Adha ya Usafiri Dar Jioni inatatulika

Kamende

JF-Expert Member
Mar 1, 2008
416
45
Wakuu heshima kwenu.

Nimelazimika kuja na hoja ya kuitaka serikali ichukue hatua za kukusudia kuwasaidia wafanyakazi wanaotoka maofisini jioni ili wafike majumbani kwa kwa wakati. Hebu fikiria mtu anatoka Posta saa 12 jioni na kwa vyovyote atafika Kiluvya saa 4 usiku ama saa 5 on busiest days.

Asubuhi kuna kanafuu kutokana na malori kuzuiliwa kutoka mjini.

Wakuu mnaonaje kama tukiishauri serikali kwamba jioni kuanzia saa 11 jioni hadi saa 3 kamili usiku malori yasiruhusiwe kutoka jijini kwenda Chalinze as malori hayo ndo yanayochangia sana kuchelewesha safari za wafanyakazi kurudi majumbani kupitia barabara ya Morogoro?. Lori likipanda kwenye tuta linachukua dakika mbili nzima kumaliza kulipita, nk.

Naomba kuwasilisha.
 
Wenye hayo malori unayotaka yacheleweshwe unawajua?, unataka mattata weye. Wenyewe wakihoji nani kaanzisha hii tafrani JF itampa ushirikiano- ole wako.
 
Hilo wazo zuri sana lakini wenyewe hawasikii / hawajui na Mnyika hapokei simu siku za hivi karibuni.
 
watandaze reli tu si nilisikia kuna mpango huo umefika wapi?
Wakuu heshima kwenu.

Nimelazimika kuja na hoja ya kuitaka serikali ichukue hatua za kukusudia kuwasaidia wafanyakazi wanaotoka maofisini jioni ili wafike majumbani kwa kwa wakati. Hebu fikiria mtu anatoka Posta saa 12 jioni na kwa vyovyote atafika Kiluvya saa 4 usiku ama saa 5 on busiest days.

Asubuhi kuna kanafuu kutokana na malori kuzuiliwa kutoka mjini.

Wakuu mnaonaje kama tukiishauri serikali kwamba jioni kuanzia saa 11 jioni hadi saa 3 kamili usiku malori yasiruhusiwe kutoka jijini kwenda Chalinze as malori hayo ndo yanayochangia sana kuchelewesha safari za wafanyakazi kurudi majumbani kupitia barabara ya Morogoro?. Lori likipanda kwenye tuta linachukua dakika mbili nzima kumaliza kulipita, nk.

Naomba kuwasilisha.
 
Hilo wazo zuri sana lakini wenyewe hawasikii / hawajui na Mnyika hapokei simu siku za hivi karibuni.
 
ni wazo zuri (kwako) ila sio zuri (kwao) pia ni wazo la muda mfupi kama ngeleja na umeme wa megawatts 100 wakati nchi inamahitaji ya umeme megawatts 20,000 by 2040.... rudi kajipange uje na suluhisho la matatizo ya usafiri kwa majiji ya tanzania (sio dsm tu) ili tukae vizuri na kwa furaha mpaka 2050... inaweza kuwa nano-science kwako ila ukweli ndo huo...do ur assignment as a grown up... NI MAONI TUU NOTHING PASONO
 
Back
Top Bottom