Wakuu nilikuwa nasoma maelekezo yaliyotolewa kuhusu Ujio wa Intake mpya, mojawapo kilichonishangaza ni kuona viwango vipya vya Ada, wakati naomba kusoma UDBS ilikuwa tsh 1,300,000/= kwa mwaka, ila leo ni tsh 1,500,000/= ukijumlisha na gharama zingine zinafika Mil. Mbili kasoro kidogo. Ni pamoja na kozi zingine viwango ni tofauti tofauti. Je huu ni Uungwana kwa Elimu ya Mtanzania tena mlala njaa na mtembea peku (bila viatu)?