Toka avuliwe uanachama ndani ya CHADEMA diwani wa mahakama kata ya Igoma Adam Chagulani amekuwa akiweweseka kisiasa hadi kupelekea kutumika na chama cha magamba (ccm) Kana kwamba haitoshi amekuwa akifanya jitihada za kuwasahawishi vijana wa CDM kujiunga na chama kilichopata usajili hivi karibuni (Chauma).
Kimsingi sina tatizo na yeye kushawishi vijana kumuunga mkono kwani ni haki yake ila tatizo ni kuwa awe anaongea na kukubaliana na wahusika kwanza kabla ya kuwapa vyeo pasipo wao kujua na kuwaweka katika mtandao.
Huyu bwana mdogo inabidi atambue kuwa tulimuunga mkono kwa sababu ya chama chake.
=============
Majibu ya Adam:
Kimsingi sina tatizo na yeye kushawishi vijana kumuunga mkono kwani ni haki yake ila tatizo ni kuwa awe anaongea na kukubaliana na wahusika kwanza kabla ya kuwapa vyeo pasipo wao kujua na kuwaweka katika mtandao.
Huyu bwana mdogo inabidi atambue kuwa tulimuunga mkono kwa sababu ya chama chake.
=============
Majibu ya Adam:
Kuna wazushi wa kupika majungu na kuaminisha watu uongo mtamu na kauli vifuniko bila kuzingatia uhalisia wa mambo na ulivyo wake.
Nzagabulu ameeandika uzushi kuwa wana Igoma walichagua Chadema kama hivyo ndivyo anijibu swali langu kama walichagua chama kwanini kwenye kata zingine hawakuchagua wagombea wa Chadema. Wewe kama unataka kugombea Udiwani jiaandae wanaigoma watakuelewa kama wewe ni mkweli unawakilisha maslahi ya jamii watakuchagua tu, waatu wanataka maendeleo siyo siasa za kwenye mitandao zisizojenga, njoo Igoma uwambie wana Igoma humu hakuna wapiga kura wa Igoma wala hawatakusaidia lolote lile.
Usilolijua uliza umeongea umeongea uzushi kuwa nimeuza mlima ni vyema ungesema mlima upi? Na nimemuuzia nani? Na bei gani ,cds ya kuuza kituo cha polisi imechija sasa mmekuja na uzushi mwingine hilo nalo litapita hizo ni kauli vifuniko na ukweli bandia, kupigia kampeni NCCR Mageuzi hilo ni kweli ni haki yangu kufanya hivyo kueneza habari,sijui dhambi iko wapi sasa.
Kumbuka kuwa ukandamizaji unaweza kuondoa ari ya kukitetea ,kukijenga au kukilinda chama sababu watu wanajikuta hawana sababu ya kutetea mifumo inayowakandamiza,kuwadidimiza au kuwadhalilisha.
Chama kinachojitakia mema hakina budi kuwa chama cha wapenda haki. Chama kilicho tayari kila mahali bila kujali nani wa kumteta na nani wakuto mtetea, wakati wakati wanadamu wanakuwazia kushindwa Mungu anakuwazia kushinda. Wanapowaza kuanguka kwako Mungu anawaza kukuinua, wanaposhangilia kuwa wamekumaliza Mungu analeta msaada maishani mwako, wanapopanga uaibike Mungu anaondoa aibu yako.
Kujiunga na chama chochote kile ni haki yangu ya kuzaliwa na kikatiba Siku nikiamua kujuinga na chama chochote hakuna wa kunuzuia, kama nimekwisha kisiasa kwanini unaweweseka kiasi hicho Mungu ndiye mpaji siyo wewe na waliokutuma kutumia IDs fake jitokeze hadharani useme usijifiche kwenye giza najua wewe mwenye unatambua uwezo wangu.
Uzushi wenu wanaigoma hawauhitaji wanataka kazi ninyi endeleeni na siasa za maji taka mtanikuta field nafanya kazi wanaigoma wanajua thamani na uwezo wangu Mungu yuko na mimi