BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
CHAMA cha ACT-Wazalendo kimesema hakitashiriki uchaguzi mdogo wa Jimbo la Konde hadi watumishi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), waliohusika katika uchaguzi uliopita watakapowajibishwa.
Akisoma maazimio ya chama katika eneo la Konde Pemba wakati wa ziara maalum ya viongozi wa ACT-Wazalendo, Kiongozi Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe alisema chama hicho hakitashiriki uchaguzi huo hadi watumishi wa ZEC wawajibishwe.
Zitto alisema kuwa wananchi ambao waliumizwa na kuteswa kwenye uchaguzi walipwe fidia, ili wapate haki yao.
Alisema azimio lingine ni pamoja wa kuundwa kwa kamati ya kisheria ya kuratibu maridhiano ya kijamiii, ili ZEC ionyeshe mwelekeo nini kifanyike yazidi kukua.
Aidha, azimio la tatu ni kuitaka Serikali ya Zanzibar na ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuzifanyia marekebisho sheria zote za uchaguzi kabla ya mwaka 2025, ili uchaguzi mkuu ujao uwe sawa katika kushindania nafasi za uongozi.
Alisema halitakuwa jambo la busara kila baada ya uchaguzi kuirudisha Zanzibar nyuma kimaendeleo, ni vyema umoja na maridhiano ya kisiasa kudumu muda wote.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho ambaye ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Othman Masoud Othman, alisema kilichomfanya mbunge mteule wa Konde kutoka CCM kuachia ngazi ni mazungumzo.
Alisema vilelezo na ushahidi waliowasilisha ni matunda na matokeo chanya yaliyopatikana ya kujiuzulu kwa mbuge mteule wa jimbo hilo.
Makamu Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, Juma Duni Haji, alisema hawako tayari kuingia kwenye uchaguzi wakati walioharibu uchaguzi huo hawajachukuliwa hatua zozote.
Chanzo: Nipashe
Akisoma maazimio ya chama katika eneo la Konde Pemba wakati wa ziara maalum ya viongozi wa ACT-Wazalendo, Kiongozi Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe alisema chama hicho hakitashiriki uchaguzi huo hadi watumishi wa ZEC wawajibishwe.
Zitto alisema kuwa wananchi ambao waliumizwa na kuteswa kwenye uchaguzi walipwe fidia, ili wapate haki yao.
Alisema azimio lingine ni pamoja wa kuundwa kwa kamati ya kisheria ya kuratibu maridhiano ya kijamiii, ili ZEC ionyeshe mwelekeo nini kifanyike yazidi kukua.
Aidha, azimio la tatu ni kuitaka Serikali ya Zanzibar na ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuzifanyia marekebisho sheria zote za uchaguzi kabla ya mwaka 2025, ili uchaguzi mkuu ujao uwe sawa katika kushindania nafasi za uongozi.
Alisema halitakuwa jambo la busara kila baada ya uchaguzi kuirudisha Zanzibar nyuma kimaendeleo, ni vyema umoja na maridhiano ya kisiasa kudumu muda wote.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho ambaye ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Othman Masoud Othman, alisema kilichomfanya mbunge mteule wa Konde kutoka CCM kuachia ngazi ni mazungumzo.
Alisema vilelezo na ushahidi waliowasilisha ni matunda na matokeo chanya yaliyopatikana ya kujiuzulu kwa mbuge mteule wa jimbo hilo.
Makamu Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, Juma Duni Haji, alisema hawako tayari kuingia kwenye uchaguzi wakati walioharibu uchaguzi huo hawajachukuliwa hatua zozote.
Chanzo: Nipashe