Ushimen
JF-Expert Member
- Oct 24, 2012
- 37,160
- 85,152
Saudi Arabia ni moja kati ya nchi nne pekee ambazo bado zinatekeleza adhabu ya kifo hadharani. Nchi nyingine ni Iran, Korea Kaskazini na Somalia.
Nchini Saudi Arabia, serikali ya kifalme inatekeleza adhabu hii kwa msimamo kwamba wanatekeleza shari'ah kama ambavyo imeelekezwa katika Qur'an Tukufu.
Hivyo basi ikitokea raia amefanya kosa ambalo linapaswa aadhibiwe kifo, adhabu hii inatekelezwa kwa mtu huyo kuchinjwa hadharani kwa upanga.
Jambo hili limekuwa linaleta shida sana kati ya Saudi Arabia na watu wa haki za binadamu. Kuna makosa ambayo raia wa Saudi Arabia wanachinjwa hadharani ambayo hata wanazuoni wengi wanaamini kwamba hayako sawa kidini bali ni juhudi za Ufalme wa Saudia kuwaziba midomo raia 'vimbele mbele'.
Kwa mfano moja ya utata mkubwa kuhusu adhabu hii ya kifo hadharani ikitokea baada ya polisi wa Saudi Arabia kuwakamata vijana wawili walioitwa Ali al-Nimr na rafiki yake Dawoud al-Marhoon kwa kosa la kuandamana mwaka 2011 kupinga utawala wa Kifalme nchini Saudi Arabia. Kipindi vijana hawa wanakamatwa walikuwa na miaka 17 pekee.
Siku chache baadae alikamatwa muhubiri wa kiislamu maarufu nchini humo kipenzi cha vijana anayeitwa Sheikh Nimr al-Nimr (mjomba wake Ali al-Nimr) kwa kosa la kutoa mawaidha yenye maudhui ya kupinga serikali.
Wote hawa walikamatwa mwaka 2011 na 2012, na mpaka kufikia mwaka 2015 wote walikuwa wamehukumiwa adhabu ya kifo kwa kuchinjwa hadharani.
Hukumu hii iliamsha hasira kubwa ya mashirika ya binadamu mpaka kufikia hatua utekelezaji wa adhabu kwa watuhumiwa hawa watatu ukasogezwa mbele, lakini bado wangali gerezani wakisubiria kuchinjwa siku yoyote ile.
(Sheikh Nimr al-Nimr walichinjwa mwaka jana, January 2, 2016 pamoja na raia wengine 47 kwa pamoja). Lakini kila hii haimaanishi kwamba hakuna watu wanaochinjwa kila siku kwa amri ya serikali ya Saudi Arabia.
Tumezoea kuona vyombo vya habari vikiripoti kuhusu ukatili wa kikundi cha ISIS kutokana na kuwachinja mateka wao wakiwa wanawarekodi, lakini uhalisia ni kwamba serikali ya Saudi Arabia inachinja watu wengi zaidi kuliko ISIS.
Pengine habari za ukatili huu unaotekelezwa na serikali ya Saudi Arabia haukemewi sana kwenye vyombo vya habari kutokana na uswahiba wa serikali hiyo na mataifa ya kimagharibi yakiongozwa na Marekani.
Mfano mwaka 2011 inakadiriwa kuwa watu 26 walichinjwa hadharani.
Mwaka 2013 zaidi ya watu 78 walichinjwa hadharani.
Mwaka 2015 jumla ya zaidi ya watu 158 walichinjwa hadharani.
Mwaka 2016 zaidi ya watu 153 walichinjwa hadharani, ambapo watu 47 kati ya hao walichinjwa kwa pamoja (mass beheading) siku ya January 2, 2016.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nchini Saudi Arabia, serikali ya kifalme inatekeleza adhabu hii kwa msimamo kwamba wanatekeleza shari'ah kama ambavyo imeelekezwa katika Qur'an Tukufu.
Hivyo basi ikitokea raia amefanya kosa ambalo linapaswa aadhibiwe kifo, adhabu hii inatekelezwa kwa mtu huyo kuchinjwa hadharani kwa upanga.
Jambo hili limekuwa linaleta shida sana kati ya Saudi Arabia na watu wa haki za binadamu. Kuna makosa ambayo raia wa Saudi Arabia wanachinjwa hadharani ambayo hata wanazuoni wengi wanaamini kwamba hayako sawa kidini bali ni juhudi za Ufalme wa Saudia kuwaziba midomo raia 'vimbele mbele'.
Kwa mfano moja ya utata mkubwa kuhusu adhabu hii ya kifo hadharani ikitokea baada ya polisi wa Saudi Arabia kuwakamata vijana wawili walioitwa Ali al-Nimr na rafiki yake Dawoud al-Marhoon kwa kosa la kuandamana mwaka 2011 kupinga utawala wa Kifalme nchini Saudi Arabia. Kipindi vijana hawa wanakamatwa walikuwa na miaka 17 pekee.
Siku chache baadae alikamatwa muhubiri wa kiislamu maarufu nchini humo kipenzi cha vijana anayeitwa Sheikh Nimr al-Nimr (mjomba wake Ali al-Nimr) kwa kosa la kutoa mawaidha yenye maudhui ya kupinga serikali.
Wote hawa walikamatwa mwaka 2011 na 2012, na mpaka kufikia mwaka 2015 wote walikuwa wamehukumiwa adhabu ya kifo kwa kuchinjwa hadharani.
Hukumu hii iliamsha hasira kubwa ya mashirika ya binadamu mpaka kufikia hatua utekelezaji wa adhabu kwa watuhumiwa hawa watatu ukasogezwa mbele, lakini bado wangali gerezani wakisubiria kuchinjwa siku yoyote ile.
(Sheikh Nimr al-Nimr walichinjwa mwaka jana, January 2, 2016 pamoja na raia wengine 47 kwa pamoja). Lakini kila hii haimaanishi kwamba hakuna watu wanaochinjwa kila siku kwa amri ya serikali ya Saudi Arabia.
Tumezoea kuona vyombo vya habari vikiripoti kuhusu ukatili wa kikundi cha ISIS kutokana na kuwachinja mateka wao wakiwa wanawarekodi, lakini uhalisia ni kwamba serikali ya Saudi Arabia inachinja watu wengi zaidi kuliko ISIS.
Pengine habari za ukatili huu unaotekelezwa na serikali ya Saudi Arabia haukemewi sana kwenye vyombo vya habari kutokana na uswahiba wa serikali hiyo na mataifa ya kimagharibi yakiongozwa na Marekani.
Mfano mwaka 2011 inakadiriwa kuwa watu 26 walichinjwa hadharani.
Mwaka 2013 zaidi ya watu 78 walichinjwa hadharani.
Mwaka 2015 jumla ya zaidi ya watu 158 walichinjwa hadharani.
Mwaka 2016 zaidi ya watu 153 walichinjwa hadharani, ambapo watu 47 kati ya hao walichinjwa kwa pamoja (mass beheading) siku ya January 2, 2016.
Sent using Jamii Forums mobile app