Adhabu ya kifo ni halali?

Kinyau

JF-Expert Member
Nov 24, 2006
910
702
Leo ni siku ya kukemea adhabu ya kifo duniani.

Katika jamii zetu kuna wahalifu wengi na wengine ni sugu na wengine tunatamani wauwawe tukiamini kuwa uovu utakoma. Lakini je adhabu ya kifo inamsaidiaje mtuhumiwa aache uovu, je akiuwawa ndio tutakuwa tumelipa ule uovu?? huwa najiuliza sipati jibu, je hiiadhabu ina malengo gani haswa?

Ukipata wasaa wa kuongea na wafungwa waliohukumiwa kunyongwa utapa simamzi ya ajabu, wana msongo, hawana tumaini lolote na wengi hujuta, hujuta sanaa na hutamani wangepewa walau kifungo cha maisha.

hii ni moja ya waraka mfupi kutoka mfungwa waliyehukumiwa kunyongwa huko zambia, mfungwa huyu pia ni mtunzi mzuri wa mashairi

Dear all,

I answer to the name of Job Kasonda Kapita. I am incarcerated in Kabwe. Prior to this I was a Policeman in the Zambia Police Force. It was during he execution of my duty that I got in this horror of a dilemma. I shot and subsequently killed a violent suspicious suspect I wanted to arrest for disorderly conduct at the police station.

His verbal provocations, threats and his refusal to be lawfully placed in police cell made it happen. All occurred within the station yard five metres from my office. I was arrested for murder on 6th October 1994. I was convicted in a bizarre manner to be cruelly hanged by the neck till proved dead on 29th February 1995 at the high court.

The judge acted unfairly and exhibited unprofessionalism of the worst manner. There was a difference between witness testimonies at the police and at the court. Being unsatisfied with the conviction and sentence I appealed to our Supreme Court. The Supreme Court upheld the conviction and sentence in 1996. Meanwhile the only option I have remained is to write a petition of mercy to the president of our country.

I am 33 years of age. I never knew the deceased and therefore had no evil intention to harm him. It was purely a misadventure by the nature of my demanding and dangerous career assigned by the government to maintain law and order. I served in the police force for four years without facing an charge or being implicated in a criminal offence.

I am looking for pen friends to support me in my situation. Someone who is loving and caring. My hobbies are Judo, Karate, Golf, Chess, reading Christian literature and solving mathematic problems. I will be thankful for any letter.

Job Kasonda Kapita
Maximum Security Prison
Box 80915
Kabwe, Zambia

Na haya ni baadh ya mashairi aliyoandika

To be hanged by the neck
It brings dreading thoughts
Fears as you see people you find vanished

They are held in the waiting cells till the day of their execution
You only hear shouting voices okay
As your friends are led to be executed
Then you hear the sound of hammers

As the prison guards put last nails on the coffin of an executed prisoner
You do not know when your day comes
You cannot sleep
Minutes are like seconds

Hours are like minutes
Days like hours
Years like days
Time flies
Lucky are those who win their case when they appeal

For they are released
It is a dilemma for those of us who lose our cases
We languish for years
You are abandoned by your family

Though they may intend to visit
They can be tired of the regular visits
As they are made to wait to see their loved ones
It takes decades for cases to be considered
The reason is best known to the authorities
We literally have nothing to do


THE DEATH PENALTY
Perceived as a deterrent to crime
but only meant for paupers
as the rich are spared.

Though implemented with glee by other societies
It is cruel, inhumane and degrading
As it violates constitutional protections of the right to life.

For example
An historical and biblical axiom that Jesus was impaled to death on false testimony
Can society permanently eliminate the horrific prospect of executing innocent people ?

INJUSTICE

Injustice!
You applaud at suffering of others,
You consider the oppression of others your good triumph!
Your triumph fraudulently won because of this your wicked;

You're an architect of misunderstanding in all the communities,
You're an agent of the devil because you don't stand up for the truth in your actions.
You're on earth to destroy than to build because of your treacherous act and vanity in everything.
 
Adhabu ya kifo ni extreme. Lakini kila extreme inayo sababu yake ambayo nayo ni extreme. Usipowahi kuibiwa sio rahisi kujua uchungu wa kuibiwa kiuhalisia. Mbaya zaidi, mwizi mwenyewe asiyekuwa "mstaarabu" wakati wa kutekeleza wizi huo, akauonjesha joto la jiwe, bila shaka hutasahau hayo na kila mwenzio akiibiwa utaipata ndani ya moyo wako hasa simanzi ya kuibiwa.

Hata wale watu wa mob justice mitaani wanaochoma moto vibaka, wezi na majambazi, ukiwauliza kwa nini wanafanya hivyo nadhani ndio utapata sababu nyingi tu zilizowafanya wahalalishe hatua zao walizozichukua.

Sasa kama tunaulizana uhalali wa adhabu ya kifo labda tuulizane pia maana ya adhabu, pia kifo. Adhabu naweza kusema ni malipo halali apewayo mtu kwa jambo alilolifanya. It is a reinforcment either to that individual or to any other one partnership to that society style. Sasa malipo hayo yanaweza kuwa chanya au hasi to the best extrem which you can prefer to name.

Kifo is simply elimination of life, be it self inflicted or otherwise. Lakini mara nyingi anayepewa adhabu ya kifo ni yule aliyeua pia. Sasa pengine ni muhimu kuulizana pia kama kuua ni halali? Kwetu hapa Tanzania adhabu za aina hiyo hutolewa kwa mtu aliyeua kwa kukusudia pasipo mashaka yoyote. Kama umeua wakati unajihami kuna lugha tofauti kisheria wanazotumia wanasheria. Mtu hapewi adhabu ya kifo from the blue.

Endapo mtu anaingia nyumbani mwako na anaua watoto wako kwa kutamba mbele yako, nawe ukapata nafasi ya kujitetea ukamuua, na ushahidi ukaonyesha kabisa kwamba ulikuwa unajaribu kujitetea kunusuru maisha zaidi kupotea, je ni halali au haramu?

Miaka michache pale Mbeya kulikuwa na makundi yenye uongozi kabisa ambao wakivamia nyumba walikuwa wanawafanya vibaya watoto wa kike na wa kiume, wake na waume wakati kila mtu anashuhudia, tena kwa vitisho kuuwawa kama mtu hakubali kufanywa mbaya. Je kama ungekuwa ni wewe ukakuta watu wanawakamata wahuni wale na kuwachoma moto ungewasikitikia ungali msibani kwa watoto wako au hata katika tukio lingine baadaye au hata ukisikia watu wa jinsi ile wanahukumiwa kifo mahakamani?

Kwa akili ya kawaida kiubinadamu si halali kukatisha maisha ya mwingine, lakini wakati mwingine ni halali. Vitani je, askari atahukumiwa kifo kwa kumuua adui?

Hayo ni maswali ninayofikiria kwa uwazi kidogo.

Lekanjobe
 
Lemme ask you a question, will you be for or against kama Ditto angehukumiwa kunyongwa? Maana yeye ni first degree murderer mtu, kama huyu ambaye kwa makusudi kabisa alifanya mauaji ya kikatili unamuweka wapi? Au mtu aliyecharanga mkewe kwa shoka na kuugawa mwili wake kwenye vipande vinne utamuweka wapi? Mtu aliyehukumia kifungo cha miaka 30 kwa mauaji ya kutisha, anatoroka gerezani na kwenda kufanya mauaji mengine ya kutisha akikamatwa afanywe nini? Adhabu ya kifo kwa wengine inafaa! Ukweli ni adhabu ya kikatili lakini haina alternative, wanaotoa adhabu hiyo kwa wengine nao wanastahili kupewa adhabu hiyo kwa mujibu wa sheria.
 
am not defending any sort of crime, but kama intention ni kumrekebisha mtu kumuua siyo suluhu. I opt for life imprisonment. Ninapoongelea hivi si kama sijawahi kuona unyama, nimeina tena kwa ndugu wa karibu kabisa and no matter the criminals intention was i believe akipewa adhabu nyingine, kifungo cha maisha kikiambatana na kazi kama kulima, useremala vitamfaa na vitaongeza tija kwa jamii. Na je mtuhumiwa anapouwawa ndio itamrudusha yule marehemu ambaye yeye anatuhumiwa kumuua?
 
Leo ni siku ya kukemea adhabu ya kifo duniani. Katika jamii zetu kuna wahalifu wengi na wengine ni sugu na wengine tunatamani wauwawe tukiamini kuwa uovu utakoma. Lakini je adhabu ya kifo inamsaidiaje mtuhumiwa aache uovu, je akiuwawa ndio tutakuwa tumelipa ule uovu?? huwa najiuliza sipati jibu, je hiiadhabu ina malengo gani haswa?
Ukipata wasaa wa kuongea na wafungwa waliohukumiwa kunyongwa utapa simamzi ya ajabu, wana msongo, hawana tumaini lolote na wengi hujuta, hujuta sanaa na hutamani wangepewa walau kifungo cha maisha.
...Soma habari hii kisha kama utaingiwa na roho ya imani, wafikirie wazazi, ndugu jamaa na marafiki wa hawa watoto maskini ya mungu.
Posted Date::10/16/2007
Watoto wabakwa hadi kufa, mtuhumiwa mmoja mbaroni
Na Andrew Gasper, Singida

KIJIJI cha Ilongero kilichopo Wilaya ya Singida Vijijini, kimekumbwa na simanzi baada ya watoto wawili wa kike wa familia moja kubakwa na kuingiliwa kinyume na maumbile hadi kufa.

Watoto hao, Twaiba (13) alikuwa anasoma darasa la sita katika Shule ya Msingi Mrama iliyoko tarafa ya Ilongero, wilayani Singida na mdogo wake Zulfa(7) aliyekuwa akisoma wa shule ya chekechea, walikutwa na mkasa huo Jumapili iliyopita wakati wanamwagilia bustani yao ya mboga.

Swedi alisema kabla ya mauaji hayo, majira ya 10:00 jioni siku hiyo, watoto hao walitumwa na wazazi wao kwenda kumwagilia bustani hiyo lakini hawakurudu na kisha miili yao kukutwa kesho yale asubuhi ikiwa imetupwa kwenye shamba la viazi lililopo karibu na korongo hilo.

"Inaelekea watu hao waliwakamata watoto hao kwa nguvu na kuwabeba huku wakiwa wamewakaba koo na kwenda nao kwenye korogo refu la mto uliopo katribu na bustani hiyo," alisema Swedi.

Walipofuatilia nyayo za watu hao hadi kwenye korogo, waligundua kuwa watoto hao walifanyiwa unyama huo kutokana na kukuta viatu (kata mbuga) na suruali ambazo zilibainika kuwa ni mali ya mtu mmoja (jina tunalo) katika eneo hilo vikiwa vimetapakaa kinyesi na damu.

Wakiwa kwenye eneo, walipelekewa taarifa na wenzao kuwa miili ya watoto hao imeonekana kwenye shamba la viazi hatua kama 300 kutoka kwenye korongo hilo.

Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Ilongero, Dk Joyce Kishindo, alisema uchunguzi wao umebaini kuwa watoto hao ambao baba yao ni mlemavu wa miguu, wameharibiwa vibaya sehemu zao za siri.

Mtoto mkubwa walipochunguzwa alibainika kuwa ameharibiwa vibaya sehemu zake zote mbili za siri na viganja vyake vya mikono pamoja na nguo zake zilikuwa na damu nyingi na kinyesi.

Kwa upande wa mdogo wake, alisema kuwa kutokana na udogo wa sehemu zake za siri walimwingia nyuma na kusababisha sehemu yake ya haja kubwa kutoa nje.

Dk Nicolaus Mabula kutoka Singiza mjini aliyeifanyia uchunguzi miili hiyo, alisema kifo Twaiba pia kilichangiwa na kukabwa koo, wakati mdogo inaonyesha kuwa aliinamishwa kichwa chini kwa muda mrefu hadi alipokufa kutokana na kukosa pumuzi.


...kisha 'hukumu' adhabu gani inawafaa hao mafisadi wawili waliofanya unyama huo, kwa mawazo yako adhabu gani inawafaa, kifungo cha maisha (walishwe na kodi yako na yangu, na wakibahatika wapate msamaha wa raisi wakipatwa ama na umri mkubwa, magonjwa yasotibika, nk, au wanyongwe hadharani hadi wafe?

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Celina Kuluba alithibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kwamba hadi juzi jioni walikuwa wanamshikilia mtu mmoja mwenye umri wa miaka 33 (jina tunalo), mkazi wa Kijiji cha Mrama kuhusiana na mauji ya watoto hao.

Kamanda Kaluba, alisema jeshi hilo limeanzisha msako wa kumtafuta mtuhumiwa mwingine aliyetajwa kwa jina moja anayedaiwa kukimbia baada ya kufanya unyama huyo.

Hata hivyo, katika hali ya kushangaza, suruali ya mtuhumiwa huyo ambayo ilikutwa katika eneo la tukio ikihusishwa na tukio hilo, ilitoweka na haijajulikana nani aliyeichukua.

Suruali hiyo ambayo inadaiwa kwamba ilikuwa imetapakaa kinyesi na damu haikuonekana baada ya mganga kutoka mjini Singida kuagiza ichukuliwe ili kuoainisha na vipimo vilivyochukuliwa kwa marehemu hao.
...

...watu kama hawa ndio wanaofaa kunyongwa huku wamening'inizwa kwenye crane, ama kumnyonga kama Barzan Tikriti (kaka'ye Saddam) aishie decapitated!
 
Naona hawa jamaa wawili wanyongwe hadharani ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.wakifungwa wataendelea kufaidi upepo wa mwenyezi mungu bure wakati hawastahili kabisa hawa ni mafisadi wakubwa sana,sio wa kupata msamaha hata kidogo,unapofanya unyama na wewe ufanyiwe unyama, DAWA YA MOTO NI MOTO HAKUNA KUREMBA MAJIBU HAPOHAPO.
 
Aisee yasikitisha na kutia hasira na kinyaa... kwa watu wazima kama hawa wapumbavu kufanya kitu kama hicho... kwani wameshindwa kupata wanawake wa kufanya nao mapenzi? Na kama hawana wapenzi, basi wameshindwa hata kutafuta marafiki? Hakika, Mzungu tena watu kama hao dawa yao wala sio kunyongwa maana wanakufa faster na kwa raha wakiwa wameshatubu (sijui kama wataweza kupewa msamaha). Hawa dawa yao ni kuwakata kiungo kimoja kimoja mpaka afe... kuanzia vidole, viganja, masikio, miguu n.k. Mungu azilaze roho za watoto wale pema peponi... na aifariji familia ile! Doh, inauma sana jamani, imagine wewe ndio watoto wako wamefanyiwa hivyo...
 
n talkin abt adhabu ya kifo...jamani vipi ile kesi ya hili jamaa letu liuaji ambayo ilishafanyiwa usanii na kuitwa kesi ya kuua bila kukusudia?kesi ya Dito.ukiwaona mzuzuri??imeendeleaje?maana me nahisi familia ile ya marehemu ilishapoozwa mambo yameishia chini chini bado wa tz kusahau kabsaa
 
..no matter what..i'm against capital punishment,just give em life and hard work!
 
n talkin abt adhabu ya kifo...jamani vipi ile kesi ya hili jamaa letu liuaji ambayo ilishafanyiwa usanii na kuitwa kesi ya kuua bila kukusudia?kesi ya Dito.ukiwaona mzuzuri??imeendeleaje?maana me nahisi familia ile ya marehemu ilishapoozwa mambo yameishia chini chini bado wa tz kusahau kabsaa

Huyu kwa jinsi mimi nilivyosoma habari kuhusiana na tukio anahitaji kufungwa kifungo cha maisha, minimum miaka 25, lakini si kuuawa. Kwani mazingira ya yeye kutoa bastola na kufyatua yalikuwa ya ugonvi.

SteveD.
 
...Soma habari hii kisha kama utaingiwa na roho ya imani, wafikirie wazazi, ndugu jamaa na marafiki wa hawa watoto maskini ya mungu.


...kisha 'hukumu' adhabu gani inawafaa hao mafisadi wawili waliofanya unyama huo, kwa mawazo yako adhabu gani inawafaa, kifungo cha maisha (walishwe na kodi yako na yangu, na wakibahatika wapate msamaha wa raisi wakipatwa ama na umri mkubwa, magonjwa yasotibika, nk, au wanyongwe hadharani hadi wafe?


...

...watu kama hawa ndio wanaofaa kunyongwa huku wamening'inizwa kwenye crane, ama kumnyonga kama Barzan Tikriti (kaka'ye Saddam) aishie decapitated!

mchongoma, hili nasupport, watumikishwe kuchimba mitaro na kuzibua vyoo kisha wanyongwe!!

SteveD.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom