther Bulaya. Hii ni kwa sababu swali lako halijaweka nadharia maalum (specific).

Kiongozi na ndugu Wana JF wote,

Spika wa bunge la JMT kapewa mamlaka na Katiba ya JMT, na mamlaka hayo kupanuliwa au/na kufafanuliwa zaidi na Kanuni za Kudumu za Bunge (Kanuni). Mamlaka hayo yanalindwa pia na Katiba na Kanuni. Spika wa Bunge la JMT anayo mamlaka katika bunge ambalo yeye ndiye kiongozi wake, ambayo yamegawanyika katika sehemu maalum mbili, Mamlaka ya lazima na mamlaka ya hiyari (mandatory and discretionary powers).

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni dola yenye mihimili mitatu, utawala, bunge ma mahakama. Mamlaka ya mhimili wa mahakama, pamoja ma mambo mengine, ni kupitia maamuzi ya mihilili migine katika utendaji haki, ikiwemo mahakama yenyewe. Hii ndiyo inaitwa Judicial Review. Judicial review hufanyika ili kujiridhisha kama haki imetendeka katika utekelezaji wa majukumu ya chombo cha dola yaliyotolewa au yaliyopo kisheria.

Katika kutoa maamuzi yake katika suala hili la judicial review lazima mahakama ijiridhishe na uwepo wa mambo yafuatayo:

1. Uamuzi umetolewa na mamlaka ya dola (Public authority).

2. Mamlaka ya dola ilitoa uamuzi huo katika kutekeleza majukumu yake iliyopewa kisheria.

3. Hakuna namna nyingine ambayo mlalamikaji angeweza kufanya zaidi ya kuomba judicial review.

4. Kinacholalamikiwa kufanyika au kutofanyika kiwe ni cha lazima (mandatory) kufanywa au kutofanywa, kisiwa cha hiari (discretional).

5.

Kama nilivyoeleza hapo juu, spika wa bunge anatekeleza majukumu yake kwa mamlaka aliyopewa kisheria. Kanuni za kudumu za bunge (2016), kanuni ya 67 (1) na (2) zinampa mamlaka spika kukataza majadiliano na anaweza kumkataza mbunge yeyote kuzungumza. Kanuni hizi zinasomeka hivi:

67.-(1) Spika anaweza kulihutubia Bunge wakati wowote na kwa

ajili hiyo, anaweza kumkatiza Mbunge yeyote anayezungumza.

(2) Endapo Spika atasimama wakati wa mjadala, na kuanza

kuzungumza, Mbunge yeyote ambaye atakuwa anazungumza

wakati huo au ambaye atakuwa amesimama mahali pake akisubiri

kuanza kuzungumza, ataketi mahali pake, na Bunge litabaki kimya

ili Spika aweze kutoa maelekezo au taarifa yake.

Kanuni ya 68 inatoa taratibu mbalimbali na taratibu mbalimbali. Kanuni za 68 (4) na (5) zinasomeka hivi:

4) Spika anaweza, ama papo hapo kutoa uamuzi wake juu

ya jambo la utaratibu lililotajwa au kuahirisha uamuzi ili alifikirie

zaidi jambo hilo na kutoa uamuzi baadaye au kutoa uamuzi na

baadaye kutoa sababu za uamuzi huo, vyovyote atakavyoamua.

(5) Katika kufikia uamuzi wake, Spika anaweza kuitaka Kamati

ya Kudumu ya Kanuni za Bunge au Kamati nyingine yoyote ya Bunge

impe ushauri kuhusu jambo husika.

Mbali na hayo, spika amepewa majukumu na mamlaka ya kudhibiti fujo na kusimamia utaratibu bungeni. Kanuni namba 72 (1), (2) na (4) zinasomeka namna hii:

72.-(1) Spika atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa, utaratibu

bora unafuatwa Bungeni, na uamuzi wa Spika kuhusu jambo lolote

la utaratibu utakuwa ni wa mwisho.

(2) Mbunge atakayekiuka utaratibu uliowekwa na Kanuni

hizi anaweza papo hapo kutakiwa na Spika afuate utaratibu na

vilevile Mbunge mwingine yeyote anaweza kusimama na

kumfahamisha Spika kuhusu ukiukwaji wa utaratibu huo na katika

kufanya hivyo, atalazimika kutaja Kanuni ya Bunge iliyoweka

utaratibu uliokiukwa.

(4) Endapo Mbunge atafanya kosa ambalo alikwishawahi

kuadhibiwa kwa mujibu wa fasili ya (2) na (3) ya Kanuni hii, Spika

atalipeleka suala lake kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka

ya Bunge kwa mujibu wa masharti ya Kanuni ya 71 ya Kanuni hizi ili

Kamati hiyo ilishauri Bunge kuhusu hatua za kinidhamu zinazostahili

kuchukuliwa dhidi ya Mbunge huyo.
Kanuni ya 68 (10) inampa spika kuwa na kauli na uamuzi wa mwisho. Kanuni hii inasema:

(10) Uamuzi wa Spika kuhusu suala lolote la utaratibu utakuwa

ni wa mwisho.


Kwa sababu bunge ni chombo chenye mamlaka yake na utaratibu wake, adhabu zimewekwa kisheria kwa yeyote anaekiua utaraitibu na utaratibu wa utekelezaji wake umewekwa. Utaratibu huu upo katika kanuni ya 73. Kanuni za 73 (1) na (2) sinasomeka:

73.-(1) Mbunge au Waziri atakayezungumzia jambo au mambo

ambayo hayaruhusiwi na Kanuni hizi, anaweza kuamriwa na Spika

au Naibu Spika au Mwenyekiti akatishe hotuba yake na kukaa mahali

pake.

(2) Endapo Mbunge au Waziri atatumia maneno au lugha

isiyotakiwa Bungeni, yaani lugha ya matusi, usafihi, uchokozi au

lugha ya maudhi na akitakiwa na Spika ajirekebishe kwa kufuta

maneno au lugha hiyo atakataa kufanya hivyo, Spika anaweza

kumwamuru Mbunge huyo atoke mara moja nje ya Ukumbi wa

Bunge na abaki huko nje kwa muda wote uliosalia wa kikao cha

siku hiyo.

Bunge nalo limepewa mamlaka ya kutoa adhabu kufuatia ukiukwaji wa taratibu au utovu wa nidhamu. Kanuni namba 74 (1), (2) na (3)(b) zinahusika. Hizi zinasomeka kama ifuatavyo:

74.-(1) Spika anaweza kutaja jina la Mbunge kwamba amedharau

Mamlaka ya Spika na kisha kupeleka jina hilo kwenye Kamati ya

Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ikiwa:-

(a) kwa maneno au vitendo, Mbunge huyo

anaonesha dharau kwa mamlaka ya Spika; au

(b) Mbunge huyo atafanya kitendo chochote cha

makusudi cha kudharau Shughuli ya Bunge au

Mbunge yeyote anayeongoza shughuli hiyo.

(2) Ikiwa maneno au vitendo vya Mbunge vilivyoainishwa

katika fasili ya (1) ya Kanuni hii vimetokea wakati Bunge likiwa katika

Kamati ya Bunge Zima, basi Mwenyekiti atasimamisha shughuli za

Kamati na ataagiza Bunge kurudia ili kumpatia Spika fursa ya kutoa

taarifa kwa Bunge kuhusu mwenendo wa Mbunge huyo na

kuwasilisha suala hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka

ya Bunge.

(3) Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itajadili

suala hilo na ikithibitika kuwa Mbunge husika ametenda kosa

inaweza kushauri kwamba:-

(a) ikiwa ni kosa lake la kwanza Mbunge huyo

asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi kumi; au

(b) ikiwa ni kosa lake la pili au zaidi Mbunge huyo

asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi ishirini;

Mbali na hayo yote, Bunge limejiwekea miiko yake lenyewe. Bungeni kuna mambo ambayo hayaruhusiwi, miongoni mwa hayo ni yale yaliyomo katika kanuni ya 64 (1)(e), (f) na (g). kanuni hizo ni kama ilivyoainishwa hapa:

64.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 100 ya Katiba yanayolinda

na kuhifadhi uhuru wa mawazo na majadiliano katika Bunge,

Mbunge:-

(a)

(d)

(e) hatazungumzia mwenendo wa Rais, Spika, Mbunge, Jaji, Hakimu au mtu mwingine yeyote anayeshughulikia utoaji wa haki, isipokuwa tu kama kumetolewa hoja mahususi kuhusu jambo husika;

(f) hatamsema vibaya au kutoa lugha ya matusi kwa Mbunge au mtu mwingine yeyote;

(g) hatatumia lugha ya kuudhi au inayodhalilisha

watu wengine.

Kwa hiyo basi ni dhairi kwamba spika wa bunge hakuenda kinyume na kanuni yoyote ya bunge kwa kumtoa mbunge Mnyika nje ya ukumbi wa bunge na kutoa adhabu palepale pasipo uwepo wa Mnyika mwenyewe. Pia spika alitumia misingi ya kanuni kuwashtaki Halima Mdee na Esther Bulaya kwenye kamati ya maadili ya bunge, na uamuzi uliotoka ni sahihi.

Sasa tunarudi kwenye swali letu. Tumeona hapo juu namna judicial review inaweza fanyika, yaani zile test tano zilizoainishwa. Spika alikuwa anafanya kazi ya mamlaka ya dola, na alikuwa anafanya maamuzi kulingana na utaratibu.

Pia judicial review, ikumbukwe sana, haitakuwa na meno kama kilichofanywa kilikuwa ni hatua za kinidhamu. Hapa ieleweke kwamba hatua ya kinidhamu ni ile ya kumchukulia hatua (kutoa uamuzi) mtu ambae ameonekana kafanya kosa dhahili pasipo kumpa mda wa kujitetea. Mnyika hakupewa mda wa kujitetea, Halima na Esther suala lao lilipelekwa kwenye kamati.

Kama chombo kinachotoa uamuzi kinatakiwa kumuita mshukiwa ili ajitetee, hii huitwa quasi judicial action na kimsingi inaweza pitiwa na mahakama katika judicial review.

Tukirudi nyuma, kanuni za buge zimetungwa kwa mamlaka ya katiba, kama bunge lenyewe lilivyo na kiti cha spika kilivyo kwa mujibu wa katiba. Ibara ya 100 ya katiba ya JMT inatoa uhuru wa majadiliano wa shughuli bungeni kwa mujibu wa kanuni na taratibu. Pia kifungu hiki kinatoa zuio kwa mahakama au chombo chochote kuhoji yaliyotokea bungini wakati bunge lipo katika kazi yake. Ibara hii inasimeka ifuatavyo:

100. Uhuru wa majadiliano na utaratibu wa shughuli Sheria Na. 15 ya 1984 ib. 14

(1) Kutakuwa na uhuru wa mawazo, majadiliano na utaratibu katika Bunge, na uhuru huo hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano, au katika mahakama au mahali penginepo nje ya Bunge.

(2) Bila ya kuathiri Katiba hii au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, Mbunge yeyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kutokana na jambo lolote alilolisema au kulifanyw ndani ya Bunge au alilolileta Bungeni kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo.

Kwa vyovyote vile basi Bunge, ikiwa ni pamoja na spika wake, haliko subject to judicial review. Hii ni kwa sababu ya kinga iliyowekewa na katiba. Ikitokwa spika amekuwa so arbitrary kama swali lilivyouliza, hakuna namna ya kufanyia uamuzi wake judicial review. Kuna mamna wanasheria huwa wanapinga baadhi ya vifungu vya sheria zikiwemo ibara za katiba kwa sababu zinakuwa zinakinzana ka Katiba (unconstitutional). Hata hivyo, hata kwa kutotilia maanani ibara ya 100 ya katiba ambayo mwingine anaweza kusema iko kinyume na katiba kwa kuzuia mamlaka ya mahakama, bado spika hatakuwa subject wa judicial review kwa sababu kafuata utaratibu, na kama kuna malalamiko kwamba katumia vibaya madaraka yae labda kwa sababu “Katoa uamuzi wa kukurupuka na uonevu/chuki” bado yuko upande salama. Maamuzi ya kumfukuza mtu bungeni, mbali tu ya kuwa yapo katika kanuni, yanatekelezwa katika misingi ya uamuzi huru au hiari. (Discretional).

Nikamjibu:
Karibuni sana Dragon asante kwa maelezo ya kitaalamu. Yoye uliyoyaandika yako valid at all fours within the legal philosophy!! Lakini actually hapo ndipo pa kuanzia. Mahakama ndiyo imepewa mamlaka ya kuangalia kama HAKI in all aspects of life inatendekea. Hivyo sheria yoyote inayotungwa kuiwezesha haki isitendeke, hiyo outright ni BATILI!
Nadhani wataalamu kama nyinyi mnaweza kuanzia hapo!. Spika akiamua kuamrisha kuwa piga, nyonga huyu ndani ya bunge asihojiwe, NO! Mtoe nje Mnyika, akikaidi vunja miguu, wakavunja, asihojiwe! NO. Hapo ndipo pa kuanzia! Nadhani context ya sentensi yangu hiyo ya mwisho unaipata!
India Mahakama ilikataa kitu kama hicho hapa Tanzania.
Tatizo hatuna Majaji wenye kufikiri philosophically katika haya mambo. Majaji kama Mwalusanya, Lugakingira, Katiti, Kyando, Mroso and few others, wangelitoa reasoned solution kwa hili!
 
Petro, you are taking a wrong course! This issue should be looked at in the eye of constitutional law/administrative. Mimi siyo mtaalamu ila napenda kusoma haya mambo, formally! Najaribu kuyaelewa nyinyi wataalamu mtuongozee!
Kanuni za bunge zinampa mamlaka makubwa spika, hivyo anaweza kufanya "upuuzi" anaoutaka! LAKINI mimi nasema hivi:

Parliament is a creature of the constitution and therefore all proceed from the parliament should conform to the dictates of the constitution! Kanuni za bunge kama zinakiuka katiba zinaweza kuwa challenged. Nieleweshe, siyo mtaalamu, but we can discuss

Dragon tumekuwa na majadiliano kuhusu hilo, nakuwekea andiko lake!

Can the arbitrary actions of the SPEAKER from his absolute power be subjected to judicial review?


Kiongozi,

Swali lako nitalijibu kwa Kiswahili, na inapobidi nitachanganya na kingereza. Katika kujibu swali lako nitajikita zaidi katika kadhia iliyotokea hivi karibuni bungeni, yaani ya John Mnyika kufukuzwa bungeni na kusimamishwa kuhudhuria baadhi ya vikao vya bunge la Jamhuri wa Muungano. Pia nitajikita kwa yaliyowakuta wabunge Halima Mdee na Esther Bulaya. Hii ni kwa sababu swali lako halijaweka nadharia maalum (specific).

Kiongozi na ndugu Wana JF wote,

Spika wa bunge la JMT kapewa mamlaka na Katiba ya JMT, na mamlaka hayo kupanuliwa au/na kufafanuliwa zaidi na Kanuni za Kudumu za Bunge (Kanuni). Mamlaka hayo yanalindwa pia na Katiba na Kanuni. Spika wa Bunge la JMT anayo mamlaka katika bunge ambalo yeye ndiye kiongozi wake, ambayo yamegawanyika katika sehemu maalum mbili, Mamlaka ya lazima na mamlaka ya hiyari (mandatory and discretionary powers).

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni dola yenye mihimili mitatu, utawala, bunge ma mahakama. Mamlaka ya mhimili wa mahakama, pamoja ma mambo mengine, ni kupitia maamuzi ya mihilili migine katika utendaji haki, ikiwemo mahakama yenyewe. Hii ndiyo inaitwa Judicial Review. Judicial review hufanyika ili kujiridhisha kama haki imetendeka katika utekelezaji wa majukumu ya chombo cha dola yaliyotolewa au yaliyopo kisheria.

Katika kutoa maamuzi yake katika suala hili la judicial review lazima mahakama ijiridhishe na uwepo wa mambo yafuatayo:

1. Uamuzi umetolewa na mamlaka ya dola (Public authority).

2. Mamlaka ya dola ilitoa uamuzi huo katika kutekeleza majukumu yake iliyopewa kisheria.

3. Hakuna namna nyingine ambayo mlalamikaji angeweza kufanya zaidi ya kuomba judicial review.

4. Kinacholalamikiwa kufanyika au kutofanyika kiwe ni cha lazima (mandatory) kufanywa au kutofanywa, kisiwa cha hiari (discretional).

5.

Kama nilivyoeleza hapo juu, spika wa bunge anatekeleza majukumu yake kwa mamlaka aliyopewa kisheria. Kanuni za kudumu za bunge (2016), kanuni ya 67 (1) na (2) zinampa mamlaka spika kukataza majadiliano na anaweza kumkataza mbunge yeyote kuzungumza. Kanuni hizi zinasomeka hivi:

67.-(1) Spika anaweza kulihutubia Bunge wakati wowote na kwa

ajili hiyo, anaweza kumkatiza Mbunge yeyote anayezungumza.

(2) Endapo Spika atasimama wakati wa mjadala, na kuanza

kuzungumza, Mbunge yeyote ambaye atakuwa anazungumza

wakati huo au ambaye atakuwa amesimama mahali pake akisubiri

kuanza kuzungumza, ataketi mahali pake, na Bunge litabaki kimya

ili Spika aweze kutoa maelekezo au taarifa yake.

Kanuni ya 68 inatoa taratibu mbalimbali na taratibu mbalimbali. Kanuni za 68 (4) na (5) zinasomeka hivi:

4) Spika anaweza, ama papo hapo kutoa uamuzi wake juu

ya jambo la utaratibu lililotajwa au kuahirisha uamuzi ili alifikirie

zaidi jambo hilo na kutoa uamuzi baadaye au kutoa uamuzi na

baadaye kutoa sababu za uamuzi huo, vyovyote atakavyoamua.

(5) Katika kufikia uamuzi wake, Spika anaweza kuitaka Kamati

ya Kudumu ya Kanuni za Bunge au Kamati nyingine yoyote ya Bunge

impe ushauri kuhusu jambo husika.

Mbali na hayo, spika amepewa majukumu na mamlaka ya kudhibiti fujo na kusimamia utaratibu bungeni. Kanuni namba 72 (1), (2) na (4) zinasomeka namna hii:

72.-(1) Spika atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa, utaratibu

bora unafuatwa Bungeni, na uamuzi wa Spika kuhusu jambo lolote

la utaratibu utakuwa ni wa mwisho.

(2) Mbunge atakayekiuka utaratibu uliowekwa na Kanuni

hizi anaweza papo hapo kutakiwa na Spika afuate utaratibu na

vilevile Mbunge mwingine yeyote anaweza kusimama na

kumfahamisha Spika kuhusu ukiukwaji wa utaratibu huo na katika

kufanya hivyo, atalazimika kutaja Kanuni ya Bunge iliyoweka

utaratibu uliokiukwa.

(4) Endapo Mbunge atafanya kosa ambalo alikwishawahi

kuadhibiwa kwa mujibu wa fasili ya (2) na (3) ya Kanuni hii, Spika

atalipeleka suala lake kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka

ya Bunge kwa mujibu wa masharti ya Kanuni ya 71 ya Kanuni hizi ili

Kamati hiyo ilishauri Bunge kuhusu hatua za kinidhamu zinazostahili

kuchukuliwa dhidi ya Mbunge huyo.
Kanuni ya 68 (10) inampa spika kuwa na kauli na uamuzi wa mwisho. Kanuni hii inasema:

(10) Uamuzi wa Spika kuhusu suala lolote la utaratibu utakuwa

ni wa mwisho.


Kwa sababu bunge ni chombo chenye mamlaka yake na utaratibu wake, adhabu zimewekwa kisheria kwa yeyote anaekiua utaraitibu na utaratibu wa utekelezaji wake umewekwa. Utaratibu huu upo katika kanuni ya 73. Kanuni za 73 (1) na (2) sinasomeka:

73.-(1) Mbunge au Waziri atakayezungumzia jambo au mambo

ambayo hayaruhusiwi na Kanuni hizi, anaweza kuamriwa na Spika

au Naibu Spika au Mwenyekiti akatishe hotuba yake na kukaa mahali

pake.

(2) Endapo Mbunge au Waziri atatumia maneno au lugha

isiyotakiwa Bungeni, yaani lugha ya matusi, usafihi, uchokozi au

lugha ya maudhi na akitakiwa na Spika ajirekebishe kwa kufuta

maneno au lugha hiyo atakataa kufanya hivyo, Spika anaweza

kumwamuru Mbunge huyo atoke mara moja nje ya Ukumbi wa

Bunge na abaki huko nje kwa muda wote uliosalia wa kikao cha

siku hiyo.

Bunge nalo limepewa mamlaka ya kutoa adhabu kufuatia ukiukwaji wa taratibu au utovu wa nidhamu. Kanuni namba 74 (1), (2) na (3)(b) zinahusika. Hizi zinasomeka kama ifuatavyo:

74.-(1) Spika anaweza kutaja jina la Mbunge kwamba amedharau

Mamlaka ya Spika na kisha kupeleka jina hilo kwenye Kamati ya

Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ikiwa:-

(a) kwa maneno au vitendo, Mbunge huyo

anaonesha dharau kwa mamlaka ya Spika; au

(b) Mbunge huyo atafanya kitendo chochote cha

makusudi cha kudharau Shughuli ya Bunge au

Mbunge yeyote anayeongoza shughuli hiyo.

(2) Ikiwa maneno au vitendo vya Mbunge vilivyoainishwa

katika fasili ya (1) ya Kanuni hii vimetokea wakati Bunge likiwa katika

Kamati ya Bunge Zima, basi Mwenyekiti atasimamisha shughuli za

Kamati na ataagiza Bunge kurudia ili kumpatia Spika fursa ya kutoa

taarifa kwa Bunge kuhusu mwenendo wa Mbunge huyo na

kuwasilisha suala hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka

ya Bunge.

(3) Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itajadili

suala hilo na ikithibitika kuwa Mbunge husika ametenda kosa

inaweza kushauri kwamba:-

(a) ikiwa ni kosa lake la kwanza Mbunge huyo

asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi kumi; au

(b) ikiwa ni kosa lake la pili au zaidi Mbunge huyo

asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi ishirini;

Mbali na hayo yote, Bunge limejiwekea miiko yake lenyewe. Bungeni kuna mambo ambayo hayaruhusiwi, miongoni mwa hayo ni yale yaliyomo katika kanuni ya 64 (1)(e), (f) na (g). kanuni hizo ni kama ilivyoainishwa hapa:

64.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 100 ya Katiba yanayolinda

na kuhifadhi uhuru wa mawazo na majadiliano katika Bunge,

Mbunge:-

(a)

(d)

(e) hatazungumzia mwenendo wa Rais, Spika, Mbunge, Jaji, Hakimu au mtu mwingine yeyote anayeshughulikia utoaji wa haki, isipokuwa tu kama kumetolewa hoja mahususi kuhusu jambo husika;

(f) hatamsema vibaya au kutoa lugha ya matusi kwa Mbunge au mtu mwingine yeyote;

(g) hatatumia lugha ya kuudhi au inayodhalilisha

watu wengine.

Kwa hiyo basi ni dhairi kwamba spika wa bunge hakuenda kinyume na kanuni yoyote ya bunge kwa kumtoa mbunge Mnyika nje ya ukumbi wa bunge na kutoa adhabu palepale pasipo uwepo wa Mnyika mwenyewe. Pia spika alitumia misingi ya kanuni kuwashtaki Halima Mdee na Esther Bulaya kwenye kamati ya maadili ya bunge, na uamuzi uliotoka ni sahihi.

Sasa tunarudi kwenye swali letu. Tumeona hapo juu namna judicial review inaweza fanyika, yaani zile test tano zilizoainishwa. Spika alikuwa anafanya kazi ya mamlaka ya dola, na alikuwa anafanya maamuzi kulingana na utaratibu.

Pia judicial review, ikumbukwe sana, haitakuwa na meno kama kilichofanywa kilikuwa ni hatua za kinidhamu. Hapa ieleweke kwamba hatua ya kinidhamu ni ile ya kumchukulia hatua (kutoa uamuzi) mtu ambae ameonekana kafanya kosa dhahili pasipo kumpa mda wa kujitetea. Mnyika hakupewa mda wa kujitetea, Halima na Esther suala lao lilipelekwa kwenye kamati.

Kama chombo kinachotoa uamuzi kinatakiwa kumuita mshukiwa ili ajitetee, hii huitwa quasi judicial action na kimsingi inaweza pitiwa na mahakama katika judicial review.

Tukirudi nyuma, kanuni za buge zimetungwa kwa mamlaka ya katiba, kama bunge lenyewe lilivyo na kiti cha spika kilivyo kwa mujibu wa katiba. Ibara ya 100 ya katiba ya JMT inatoa uhuru wa majadiliano wa shughuli bungeni kwa mujibu wa kanuni na taratibu. Pia kifungu hiki kinatoa zuio kwa mahakama au chombo chochote kuhoji yaliyotokea bungini wakati bunge lipo katika kazi yake. Ibara hii inasimeka ifuatavyo:

100. Uhuru wa majadiliano na utaratibu wa shughuli Sheria Na. 15 ya 1984 ib. 14

(1) Kutakuwa na uhuru wa mawazo, majadiliano na utaratibu katika Bunge, na uhuru huo hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano, au katika mahakama au mahali penginepo nje ya Bunge.

(2) Bila ya kuathiri Katiba hii au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, Mbunge yeyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kutokana na jambo lolote alilolisema au kulifanyw ndani ya Bunge au alilolileta Bungeni kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo.

Kwa vyovyote vile basi Bunge, ikiwa ni pamoja na spika wake, haliko subject to judicial review. Hii ni kwa sababu ya kinga iliyowekewa na katiba. Ikitokwa spika amekuwa so arbitrary kama swali lilivyouliza, hakuna namna ya kufanyia uamuzi wake judicial review. Kuna mamna wanasheria huwa wanapinga baadhi ya vifungu vya sheria zikiwemo ibara za katiba kwa sababu zinakuwa zinakinzana ka Katiba (unconstitutional). Hata hivyo, hata kwa kutotilia maanani ibara ya 100 ya katiba ambayo mwingine anaweza kusema iko kinyume na katiba kwa kuzuia mamlaka ya mahakama, bado spika hatakuwa subject wa judicial review kwa sababu kafuata utaratibu, na kama kuna malalamiko kwamba katumia vibaya madaraka yae labda kwa sababu “Katoa uamuzi wa kukurupuka na uonevu/chuki” bado yuko upande salama. Maamuzi ya kumfukuza mtu bungeni, mbali tu ya kuwa yapo katika kanuni, yanatekelezwa katika misingi ya uamuzi huru au hiari. (Discretional).

Nikamjibu:
Karibuni sana Dragon asante kwa maelezo ya kitaalamu. Yoye uliyoyaandika yako valid at all fours within the legal philosophy!! Lakini actually hapo ndipo pa kuanzia. Mahakama ndiyo imepewa mamlaka ya kuangalia kama HAKI in all aspects of life inatendekea. Hivyo sheria yoyote inayotungwa kuiwezesha haki isitendeke, hiyo outright ni BATILI!
Nadhani wataalamu kama nyinyi mnaweza kuanzia hapo!. Spika akiamua kuamrisha kuwa piga, nyonga huyu ndani ya bunge asihojiwe, NO! Mtoe nje Mnyika, akikaidi vunja miguu, wakavunja, asihojiwe! NO. Hapo ndipo pa kuanzia! Nadhani context ya sentensi yangu hiyo ya mwisho unaipata!
India Mahakama ilikataa kitu kama hicho hapa Tanzania.
Tatizo hatuna Majaji wenye kufikiri philosophically katika haya mambo. Majaji kama Mwalusanya, Lugakingira, Katiti, Kyando, Mroso and few others, wangelitoa reasoned solution kwa hili!
Mkuu, nashukuru kwa hoja na mchango wako. Lakini, hoja yangu ni iwapo Spika ana mamlaka kutoa adhabu kama alivyofanya kwa Mnyika chini ya Kanuni za Bunge au la. Tuanzie hapo kwanza kabla ya yote.
 
Nakiri kuchelewa kuleta hoja hii hapa. Lakini, mniwie radhi na kunisoma ninachokileta hapa kwa mjadala. Kimsingi, Bunge linaoongozwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Sheria na hasa kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la mwaka 2013.

Kanuni za Bunge ndizo hasa zinazoratibu shughuli na mwenendo mzima wa Bunge kuanzia uongozi; Kamati za Bunge; vikao na kadhalika. Kila jambo linalofanyika Bungeni huratibiwa na Kanuni za Bunge. Kanuni ndiyo nyenzo muhimu kwa kila Mbunge.

Nimejipa muda wa kuzisoma Kanuni husika (nitaziambatanisha hapa) ili nione uhalali wa adhabu aliyopewa Mbunge wa Kibamba John John Mnyika ya kutohudhuria vikao vya Bunge vya juma zima. Ni adhabu iliyotamkwa na Spika Job Ndugai wakati Mnyika akitolewa nje ya Bunge.

Katika Kanuni za Bunge, sikuona mahali popote ambapo Spika au Kiti cha Spika kwa ujumla kinapewa mamlaka ya kumfanya Mbunge asihudhurie, yaani kumsimamisha, kuhudhuria vikao vya Bunge. Nimeikosa Kanuni au Fasili fulani inayompa mamlaka hayo.

Kisheria na kikanuni, suala la Mnyika lilipaswa kupelekwa kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuchunguzwa, kujadiliwa na mapendekezo kutolewa. Kumsimamisha vikao bila ya kumsikiliza ni kinyume na kanuni za haki za msingi za kusikilizwa kabla ya kuadhibiwa. Ilitosha kumtoa nje ya Bunge ili kulinda utulivu na amani Bungeni.

Katika kukosekana kwa Kanuni au Fasili inayompa madaraka Spika kumsimamisha Mbunge kuhudhuria vikao bila kusikilizwa au kujadiliwa na Kamati ya Maadili, adhabu ya Spika Ndugai ni halali? Au ndiyo batili tangu mwanzo (void ab initio)?
Petro pitia andiko la Dragon , kutoka hapo njoo na maoni yake. ameandika vizuri!
 
Mi najiuliza, je Mh. Mnyika hakufanya kosa au kafanya kosa kwa kitendo chake cha kulalamika ndani ya bunge bila ya idhini ya spika. Je spika alipo simama na pia kumtaka Mh. Mnyika kukaa chini na Mnyika kutotii amri ya spika ni kosa kwa mujibu wa kanuni za bunge au si kosa? Labda tuanzie hapo.
Hilo ni kosa na kikanuni alipaswa kutolewa nje kama ilivyofanyika. Vipi kuzimamishwa kuhudhuria vikao vya juma zima? Ndiyo hoja yangu
 
Back
Top Bottom