Uchaguzi 2020 Adadi Rajabu na Andrew Chenge, wasomi wabobezi waliokatwa na kuinamisha vichwa. Usomi ni ukondoo?

Sexless

JF-Expert Member
Mar 11, 2017
21,567
50,393
Adadi Rajabu na Andrew Chenge ni watu wasomi wa kupigiwa mfano na walishika nafasi nyeti sana nchi hii. Kiu yao ya kuendelea kuitumikia nchi hii imekatizwa na kikundi kidogo tu cha watu tena na darasa la saba au wenye vyeti vya kuungaunga. Inauma sana.

Hivi kweli hawa wenye vyeti vinavyotiliwa mashaka wanafika mahali wanawanyanyasa wasomi wenye vyeti vya kupigiwa mfano? Kama taifa tunadhani hili ni sawa?

Kama wasomi hawa wamekatwa na kuufyata nani basi atakuja kuupinga uonevu huu? Kwanini wasomi katika taifa hili wanakuwa na ukondoo badala ya kutumia elimu yao kuinua vichwa na kudai haki?
 
Inashangaza sana jinsi hawa watu wanavyomuogopa huyo yesu fake. Yaani maamuzi ya kustaajabisha kuhusu wagombea lakini wanahofia kumchana live. Oops! nilisahau kuna TEUZI hivyo ni lazima WAUFYATE na baadaye wasifie juhudi ili waweze KUTEULIWA. Njaa mbaya sana!!!
 
Mkuu Naomba Niliangalie Kwa Jicho Hili;

< Mzee Wetu Andrew Chenge.:Amehudumu Kwa Muda Mrefu Na Kujizolea Sifa Kedekede Kisheria.Amekaa Bungeni Kwa Miongo 3 Sasa.....Kwa Kipindi chote hicho nadhani Inatosha APUMZIKE Kwani Tumeona Mzee Wassira,pamoja na kuwepo katika BARAZA LA MAWAZIRI LA BABA WA TAIFA,mwaka huu bado alijitokeza KUOMBA NIA NA KURA KUTOTOSHA.

< Dr.Adadi Rajab,Amehudumu Kama mwanasheria wa Polisi then DCI halafu kuwa BALOZI na Mbunge,huyu hajakaa Siasani kwa muda mrefu Kama Alivyokaa Mzee Chenge ila ninadhani CCM wametaka AMSHAAMSHA Jimboni Muheza Kwani Mkoa Wa Tanga Kwa Muda Mrefu Ni Ngome Ya CCM ila Hali inaanza kubadilika kidogokidogo kwa kule kuonekana KIZAZI KIPYA kinaanza kuvutika na CHADEMA NA ACT WAZALENDO.

Na Dr Adadi Ni mwanasiasa Mpole,Mtulivu na Smart Ila Hana KIPAWA CHA PURUKUSHANI MAJUKWAANI.CCM imetaka DAMU YENYE KUCHANGAMKA Kupambana na wapinzani Moto.

All and All HAKUNA wa kubishia INTELLECTUAL potentials na credentials walizonazo mh.Chenge na mh.Dr.Adadi.Ninawaona kuFIT Sana kwenye nafasi za kutuwakilisha KIDIPLOMASIA na hata kuwa THINK TANKERS wafundishe vyuo Vikuu,kitu wasichopenda wanasiasa wengi wastaafu wenye ELIMU zao.
 
Inashangaza sana jinsi hawa watu wanavyomuogopa huyo yesu fake. Yaani maamuzi ya kustaajabisha kuhusu wagombea lakini wanahofia kumchana live. Oops! nilisahau kuna TEUZI hivyo ni lazima WAUFYATE na baadaye wasifie juhudi ili waweze KUTEULIWA. Njaa mbaya sana!!!
Hivi wagombea wa CCM wanawahusu nini? Si ndo vizuri walivyokatwa ili mtumie mwanya huo mkashinde kwenye majimbo yao.
 
Inashangaza sana jinsi hawa watu wanavyomuogopa huyo yesu fake. Yaani maamuzi ya kustaajabisha kuhusu wagombea lakini wanahofia kumchana live. Oops! nilisahau kuna TEUZI hivyo ni lazima WAUFYATE na baadaye wasifie juhudi ili waweze KUTEULIWA. Njaa mbaya sana!!!
ukiona hivyo wana madudu mengi nafsi zao zimejaa hofu ya kuumbuliwa.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
wangeliweza kujiunga na vyama vingine, wangelishinda kwa kura nyingi, lakini sasa wana makandokanda mengi. Jiwe atawafuata, mfano Chenge atafuatwa na rada etc....
 
Mkuu Naomba Niliangalie Kwa Jicho Hili;

< Mzee Wetu Andrew Chenge.:Amehudumu Kwa Muda Mrefu Na Kujizolea Sifa Kedekede Kisheria.Amekaa Bungeni Kwa Miongo 3 Sasa.....Kwa Kipindi chote hicho nadhani Inatosha APUMZIKE Kwani Tumeona Mzee Wassira,pamoja na kuwepo katika BARAZA LA MAWAZIRI LA BABA WA TAIFA,mwaka huu bado alijitokeza KUOMBA NIA NA KURA KUTOTOSHA.

< Dr.Adadi Rajab,Amehudumu Kama mwanasheria wa Polisi then DCI halafu kuwa BALOZI na Mbunge,huyu hajakaa Siasani kwa muda mrefu Kama Alivyokaa Mzee Chenge ila ninadhani CCM wametaka AMSHAAMSHA Jimboni Muheza Kwani Mkoa Wa Tanga Kwa Muda Mrefu Ni Ngome Ya CCM ila Hali inaanza kubadilika kidogokidogo kwa kule kuonekana KIZAZI KIPYA kinaanza kuvutika na CHADEMA NA ACT WAZALENDO.

Na Dr Adadi Ni mwanasiasa Mpole,Mtulivu na Smart Ila Hana KIPAWA CHA PURUKUSHANI MAJUKWAANI.CCM imetaka DAMU YENYE KUCHANGAMKA Kupambana na wapinzani Moto.

All and All HAKUNA wa kubishia INTELLECTUAL potentials na credentials walizonazo mh.Chenge na mh.Dr.Adadi.Ninawaona kuFIT Sana kwenye nafasi za kutuwakilisha KIDIPLOMASIA na hata kuwa THINK TANKERS wafundishe vyuo Vikuu,kitu wasichopenda wanasiasa wengi wastaafu wenye ELIMU zao.
Majibu yenye akili nyingi, ni aibu kuwa na Taifa la wasomi wataka vyeo tu. Uwakilishi wa wananchi sio lazima uwe msomi saana maana hata hao unaowawakisha elimu zao ni za kawaida tu, huitaji PHD kujua kama kijijini kwenu hakuna daraja na watu wanateseka, kujua kama Huduma za afya, usalama, elimu na nyinginezo haziwafikii wananchi wako.
 
huitaji PHD kujua kama kijijini kwenu hakuna daraja na watu wanateseka
Hoja siyo kuiwakilisha. Hoja hapa ni nani amekatiza hamu na nia ya hawa wasomi kuwawakilisha wananchi? Kwann kilaza mwenye phD feki aamue hatma yao?
 
Hoja siyo kuiwakilisha. Hoja hapa ni nani amekatiza hamu na nia ya hawa wasomi kuwawakilisha wananchi? Kwann kilaza mwenye phD feki aamue hatma yao?
Sexless ndio demokrasia hiyo kama Amerika vile, unapitishwa na wajumbe (wananchi) then kamati kuu (electoral votes) inakuchinjilia baharini.

Chenge sio wakwanza na hatakuwa wa mwisho.
 
Inashangaza sana jinsi hawa watu wanavyomuogopa huyo yesu fake. Yaani maamuzi ya kustaajabisha kuhusu wagombea lakini wanahofia kumchana live. Oops! nilisahau kuna TEUZI hivyo ni lazima WAUFYATE na baadaye wasifie juhudi ili waweze KUTEULIWA. Njaa mbaya sana!!!
Hivi NABII LUGOLA anasemaje kuhusu hili?
 
Hawa wasomi walifanya nini kuruhusu wagombea binafsi?

Rajabu alikuwa DCI na balozi. Amekuwa mbunge. Chenge amekuwa AG na waziri. Amekuwa mbunge.

Wamefanya nini kuhakikisha wagombea binafsi wanaruhusiwa?

Wagombea binafsi wangekuwa wanaruhusiwa, wagombea hawa wangeweza kusimama wakagombea kama wagombea binafsi.
 
Hoja siyo kuiwakilisha. Hoja hapa ni nani amekatiza hamu na nia ya hawa wasomi kuwawakilisha wananchi? Kwann kilaza mwenye phD feki aamue hatma yao?
Kwa kuwa kwenye "saccos" yenye wasomi kama Prof Safari na Yule aliye enda SAU
Wanaongozwa na DJ aka Darasa la Saba Is Zamani
 
Hivi niny huwa na elimu gan mpaka kumwita mtu na phd feki.... Si amesoma chuo kinachotambulika udsm kwa ushirikiano na chuo cha nje... Si kafanya research na research report yake ilikubalka.... Before phd si ana first degree na masters....
Ngoja wapumzike na vijana wapate nafasi.. mfano FA ni msomi pia ana masters ya uchumi ngoja akalitumikie taifa.
Ww unanini pumbavu muwe mnaachaga dharau nyangau
Hoja siyo kuiwakilisha. Hoja hapa ni nani amekatiza hamu na nia ya hawa wasomi kuwawakilisha wananchi? Kwann kilaza mwenye phD feki aamue hatma yao?
 
Mlivyo wapuuzi, wangerudi mngesema ati CCM hakuna jipya na shobo nyingi, wamekatwa maneno pia! Hamfai kwa lolote
 
Hoja siyo kuiwakilisha. Hoja hapa ni nani amekatiza hamu na nia ya hawa wasomi kuwawakilisha wananchi? Kwann kilaza mwenye phD feki aamue hatma yao?
Kwa hiyo wewe ulitaka miaka yote waongoze wao tu?Kwani hakuna watu wengine wanaoweza kuongoza?Katika miaka hiyo yote waliyoongoza walifanya kitu gani cha maana?Kwani maisha ni kuwa mbunge tu?wakazitumie elimu zao mtaani kuonesha utofauti na watu wasio na elimu.
 
Adadi Rajabu na Andrew Chenge ni watu wasomi wa kupigiwa mfano na walishika nafasi nyeti sana nchi hii. Kiu yao ya kuendelea kuitumikia nchi hii imekatizwa na kikundi kidogo tu cha watu tena na darasa la saba au wenye vyeti vya kuungaunga. Inauma sana.

Hivi kweli hawa wenye vyeti vinavyotiliwa mashaka wanafika mahali wanawanyanyasa wasomi wenye vyeti vya kupigiwa mfano? Kama taifa tunadhani hili ni sawa?

Kama wasomi hawa wamekatwa na kuufyata nani basi atakuja kuupinga uonevu huu?

Kwanini wasomi katika taifa hili wanakuwa na ukondoo badala ya kutumia elimu yao kuinua vichwa na kudai haki?
[/QUOTE
yetu macho lkn wakianza kuumana wenyewe inakuwa nzuri sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom