Adha tunazopata mitaani kwa matangazo kwa kupitisha magari ya Ma-Speaker makubwa kwa kupaza sauti

BigBros

JF-Expert Member
Feb 12, 2014
1,238
630
Kila mwanachi anastahili kupata utulivu nyumbani kwake. Hiyo ni haki ya msingi kwa kila raia. Mbali ya hayo wengine tuna wazee wenye matatizo mbali mbali, wengi wao wanahitaji utulivu majumbani mwao. Pia wengine tunawatoto wachanga, kina mama wajawazito etc etc.

Kelele za aina yoyote hazipaswi kufanyika katika maeneo waishio watu. Haijalishi ni matangazo ya nini. Hata kama ni matangazo muhimu kama vile dini, basi haipaswi kupita mitaani kupasua masikio yetu na nyimbo za dini kwa kisingizio cha Mungu. Mwenye kutaka kusikia hayo aende kanisani au misikitini. Sio haki kusumbua watu kwa kisingizio cha dini. Hata Mungu hapendi uwe msumbufu kwa wengine. Kama kweli wewe ni mtu wa Mungu basi hupaswi kuwa msumbufu kwa wengine.

Jambo la kushangaza hawa watu wanapewa vibali na watumia vibali hivyo kuwa adha kubwa kwa wananchi.

Tunaomba Serikali ya Awamu ya 5 ilichukulie hili jambo kwa karibu na kudhibiti utoaji wa vibali kiholela. Utulivu wa wananchi upewe kipaumbele na uzingatiwe.

Asanteni.View attachment New saved.mp4

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi nachukia matangazo ya pedi kwenye taarifa ya habari(hasa itv),ukiwa na dada,mama shangazi au ndugu yeyote wa kike huwa natafuta ardhi yakunimeza...anyway hata hayo maspeaker yanaboa
 
Hahahaha, yeah ni kweli lakini hiyo TV una option ya kabadilisha Channel au hata kuizima ukiona yaonyesha mambo kinyume na maadili. Lakini hilo la kupitisha gari la mziki unalazimishwa kusikiliza hayo matangazo kwa nguvu hata kama hutaki au huna hali ya kusikiliza. Kila mtu afanye mambo yake bila kumkera mwengine. Hili jambo viongozi wetu wa Serikali za mitaa wanatakiwa wawe wasimamizi wa haki sawa kwa kila mtu. Kwa kweli hawafanyi hivyo. Huo ndiyo kweli. Hivi vitu wanaona lakini hawajali. Tunawalalamikia lakini hawafanyi chochote. Wao wenyewe ndio wanatoa vibali. Hawa jamaa wanapiga huo mziki tokea asubuhi hadi jioni. Ni adha ya siku nzima.

Kisayansi hizo kelele tunasema zinasababisha Noise Pollution. Ina sababisha stress ya hali ya juu. Ni uchafuzi wa mazingira kama vile utupaji taka. Mtu akitupa taka kinyume na sheria ni lazima akamatwe basi na hizo kelele ni uchafuzi wa mazingira.

Nchi zilizoendelea huwezi kuona upuuzi huu. Mambo haya yapo baadhi ya nchi za kiafrica tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani hao wana baraka za Serikali ya mitaa. Kibaya zaidi Huwezi kuwafanya chochote. Watakuonyesha kibali chao. Suala linakuja, wanapewaje vibali???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
matangazo haya ni moja vyanzo vya mapato kwa serikali husika,wao ndio wanaotoa vibali na vibali hivi vinakuja na sheria zake kama ;muda wa matangazo,eneo lengwa,na kikubwa zaidi kiwango cha sauti ya matangazo yenyewe ni muhimu kiwe ndani kisheria,ila kwa sababu tunaishi in a shithole country kila mtu anajifanyia analotaka,na mkuu hapo juu kuhusu matangazo ya sanitations pads nimeshindwa kabisa kukuelewa,tatizo ni nini kuona pad?na please mkuu anza kuchangia hizi sanitation pads kwa dada zetu na mama zetu.
 
Mkoa wa pwani ndio balaa. Msagasumu kama amealikwa kwenye bar fulani. Basi siku tatu kabla makirikuu na wasichana wanaomwaga razi yaani wacheza uchi. Si mijispika hiyo. Siyo sauti hiyo. Siyo miziki hiyo. Natamani nihamie Buguruni labda kumetulia
 
mimi natumia enjoys pedi wewe je? bora hata maspika ila sio matangaza ya tv na radio za bongo siku hizi
 
matangazo haya ni moja vyanzo vya mapato kwa serikali husika,wao ndio wanaotoa vibali na vibali hivi vinakuja na sheria zake kama ;muda wa matangazo,eneo lengwa,na kikubwa zaidi kiwango cha sauti ya matangazo yenyewe ni muhimu kiwe ndani kisheria,ila kwa sababu tunaishi in a shithole country kila mtu anajifanyia analotaka,na mkuu hapo juu kuhusu matangazo ya sanitations pads nimeshindwa kabisa kukuelewa,tatizo ni nini kuona pad?na please mkuu anza kuchangia hizi sanitation pads kwa dada zetu na mama zetu.
Yawezekana kuwa ni chanzo cha mapato ya Serikali. Lakini Serikali hiyo hiyo inavyanzo vingi mno vya mapato kushinda kutumia njia hii ambayo kwanza ni usumbufu kwa wananchi na la pili hakuna kipato significant kinachopatikana hapo kiasi kwamba Serikali isisjali wananchi wake.

Kama tukitazama kwa mtazamo wa mapato ya Serikali basi wangehalalisha ulimaji wa Mirungi haidaru na Kilimanjaro kwani inakipato kikubwa kwa Taifa kushinda hayo matangazo. Kama vyanzo vyote vya mapato ya Serikali haikutosheleza mahitaji basi hayo makelele ya maspika hayatasaidia chochote zaidi ya kuwabughudhi wananchi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jitahidi tu kuzoea mkuu. Vuta picha Mungu akijalia uzima 2020 wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani hali itakuwaje ya hayo matangazo!!!
 
Jitahidi tu kuzoea mkuu. Vuta picha Mungu akijalia uzima 2020 wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani hali itakuwaje ya hayo matangazo!!!
Hayo yote ni makosa ambayo hayapaswi kufanyika mitaani. Yafanywe uwanjani au Mahala maalum bila ya kuwa kikwazo kwa wananchi.

Mabadiliko haya yatafanywa iwapo sisi wananchi tutaonyesha na kushikamana kwa kulipigia kelele hili jambo. Ikiwa tutakaa kwa mentality ya kuwa tuvumilie basi hatutaweza kupata utulivu tunaostahiki kupata.

Umoja ni nguvu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yawezekana kuwa ni chanzo cha mapato ya Serikali. Lakini Serikali hiyo hiyo inavyanzo vingi mno vya mapato kushinda kutumia njia hii ambayo kwanza ni usumbufu kwa wananchi na la pili hakuna kipato significant kinachopatikana hapo kiasi kwamba Serikali isisjali wananchi wake.

Kama tukitazama kwa mtazamo wa mapato ya Serikali basi wangehalalisha ulimaji wa Mirungi haidaru na Kilimanjaro kwani inakipato kikubwa kwa Taifa kushinda hayo matangazo. Kama vyanzo vyote vya mapato ya Serikali haikutosheleza mahitaji basi hayo makelele ya maspika hayatasaidia chochote zaidi ya kuwabughudhi wananchi.

Sent using Jamii Forums mobile app
nakubaliana nawe mkuu,tatizo hapa ni utekelezaji mbovu,sharia zipo wazi kwani zinaelezea muda wa tangazo,eneo lengwa,na kipimo cha sauti wakati tangazo linapita mtaani,(na hii inahusu vilevile kumbi za starehe zilizo kwenye makazi).
 
nakubaliana nawe mkuu,tatizo hapa ni utekelezaji mbovu,sharia zipo wazi kwani zinaelezea muda wa tangazo,eneo lengwa,na kipimo cha sauti wakati tangazo linapita mtaani,(na hii inahusu vilevile kumbi za starehe zilizo kwenye makazi).
Cha ajabu ni kwamba kama hilo linaeleweka iweje hawa watu hawachukuliwi hatua wakati tunapolalamikia ofisi za Serikali za mitaa?? Au hili jambo haliwahusu wao??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom