adhabu ipi 'tamu'?

Mbu

JF-Expert Member
Jan 11, 2007
12,753
7,839
Hivi adhabu gani ya kifo inamfaa 'muuaji sugu', (serial killer)?... i.e mtu kamlawiti/kumnajisi mtoto/kikongwe kisha kamnyonga/kamchinja (victim wake) mpaka kufa nk... ili iwe 'funzo' kwa 'wanaotamani' kuua...?

...apigwe mawe hadi afe, (stoning)

...akatwe kichwa, (beheading)

...anyongwe hadi afe, (hanging)

Imagine;... hangman makes the noose too short a drop that the prisoner 'slowly' strangles, or too long a drop that the prisoner can be decapitated!

...apigwe sindano ya sumu afe, (Lethal injection)

...apigwe shoti ya umeme hadi afe, (Electric chair)

...apigwe risasi hadi afe, (firing squad)

...awekewe gesi ya sumu hadi afe, (poison gas)

kati ya hizo, ipi 'inafaa' sana kwa magereza yetu Tanzania?
 
Tatizo ni kwamba akishakufa hatupati tena muda wa kumsikia na kufahamu alijisikiaje. Kama kweli alijutia kosa au la. Nafikiri mtu kama huyu ahasiwe halafu akatwe mkono mmoja. Tumwache jamii imkejeli,,, hapo ataipata tamu yake!!
 
hivi adhabu gani ya kifo inamfaa 'muuaji sugu', (serial killer)?... i.e mtu kamlawiti/kumnajisi mtoto/kikongwe kisha kamnyonga/kamchinja (victim wake) mpaka kufa nk... ili iwe 'funzo' kwa 'wanaotamani' kuua...?

...apigwe mawe hadi afe, (stoning)

...akatwe kichwa, (beheading)

...anyongwe hadi afe, (hanging)



...apigwe sindano ya sumu afe, (Lethal injection)

...apigwe shoti ya umeme hadi afe, (Electric chair)

...apigwe risasi hadi afe, (firing squad)

...awekewe gesi ya sumu hadi afe, (poison gas)

kati ya hizo, ipi 'inafaa' sana kwa magereza yetu Tanzania?

Bw. Mchongoma,

Vipi tena mzee? Mambo makubwa na yanayotisha haya! Nafikiri yanasisimua kwa kuyaongelea tu!

Anyway, I don't support death penalty. So kwa maoni yangu, adhabu zote hizo hazifai.
 
hivi adhabu gani ya kifo inamfaa 'muuaji sugu', (serial killer)?... i.e mtu kamlawiti/kumnajisi mtoto/kikongwe kisha kamnyonga/kamchinja (victim wake) mpaka kufa nk... ili iwe 'funzo' kwa 'wanaotamani' kuua...?

...apigwe mawe hadi afe, (stoning)

...akatwe kichwa, (beheading)

...anyongwe hadi afe, (hanging)



...apigwe sindano ya sumu afe, (Lethal injection)

...apigwe shoti ya umeme hadi afe, (Electric chair)

...apigwe risasi hadi afe, (firing squad)

...awekewe gesi ya sumu hadi afe, (poison gas)

kati ya hizo, ipi 'inafaa' sana kwa magereza yetu Tanzania?

Mi naona kipimo ambacho huyo mpimaji kawapimia wenzie nae apimiwe hicho hicho, ila cha kwake kishindiliwe na kusukwasukwa. Kufuta adhabu ya kifo ndio kunafanya madhambi haya yazidikila uchao. Naweza kukosolewa kwa hili, ila naunga mkono adhabu ya kifo.
 
hivi adhabu gani ya kifo inamfaa 'muuaji sugu', (serial killer)?... i.e mtu kamlawiti/kumnajisi mtoto/kikongwe kisha kamnyonga/kamchinja (victim wake) mpaka kufa nk... ili iwe 'funzo' kwa 'wanaotamani' kuua...?

...apigwe mawe hadi afe, (stoning)

...akatwe kichwa, (beheading)

...anyongwe hadi afe, (hanging)



...apigwe sindano ya sumu afe, (Lethal injection)

...apigwe shoti ya umeme hadi afe, (Electric chair)

...apigwe risasi hadi afe, (firing squad)

...awekewe gesi ya sumu hadi afe, (poison gas)

kati ya hizo, ipi 'inafaa' sana kwa magereza yetu Tanzania?

Mimi nadhani badala ya kujadili adhabu gani inafaa kwa watu hawa,tuanze kujadili kama adhabu ya kifo iendelee kutumika hapo Tanzania ama iondolewe.Mimi nafikiri muda na wakati muafaka wa kuifuta adhabu ya kifo "Death Penalty or Capital Punishment" kwenye nchi yetu ndo huu.Tusijirudishe nyuma,tujisogeze mbele.Adhabu ya kifo mimi sikubaliani nayo na wala siungi mkono nchi yoyote ile duniani inayotekeleza hii adhabu.
 
Bw. Mchongoma,

Vipi tena mzee? Mambo makubwa na yanayotisha haya! Nafikiri yanasisimua kwa kuyaongelea tu!

Anyway, I don't support death penalty. So kwa maoni yangu, adhabu zote hizo hazifai.

...QM, ha ha ha... unajua matendo ya ubakaji watoto yamekuwa yakiongezeka siku hadi siku, au labda ndio uhuru wa vyombo vya habari? ...

Mimi nadhani badala ya kujadili adhabu gani inafaa kwa watu hawa,tuanze kujadili kama adhabu ya kifo iendelee kutumika hapo Tanzania ama iondolewe.Mimi nafikiri muda na wakati muafaka wa kuifuta adhabu ya kifo "Death Penalty or Capital Punishment" kwenye nchi yetu ndo huu.Tusijirudishe nyuma,tujisogeze mbele.Adhabu ya kifo mimi sikubaliani nayo na wala siungi mkono nchi yoyote ile duniani inayotekeleza hii adhabu.

...sawa Mkuu, ila ukisoma hii habari, unadhani huyo 'mtuhumiwa' sugu adhabu gani inamstahili, gerezani keshapazoea!

wanafunzi wawili wafa kwa kubakwa

na Jumbe Ismailly, Singida

MWANAFUNZI wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Mrama, iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Singida na mdogo wake aliyekuwa akisoma shule ya awali katika shule hiyo, wamefariki dunia baada ya kubakwa na kulawitiwa na watu wasiojulikana.

Wanafunzi hao wametajwa kuwa ni Twaiba Athumani (13) anayesoma darasa la sita na Zulfa Athumani (7), aliyekuwa akisoma shule ya awali.

Akizungumzia tukio hilo jana, baba wa watoto hao, Athumani Jumanne, alisema tukio hilo lilitokea juzi, kati ya saa 12 jioni na 2 usiku, umbali wa kilomita takriban mbili kutoka nyumbani kwake, kwenye eneo la shamba la viazi la mkazi mmoja wa kijiji hicho.

Alisema kabla ya tukio hilo watoto hao walitoka nyumbani majira ya saa 10:30 jioni kwenda kisimani kuchota maji kwa ajili ya kufulia nguo na kwamba mpaka inafika saa 2 usiku walikuwa hawajarudi.

“Mpaka saa mbili asubuhi walikuwa hawajarudi...ilibidi tuwafuatilie hadi kwenye eneo lililokuwa na korongo na ndipo tulipookota kiatu cha tairi cha mtuhumiwa mmoja na tulipoendelea kufuatilia hadi kwenye shamba la viazi ndipo tulipoikuta miili ya marehemu ikiwa imetapakaa vinyesi na damu.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji, Issah Swedi, alisema mtuhumiwa Mile aliyetoroka inasemekana alitoka gerezani hivi karibuni baada ya kumaliza kutumikia kifungo kwa makosa ya ubakaji na kwamba amekuwa na uzoefu wa kuishi gerezani kuliko uraiani.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ilongero, Greace Kishindo, alithibitisha kupokea maiti hizo huku zikiwa zimetapaa damu na vinyesi.
 
Ushirikina waimarisha ubakaji watoto na vikongwe

2005-07-20 10:02:40
Na Renatus Masuguliko, Mwanza

Matukio ya kihalifu ya ubakaji wa watoto na wanawake vikongwe, yanaendelea kutokea nchini ambayo baadhi kuhusihwa na imani za kishirikina, yana athari mbaya kwa waathirika, hata kuvuruga mifumo ya maisha yao, ikiwa ni pamoja na kuwachanganya kisaikolojia na kuwaambukiza magonjwa mbalimbali yakiwemo ukimwi.
Makala hii ya Mwandishi
Jacqueline Mosha yajadili suala hilo.

Tabia ya baadhi ya vijana na watu wazima kubaka wazee (vikongwe), kunajisi na kulawiti watoto wadogo,taratibu inageuka kuwa kama mtindo wa maisha ya jamii yetu.

Matukio hayo, kwa kiasi kikubwa yanachangia kusababisha matatizo ya kisaikolojia kwa waathirika, kukatisha tamaa, kujichukia, kutojiamini na uoga.

Sababu mbalimbali umetajwa kuchangia tatizo hilo. Baadhi ya watu kudai kuwa ni kukithiri kwa vitendo vya imani za kishirikina. Na wengine wanasema ni matokeo ya uhalifu wa kutumia dawa za kulevya au tamaa za kufanya ngono zisizodhibitiwa.

Hakimu Mfawidhi wa wilaya ya Nzega, Ancient Rutechura, aliwahi kukaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa ''washitakiwa wengi wa kesi za kubaka na kunajisi hufungwa vifungo vya maisha.Hadi sasa kuna kesi 37 zilizoripotiwa katika mahakama za Wilaya ya Nzega kwa kipindi cha mwaka huu''.

Hakimu huyo, aliongeza kuwa washitakiwa wengi wanaofikishwa mahakamani kwa kesi za ubakaji, hudai kuwa wameambiwa na waganga wa kienyeji wabake watoto wadogo na wazee ambao hawapati hedhi.

Katika kutekeleza ushauri wa waganga wa kienyeji,watu hao hujikuta wakibaka wazee au watoto ili kuhakikisha kuwa mambo yao yanawanyookea kwa kupata fedha au mifugo mingi.

...takwimu nazo zinasemaje;...

Kumbukumbu zinaonyesha kuwa, kwa miaka mitatu kuanzia mwaka 2000/ 2002 kesi za ubakaji na ulawiti wa watoto na wanawake zipatazo 97 ziliripotiwa kwa wastani nchini tangu sheria ya ubakaji ya mwaka 1998 ianze kutumika.

Kesi za ubakaji zilizoripotiwa katika vyombo vya Sheria hapa nchini, utafiti unaonyesha kuwa wengi wa watuhumiwa ni vijana wenye rika la kati ya miaka 18 hadi miaka 30.

Utafiti umebainisha kuwa, kesi za ubakaji ziliongezeka mara mbili katika mikoa wa Pwani tangu Sheria ya mwaka 1998 ianze kutumika.

Aghalabu, kati ya kesi 245 za ubakaji zilizotokea katika Pwani mnamo mwaka 1996, ni kesi 120 tu ndizo zilizoripotiwa kwenye vyombo vya kisheria baada ya kupitishwa kwa sheria ya kuzuia ubakaji. Pia kati ya mwaka 1996 -1997 kuliripotiwa kesi 50 tu za ubakaji na mwaka 1998 - 1999 kesi 120 ziliripotiwa katika vyombo vya Sheria.

Kwa upande wa mkoa wa Dar-es Salaam,utafiti umebainisha kuwa uliongoza kwa kuwepo vitendo vingi vya ubakaji ambapo kesi 515 ziliripotiwa.

Kadhalika mkoa wa Dodoma ulikuwa na kesi za ubakaji zaidi ya 9,000 zilizoripotiwa kwa muda wa miaka mitatu kuanzia mwaka 1999 mpaka mwaka 2001.

Takwimu zinaonyesha kuwa, mwaka 1999 mkoa wa Dodoma ulikuwa na kesi 2,659 za ubakaji zilizoripotiwa, wakati mwaka 2000 kesi 3,116 na mwaka 2001 kesi 3,444 ziliripotiwa.

Utafiti pia umebaini kuwa,mkoa wa Mbeya uliripotiwa kuwa wa pili kwa kuwa na idadi kubwa ya vitendo vya ubakaji nchini mwaka 2001, huku kesi 366 za ubakaji zilizoripotiwa katika vyombo vya sheria.

Mkoa wa Kagera kwa mujibu wa takwimu, uliripotiwa kuwa wa tatu, kwa kuwa na idadi kubwa ya vitendo vya ubakaji mwaka 2001. Kesi 277 ziliripotiwa katika vyombo vya Sheria.

Zanzibar imeripotiwa kuwa ya mwisho kwa kuwa na idadi ndogo ya vitendo vya ubakaji ambapo kesi 23 tu ziliripotiwa.
 
Mimi nadhani badala ya kujadili adhabu gani inafaa kwa watu hawa,tuanze kujadili kama adhabu ya kifo iendelee kutumika hapo Tanzania ama iondolewe.Mimi nafikiri muda na wakati muafaka wa kuifuta adhabu ya kifo "

Nakubaliana nawe Brown..Capital punishment should be abolished is against humanity, kama hatuwezi tutengeneza uhai basi tusiutoe kwa namna yeyote ile.. adhabu kubwa iwe kifungo cha maisha ....ama miaka mingi jela ie 30-50 hivi
 
kama hamna adhabu inayostahili, Mob justice kama hii itakuwa 'kama kawaida'!...

Posted Date::9/26/2007
Wanakijiji wamuua mwenzao kwa madai ya ubakaji
Na Yusuf Dai, Babati

MKAZI wa Kijiji cha Singe wilayani hapa Mkoa wa Manyara, Jumanne Abdallah (20), ameuawa na wenzake kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa darasa la tatu.Jumanne aliuawa Septemba 22 majira ya jioni katika shamba lake.

Ilidaiwa kuwa, wakati akichunga ng'ombe wake kwenye shamba hilo, wanafunzi watatu wa Shule ya Msingi Gendi walifika shambani hapo na kuanza kuokota mbaazi zilizodondoka baada ya kuvunwa.

Iliendelea kudaiwa kuwa, jambo linaloelezwa kuwa baada ya Jumanne kuwaona, aliwafukuza wanafunzi hao na kumkamata ambaye sweta lake lilinasa kwenye mti.

Ilidaiwa kuwa, baada ya mwanafunzi huyo kuanguka, Jumanne alimkamata na kumbaka.

Wanafunzi waliokimbia walifika kijijini na kutoa taarifa ya kukamatwa kwa mwenzao, ndipo wanakijiji wakatoka kwenda kufuatilia tukio hilo.

Ilidaiwa kuwa, walipofika shambani hapo, walimkuta mwanafunzi huyo akitambaa kwa magoti kutokana na maumivu huku akiwa ametapakaa damu kwenye mapaja.

Wakati huo, Jumanne alikuwa amekimbia na ndipo baadhi ya wakazi wa kijiji hao, walimchukua mwanafunzi huyo na kumpeleka katika Hospitali ya Wilaya ya Babati kwa matibabu.

Mwanafunzi huyo baada ya kufanyiwa uchunguzi katika hospitali hiyo, alihamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro ya KCMC kwa matibabu kutokana na kujeruhiwa vibaya.

Habari kutoka kwa ndugu wa mtoto huyo zinadai kuwa, hali yake bado si nzuri kwa kuwa hawezi kuzungumza na tumbo lake limevimba.

Wakati mwanafunzi huyo akiendelea na matibabu KCMC, wakazi wa kijiji hicho, waliendelea kumsaka Jumanne na kumkamata nyumbani kwake.

Wanakijiji hao, walimpeleka hadi shuleni ambako wanafunzi wawili waliokimbia baada ya kuwakimbiza, walimthibitisha kuwa ndiye aliyembaka mwenzao.

Baada ya wanafunzi hao kumtambua, wanakijiji hao waliondoka naye kwa lengo la kumpeleka Kituo cha Polisi cha Babati. Hata hivyo, njiani walianza kumshambulia kwa kipigo na kufia Hospitali ya Wilaya muda mfupi baada ya kufikishwa kwa matibabu.
 
Nakubaliana nawe Brown..Capital punishment should be abolished is against humanity, kama hatuwezi tutengeneza uhai basi tusiutoe kwa namna yeyote ile.. adhabu kubwa iwe kifungo cha maisha ....ama miaka mingi jela ie 30-50 hivi

...Mkuu Ushirombo, kwa mazingira ya magereza yetu, unategemea atapata 'fundisho' kwa kosa alilofanya? fikiria kama huyu;

Mwenyekiti wa Kijiji, Issah Swedi, alisema mtuhumiwa Mile aliyetoroka inasemekana alitoka gerezani hivi karibuni baada ya kumaliza kutumikia kifungo kwa makosa ya ubakaji na kwamba amekuwa na uzoefu wa kuishi gerezani kuliko uraiani

...alishamaliza kutumikia kifungo huyo, halafu kawabaka na kuwalawiti wale watoto mpaka kawaua! huyo unatarajia kifungo kitamsaidia nini?

mimi naona anafaa kupigwa nyundo kwenye korodani zake mpaka afe!!!
 
Wale wote wanaopinga adhabu ya Kifo aidha wanategemea au wana hofu kuwa kuna siku wanaweza kubaka au kuuwa kwa kukusudia. Kwao wanaona ni bora ukibaka au ukiuwa kwa kukusudi, jamii ikuonee huruma na kukumbatia kwa machafu na dhurma uliyoifanya...! je unaweza kupima adhari anayopata m'bakwaji.. au adhari anayopata mfiwa kwa kufiwa na Baba, Mama au mtoto...?!

Umepoteza uhai wa mtu kwa kumuondolea uhai wake au umebaka kwa tamaa zako za mwili, kisha unategemea ukale na kulala bure JELA huku ukilindwa na kupewa matibabu kila inapobidi...!?

Je wewe ukibakwa au kupoteza Mtoto au Dada, au Mke na kisha hukumu ikapitishwa kuwa muuwaji amefungwa miaka 10 jela na baada ya kutumikia miaka 6 akapewa parole na yupo mtaani anaendelea na maisha utafanya nini?
Fikiri kabla ya kujibu, siku moja unaweza kuwa Mhanga wa kubakwa... au unataka ukipigwa shavu hili ugeuze na la pili?
 
Mimi nadhani badala ya kujadili adhabu gani inafaa kwa watu hawa,tuanze kujadili kama adhabu ya kifo iendelee kutumika hapo Tanzania ama iondolewe.Mimi nafikiri muda na wakati muafaka wa kuifuta adhabu ya kifo "Death Penalty or Capital Punishment" kwenye nchi yetu ndo huu.Tusijirudishe nyuma,tujisogeze mbele.Adhabu ya kifo mimi sikubaliani nayo na wala siungi mkono nchi yoyote ile duniani inayotekeleza hii adhabu.
huwezi kujua uzito wa jambo mpaka liwe limekupata. mungu akuepushie mbali.ila jaalia una mwanao au mke,au mama kipenzi na akaja jamaa akamtoa roho mbele ya macho yako huku unaangalia ,aidha kwa kumchinja au kumbaka au namna yeyote ile. je zungumza kiukweli kabisa . kipi kitakata kiu ya kisasi chako?. nadhani hata akiuliwa basi utaona haijatosha. unasema unayoyasema kwasababu halijakukuta wewe, hivyo , "mzigo wa mwenzio unauona kanda la usufi".
 
Atupwa jela maisha kwa kulawiti

2007-06-25 09:03:35
Na Jumbe Ismailly, Singida

Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida, imemuhukumu kijana mmoja kutumikia kifungo cha maisha jela, baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti binti mwenye umri wa miaka mitano.

Aliyehukumiwa ni Tumaini Moses (23), maarufu kwa jina la Kisigi, mkazi wa Kijiji cha Ngamu wilaya ya Singida Vijijini.

Baada ya Hakimu wa Mahakama hiyo, Bw. John Chaba, kutoa hukumu hiyo, kijana huyo aliangua kilio na kusababisha Mahakama hiyo kusimamisha shughuli zake kwa muda.

Hivi kweli Hakimu unanihukumu kwenda jela maisha? Hunionei huruma hata kidogo?
alisikika akilia kijana huyo.

Awali, Mwendesha Mashtaka Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Bw. Phillipo Mzirai, alidai kuwa Oktoba 2 mwaka jana katika Kijiji cha Ngamu Singida Vijijini, mshtakiwa huyo alimwingilia kimwili binti mwenye umri wa miaka mitano na kumharibu vibaya sehemu zake za siri.

Mziray alidai kuwa siku hiyo ya tukio, mama wa binti huyo Fatuma Jumanne, alikuwa anatoka msikitini na kusikia mtoto wake akilia kwa sauti kubwa. Ndipo alipokimbia kwenda kujua kilichokuwa kikimsibu mwanaye.

Baada ya kufika nyumbani kwake na kuingia chumbani, alimkuta mshtakiwa akiendelea kumwingilia binti yake kimwili.

Bw. Mziray alidai Bi. Fatuma alichukua fimbo na kumchapa kwa nguvu mshtakiwa huyo mgongoni.

Kutokana na kipigo hicho, mshtakiwa alimwachia binti huyo na kufunga zipu yake na kukimbia.

Baadaye mtu huyo alikamatwa na kufikishwa kituo kidogo cha polisi cha Kijiji cha Ngamu.

...kifungo cha maisha Bw Kisigi anaona hakimu anamuonea! yeye alipokuwa 'kamkunja' binti wa miaka mitano na kilio chote kabinti hako kalivyokuwa kanaugulia maumivu kwa 'kuchanwa chanwa' sehemu zake za siri...

imagine; uchungu, na woga ulokuwa umemkabili huyo binti maskini!

...inaelekea 'asingefumwa' angekatoa roho hako kabinti kupoteza ushahidi, na DNA testing ilivyo 'ghali' kwa forensic examination Bongo... labda Bw Kasigi angeendelea 'kutesa' tu mtaani!

huyu adhabu ambayo ingemfaa ni ile ya 'kutwangwa' mawe hadi afe!
 
Mama na mwana watoa ushahidi dhidi ya Nguza

...lakini twendeni mbele tukirudi nyuma, hivi ni kweli Babu Seya na wanawe wote walikuwa na haka kamtindo wajemeni?... au 'ushahidi haukutosha'?

2003-12-17 23:13:38
Na Agnes Shayo

Mtoto na mama yake, jana walitoa ushahidi katika kesi ya kulawiti na kuwabaka wanafunzi wa shule ya msingi inayomkabili mwanamuziki maarufu Nguza Viking na watoto wake watatu.

Hao walikuwa ni mashahidi wa 12 kutoa ushahidi wao tangu kuanza kwa kesi hiyo.
Hata hivyo, majina ya mama na mtoto waliotoa ushahidi huo, hayakufahamika.

Kesi hiyo inasikilizwa mbele ya Hakimu Eddy Lyamuya wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kwamba itaendelea tena leo mahakamani hapo ambapo upande wa mashtaka utaendelea na mashahidi wengine.

Washtakiwa katika kesi hiyo ni Nguza Viking (50) na watoto wake Papi Kocha (22), Nguza Mbanga (27) na Francis Nguza (17).

Pia mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni mwalimu Sigirinda Ngomboka (47).

Ilidaiwa kuwa, kati ya Septemba na Oktoba, mwaka huu, huko Sinza ‘B' nyumba namba 607, washtakiwa waliwabaka na kuwalawiti wanafunzi wenye umri wa kati ya miaka sita na minane isivyo halali kwa kusaidiwa na mwalimu Sigirinda.

Upande wa mashtaka unategemea mashahidi 25 katika kesi hiyo.

...hawa wamefungwa maisha vile?

...halafu Mzee Maumba fundi cherahani wa Ilala yeye alifungwa miaka 30? yuko wapi, au keshakufa!?
 
...Mimi nafikiri muda na wakati muafaka wa kuifuta adhabu ya kifo "Death Penalty or Capital Punishment" kwenye nchi yetu ndo huu.Tusijirudishe nyuma,tujisogeze mbele.Adhabu ya kifo mimi sikubaliani nayo na wala siungi mkono nchi yoyote ile duniani inayotekeleza hii adhabu.

Nakubaliana nawe Brown..Capital punishment should be abolished is against humanity, kama hatuwezi tutengeneza uhai basi tusiutoe kwa namna yeyote ile.. adhabu kubwa iwe kifungo cha maisha ....ama miaka mingi jela ie 30-50 hivi

...sawa wakuu, lakini mnaposoma habari kama hii;

Utajiri! Denti auawa kisa? Pesa

2007-11-16 19:35:04
Na Mwandishi Wetu, Bunda

Tukio hilo la kinyama linadaiwa kutokea pale katika kijiji cha Kaburabura, mishale ya saa 1:45 usiku jana.

Inaelezwa kuwa baada ya wauaji kukamilisha kazi yao ya kumcharanga mapanga binti huyo na kumtoa roho, walimkata mguu wa kulia na viungo vingine kadhaa kabla ya kuondoka zao.

Namna ilivyokuwa, wasimuliaji wanasema kuwa wauaji walivamia nyumba anayoishi binti huyo (albino) na kumkuta akipata chakula cha jioni na wazazi wake.

Wanasema baada ya wauaji waliokuwa zaidi ya wanne kutinga nyumbani kwa binti huyo, walianza kutembeza mapanga na kutaka kuondoka na binti huyo.

Inaelezwa zaidi kuwa baada ya kuona hivyo, baba wa mtoto huyo aitwaye Daudi Masatu akajaribu kupambana nao bila mafanikio.

Wanasema alipozidiwa kwa kurushiwa mapanga mfululizo, baba huyo akaamua kutimua mbio. Baada ya hapo, wanasema mama wa binti huyo, Muhujo Mwenura, naye akajaribu kuokoa maisha ya binti yake huyo albino kwa kuanza kupambana na wavamizi.

Hata hivyo, inaelezwa kuwa mama huyo alizidiwa kama mumewe baada ya kufyekwa vidole vitatu vya mkono kwa panga.

Mashuhuda ambao baadhi ni majirani wa eneo la tukio, wamesema baada ya kuwashinda baba na mama wa binti huyo, wauaji wakatimiza dhamira yao kwa kumcharanga mapanga ya kichwa binti huyo albino, kisha alipoishiwa nguvu wakamkata mguu wake wa kulia na kuondoka nao.

``Walimuacha akitapatapa kwa maumivu huku akivuja damu muda mfupi baadaye, binti akafariki dunia na kuacha msiba mkubwa,`` akasema mmoja wa wasimuliaji wa tukio hilo.

...hamuoni haja ya adhabu 'inayostahili' kwa wauaji walofanya ukatili huu ni kifo tu?
 

...nahitimisha;


2007-11-17 14:48:08
Na Emmanuel Lengwa, Dodoma

...Kuhusu kufuta adhabu ya kifo, Dk. Nagu amesema adhabu ya kifo bado ni adhabu halali kwa Tanzania.

Hata hivyo, amesema ili kujiridhisha kama bado adhabu hiyo inafaa kwa wakati huu, Serikali imeiagiza Tume ya Kurekebisha Sheria kupata maoni ya wananchi walio wengi ili kuona kama jamii bado inaihitaji.

Amesema Serikali itafanya tathimini kama kwa sasa ni wakati muafaka wa kuifuta adhabu hiyo baada ya kupokea matokeo ya utafiti.

...bado naamini hukumu ya kifo bado inastahili Tanzania haswa kwa kuzingatia jinsi vitendo vya mauaji baada ya ubakaji, kama 'vinavyoripotiwa', vinazidi kuongezeka haswa 'victims' ambao wengi wao ni watoto wadogo na vikongwe.

Mbaya zaidi, vitendo hivyo vina'rutubishwa' zaidi kutokana na imani potofu za ushirikina ikiwemo 'kujiongezea' bahati ama 'kujiponya' UKIMWI!!
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom