Ada ya SIDO ni kubwa sana kwa hali hii ni ngumu kusaidia Mwananchi wa kawaida

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
18,587
22,189
Serikali iliamua kuanzisha shirika la kuendeleza viwanda vidogo (SIDO) kwa lengo la kuwasaidia wananchi wajikwamue kiuchumi kwa kuzalisha bidhaa zao ndogondogo za matumizi ya kilasiku.

Kutokana na mpango huo wa Serikali, SIDO inatakiwa iwe mbele kuhakikisha inaisaidia Serikali katika kuwaelimisha Wananchi ujuzi wa kutengeneza bidhaa za viwanda vidogovidogo, lakini mambo ni tofauti kabisa! SIDO badala yake inawakomoa Wananchi wanaotafuta ujuzi wa kutengeneza bidhaa za mitaani mfano sabuni, mifuko ya karatasi ambavyo kwa sasa ni muhimu sana kimazingira.

Uasi wa SIDO dhidi ya serikali unaanzia pale inapoandaa kozi ya siku tano kutengeneza sabuni kwa shilingi lakini moja na nusu (150,000/=)! Ni kiwango cha ada cha juu sana kuliko ada inayotozwa kwenye vyuo vikuu vyetu! Kama SIDO inania ya dhati ya kuipeleka Tanzania kwenye viwanda haina budi kupunguza tozo hizo za ada zilingane na uwezo wa wananchi;

Pia ni jukumu la serikali kuingilia kati na kuiweka SIDO mikononi mwake kama nguzo ya kulipeleka taifa kwenye uchumi wa viwanda na kulirudisha taifa kwenye umaarufu wa SIDO ya miaka ya sabini.

Ninawasilisha.
 
Ndugu yangu ukitegemea mwanasiasa au mtu akusaidie utakufa hujafanya chochote, fanya juhudi binafsi mkuu
 
Ndugu yangu ukitegemea mwanasiasa au mtu akusaidie utakufa hujafanya chochote, fanya juhudi binafsi mkuu
Hii nimeandika kwa niaba ya maelfu ya wananchi wanaohitaji ujuzi lakini wanakwamishwa na vyombo vya serikali tulivyovianzisha na kuviendesha kwa kodi zetu, SIDO si ya mtu binafsi sasa unaposema tusiitegemee tupambane na hali zetu sikuelewi, anyway this is JF of GT.
 
Hahaha wanaotoza hizo ada ni wanaokwenda kutoa hayo mafunzo. SIDO hawatoi hayo mafunzo wanaajiri wataalamu kuja kuyatoa kwa ujira.
Mkurugenzi wake anakula raha tu. Wewe ujifunze kutengeneza sabuni hizi za kupika, wenye viwanda wanaagiza nje, kwanini ujifunze sasa ikiwa soko liko saturated na bidhaa cheap kutoka nje?!
 
Hahaha wanaotoza hizo ada ni wanaokwenda kutoa hayo mafunzo. SIDO hawatoi hayo mafunzo wanaajiri wataalamu kuja kuyatoa kwa ujira.
Mkurugenzi wake anakula raha tu. Wewe ujifunze kutengeneza sabuni hizi za kupika, wenye viwanda wanaagiza nje, kwanini ujifunze sasa ikiwa soko liko saturated na bidhaa cheap kutoka nje?!
Sabuni ni mfano tu, ada zao zimejikita kiasi hicho, jambo juu kwenye mada hii ni SIDO kuisaidia serikali kwenye uchumi wa viwanda kwa kuwafunza wananchi ili waanzishe viwanda vidogvidogo kama ilivyo India na China ambako ni vingi kuliko vikubwa.
Tusitegemee uchumi wa viwanda vikubwa kabla ya utitiri wa viwanda vidogo ambavyo vimebadili maisha ya wachina kwa muda mfupi sana, kumbuka walipokuja hapa miaka ya sabuni tulikuwa tunawacheka kwa kuvaa nguo mpya zenye viraka!
Kichocheo cha kuwafikia ni SIDO iliyoanzishwa kwa madhumuni hayo kuisaidia serikali kufikia malengo yake vinginevyo nayo itakuwa kama TCRA mbele yetu.
 
Sabuni ni mfano tu, ada zao zimejikita kiasi hicho, jambo juu kwenye mada hii ni SIDO kuisaidia serikali kwenye uchumi wa viwanda kwa kuwafunza wananchi ili waanzishe viwanda vidogvidogo kama ilivyo India na China ambako ni vingi kuliko vikubwa.
Tusitegemee uchumi wa viwanda vikubwa kabla ya utitiri wa viwanda vidogo ambavyo vimebadili maisha ya wachina kwa muda mfupi sana, kumbuka walipokuja hapa miaka ya sabuni tulikuwa tunawacheka kwa kuvaa nguo mpya zenye viraka!
Kichocheo cha kuwafikia ni SIDO iliyoanzishwa kwa madhumuni hayo kuisaidia serikali kufikia malengo yake vinginevyo nayo itakuwa kama TCRA mbele yetu.
Labda SIDO yetu haina maono, binafsi sijawahi kuona SIDO imesaidia yeyote kwa program zake hata kusingekua na hizo ada.
VETA nimeona mchango wake kwa watanzania kujikwamua kimaisha kwa kufanya kazi kutokana na ujuzi walioupata VETA.
 
Labda SIDO yetu haina maono, binafsi sijawahi kuona SIDO imesaidia yeyote kwa program zake hata kusingekua na hizo ada.
VETA nimeona mchango wake kwa watanzania kujikwamua kimaisha kwa kufanya kazi kutokana na ujuzi walioupata VETA.
Kwa hali hii SIDO haina sababu kuendelea kuwepo ifutwe, lakini pia serikali haijui kuwa SIDO ndiyo kichocheo kuiwezesha nchi kuingia kwenye uchumi wa viwanda labda tu kama serikali inataka viwanda vya wawekezaji pekee.
 
Kwa hali hii SIDO haina sababu kuendelea kuwepo ifutwe, lakini pia serikali haijui kuwa SIDO ndiyo kichocheo kuiwezesha nchi kuingia kwenye uchumi wa viwanda labda tu kama serikali inataka viwanda vya wawekezaji pekee.
Hata SIDO haiwezi kutusaidia kuleta viwanda. Hawana program yoyote ya kusaidia kiwanda, hayo mafunzo ya ujasiliamali wanayotoa hayawezi kuleta kiwanda. Labda VETA ningewwza kukubali inaweza leta mafundi wa vipuri na mitambo.
SIDO ifutwe tu.
 
Serikali iliamua kuanzisha shirika la kuendeleza viwanda vidogo (SIDO) kwa lengo la kuwasaidia wananchi wajikwamue kiuchumi kwa kuzalisha bidhaa zao ndogondogo za matumizi ya kilasiku.

Kutokana na mpango huo wa Serikali, SIDO inatakiwa iwe mbele kuhakikisha inaisaidia Serikali katika kuwaelimisha Wananchi ujuzi wa kutengeneza bidhaa za viwanda vidogovidogo, lakini mambo ni tofauti kabisa! SIDO badala yake inawakomoa Wananchi wanaotafuta ujuzi wa kutengeneza bidhaa za mitaani mfano sabuni, mifuko ya karatasi ambavyo kwa sasa ni muhimu sana kimazingira.

Uasi wa SIDO dhidi ya serikali unaanzia pale inapoandaa kozi ya siku tano kutengeneza sabuni kwa shilingi lakini moja na nusu (150,000/=)! Ni kiwango cha ada cha juu sana kuliko ada inayotozwa kwenye vyuo vikuu vyetu! Kama SIDO inania ya dhati ya kuipeleka Tanzania kwenye viwanda haina budi kupunguza tozo hizo za ada zilingane na uwezo wa wananchi;

Pia ni jukumu la serikali kuingilia kati na kuiweka SIDO mikononi mwake kama nguzo ya kulipeleka taifa kwenye uchumi wa viwanda na kulirudisha taifa kwenye umaarufu wa SIDO ya miaka ya sabini.

Ninawasilisha.
SIDO Arusha wanatoa mafunzo ya sabuni kwa 70,000 . Mkuu naomba unielekeze ofisi za SIDO dar es salaam.
 
Back
Top Bottom