Kaizer
Platinum Member
- Sep 16, 2008
- 25,320
- 17,822
Adai fidia ya Sh700,000 kwa kunyimwa unyumba
Glory Kimath
MAHAKAMA ya mwanzo Temeke imeanza kusikiliza kesi ya madai iliyofunguliwa na Juma Ally, ambaye anadai fidia ya Sh700,000 kutokana na mkewe, Fatuma Seleman kumnyima unyumba. Wanandoa hao wamefikishana mahakamani hapo baada ya mke kuchukuliwa na wazazi wake miaka mitatu baada ya kufunga ndoa yao.
Kesi hiyo, inayosikilizwa na hakimu Silvesta Nyanda, ilikuwa kivutio kwa watu wengi ambao juzi walifika kuisikiliza. Wawili hao walianza maisha ya ndoa Januari 28,2006 lakini ndoa yao ikafikia kikomo Machi 30, 2008 wakati Fatuma alipochukuliwa na wazazi wake, mahakama iliambiwa jana.
Mdai kwenye kesi hiyo ya aina yake, Juma aliieleza mahakama hiyo kuwa ameamua kufungua kesi ya madai ya kiasi hicho cha fedha kama fidia ya usumbufu ya kutopata haki yake ya unyumba kwa kipindi cha miaka mitatu. Alisema fidia hiyo pia inajumuisha gharama za mavazi na matunzo mbalimbali aliyokuwa anampa mkewe kwa kipindi hicho chote kabla na baada ya kuchukuliwa na wazazi wake.
Tangu nimwoe hajawahi kunipa haki yangu ya tendo la ndoa kwa kipindi chote tulichokuwa kama mke na mume na nimemhudumia kwa mambo mengi kwa hiyo nina haki ya kudai fidia kwa sababu sijawahi kumtumia," alisema. Mkewe alikuwepo mahakamani hapo na akakataa kumnyima unyumba mumewe kwa maelezo kuwa aliyeshindwa kutumia haki yake ni Juma mwenyewe.
Mimi nilikuwa mke wake kwa kipindi chote hicho," alikiri Fatuma. "Niliishi naye kwa uvumilivu tu kwani huyu kijana ana upungufu wa nguvu za kiume... yaani hajiwezi kabisa. Huo ndio ukweli mheshimiwa.
"Nilipochoka kuvumilia wazazi wangu walikuja kunichukua. Maelezo hayo yaliibuka mjadala mpya baada ya mume huyo kuyapinga, akisema kuwa ni ya uongo kwa kuwa ameshawahi kuwa na mke na amezaa naye. "Ni kweli kwamba hauna nguvu za kiume," Hakimu Nyanda alimuuliza Juma.
Sio kweli mheshimiwa huyu msichana ananisingizia. Mimi nilishakuwa na mke na tulipata mtoto mmoja wa kike, lakini kwa sasa siko nayee tena, alijibu.
Alieleza mahakamani hapo kuwa awali alifungua madai ya mahari yake ya Sh50,000 lakini hadi sasa hajalipwa, kitu ambacho aliieleza mahakama kuwa kimechangia kuongezeka kwa kiwango cha madai hayo. Kesi hiyo iliahirishwa hadi Desemba mosi, siku ambao mdai atatakiwa kuwasilisha uthibitisho kuwa ana nguvu za kiume.
Source: Mwananchi Read News
My Take:
wadau kumbe haya mambo yanaweza kuwa mazito kiasi hiki! walio na ujuzi wa sheria ya ndoa ya mwaka 1971 watualeze isije ikawa wengi wanakufa na tai zao shingoni kumbe haya mambo yanatatulika mahakamani
Sijui jamaa akienda hospitali vipimo gani watachukua kuthibitisha uwezo wake wa nguvu za kiume? LOL
Glory Kimath
MAHAKAMA ya mwanzo Temeke imeanza kusikiliza kesi ya madai iliyofunguliwa na Juma Ally, ambaye anadai fidia ya Sh700,000 kutokana na mkewe, Fatuma Seleman kumnyima unyumba. Wanandoa hao wamefikishana mahakamani hapo baada ya mke kuchukuliwa na wazazi wake miaka mitatu baada ya kufunga ndoa yao.
Kesi hiyo, inayosikilizwa na hakimu Silvesta Nyanda, ilikuwa kivutio kwa watu wengi ambao juzi walifika kuisikiliza. Wawili hao walianza maisha ya ndoa Januari 28,2006 lakini ndoa yao ikafikia kikomo Machi 30, 2008 wakati Fatuma alipochukuliwa na wazazi wake, mahakama iliambiwa jana.
Mdai kwenye kesi hiyo ya aina yake, Juma aliieleza mahakama hiyo kuwa ameamua kufungua kesi ya madai ya kiasi hicho cha fedha kama fidia ya usumbufu ya kutopata haki yake ya unyumba kwa kipindi cha miaka mitatu. Alisema fidia hiyo pia inajumuisha gharama za mavazi na matunzo mbalimbali aliyokuwa anampa mkewe kwa kipindi hicho chote kabla na baada ya kuchukuliwa na wazazi wake.
Tangu nimwoe hajawahi kunipa haki yangu ya tendo la ndoa kwa kipindi chote tulichokuwa kama mke na mume na nimemhudumia kwa mambo mengi kwa hiyo nina haki ya kudai fidia kwa sababu sijawahi kumtumia," alisema. Mkewe alikuwepo mahakamani hapo na akakataa kumnyima unyumba mumewe kwa maelezo kuwa aliyeshindwa kutumia haki yake ni Juma mwenyewe.
Mimi nilikuwa mke wake kwa kipindi chote hicho," alikiri Fatuma. "Niliishi naye kwa uvumilivu tu kwani huyu kijana ana upungufu wa nguvu za kiume... yaani hajiwezi kabisa. Huo ndio ukweli mheshimiwa.
"Nilipochoka kuvumilia wazazi wangu walikuja kunichukua. Maelezo hayo yaliibuka mjadala mpya baada ya mume huyo kuyapinga, akisema kuwa ni ya uongo kwa kuwa ameshawahi kuwa na mke na amezaa naye. "Ni kweli kwamba hauna nguvu za kiume," Hakimu Nyanda alimuuliza Juma.
Sio kweli mheshimiwa huyu msichana ananisingizia. Mimi nilishakuwa na mke na tulipata mtoto mmoja wa kike, lakini kwa sasa siko nayee tena, alijibu.
Alieleza mahakamani hapo kuwa awali alifungua madai ya mahari yake ya Sh50,000 lakini hadi sasa hajalipwa, kitu ambacho aliieleza mahakama kuwa kimechangia kuongezeka kwa kiwango cha madai hayo. Kesi hiyo iliahirishwa hadi Desemba mosi, siku ambao mdai atatakiwa kuwasilisha uthibitisho kuwa ana nguvu za kiume.
Source: Mwananchi Read News
My Take:
wadau kumbe haya mambo yanaweza kuwa mazito kiasi hiki! walio na ujuzi wa sheria ya ndoa ya mwaka 1971 watualeze isije ikawa wengi wanakufa na tai zao shingoni kumbe haya mambo yanatatulika mahakamani
Sijui jamaa akienda hospitali vipimo gani watachukua kuthibitisha uwezo wake wa nguvu za kiume? LOL