Kuhamishiwa wizara nyingine nayo ni hatua nzuri tu! si unajua kule aliko hakuna commission kama nishati na madini!
Ndugu wa JF ningependa kupata taarifa kama kuna hatua yeyote aliyochukuliwa Bw. Adam Malima kwani nikinukuu kupitia kipindi cha Tuongee Asubuhi kilichorushwa na STAR TV mwezi uliopita SMG hairuhusiwi kumilikiwa na raia na hairuhusiwi kuuzwa katika maduka ya Siraha mtu anayeruhusiwa kumiliki uraiani na Kanal wa jeshi mstaafu tu.
Ningependa kupata taarifa kutoka jeshi la police kwa wanaojua sheria hizo kwa ufafanuzi kama sio vinginevyo jeshi la police litakuwa halijatenda haki kwa watanzania kwa kumuachia Mtuumiwa bwana Adam Malima kwa kumiliki Siraha kinyume cha sheria za Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Nawasilisha!
Wanasema ni upepo tu na umepitaNdugu yangu mwanaJFUmeleta jambo la muhimu kwenye jukwaa hili.Tuwaombe kwa moyo wa dhati wanaJF tulipigie kelele hili jambo maana hatujajua kama polisi wamemaliza upelelezi wao, maana RPC Morogoro amehamishwa kwa mujibu wa taarifa ya magazeti ya jana.Naomba tusaidiane sana kwa hili jamani huyu jamaa hatujui kama alikuwa anafadhili makundi ya uhalifu au ameinunua kwenye makundi ya uhalifu au kapewa kutoka wapi.