ACT Wazalendo wasema hawatashiriki uchaguzi mdogo ujao,NEC haijazungumzia kasoro za uchaguzi uliopita

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287
DAR: Chama cha ACT Wazalendo kimesema hakitashiriki uchaguzi mdogo wa Wabunge na Madiwani uliopangwa kufanyika tarehe 17 Februari kutokana kuwepo kwa kasoro nyingi uchaguzi uliopita na Tume ya Uchaguzi kutozunguzumzia kasoro hizo

Wakiongea na waandishi wa habari leo, Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo bara, ndugu Msafiri Mtemelwa na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano ya Umma, ndugu Ado Shaibu wamesema Tume ya Uchaguzi ilikutana na wadau na kuzungumza nao na kukiri baadhi ya kasoro kwenye uchaguzi mdogo uliopita na kuwakemea Wakuu wa Wilaya na Mikoa kutoshiriki katika kampeni za uchaguzi

Ila tume hiyo haijakemea kasoro nyingine zilizojitokeza kama matumizi ya vyombo vya dola ambavyo vimekuwa viliwatisha wananchi na kuwapiga wakati wa uchaguzi

Naibu Katibu huyo amesema alishuhudia kwenye uchaguzi uliofanyika kata ya Muungano huko Urambo Tabora polisi wa FFU wakiwa wengi kupita kiasi kitu ambacho anasema kinawaogopesha watu kutoshiriki

Amezungumzia pia Chama tawala (CCM) kiliwatumia Wakurugenzi wa Halmashauri walioteuliwa na Rais kwa kuzingatia Ukada ili kushinda uchaguzi

Ameendelea kusema baada ya mbinu zote kushindwa chama tawala kilijitangazia ushindi na tume kutojali kabisa malalamiko
 
Nadhani ACT wamefanya sawa kabisa, wasimamie hapo hapo ngoja cdm washiriki kisha wafanyiwe fujo ili ACT waendelee kuweka mbinyo kwamba kuna tatizo kwenye zoezi zima la uchaguzi. Uchaguzi huu naona kabisa ukimuweka wazi rais pamoja na chama kwamba wanaongoza nchi kwa mabavu na sio ridhaa ya wananchi. Act wazalendo shikilieni hapo hapo ngoja cdm washiriki kuleta uthibisho wa madai ya tume ya uchaguzi kuchezea sheria ili kuibeba ccm.
 
Chama cha ACT-Wazalendo kimesema hakitashiriki uchaguzi katika majimbo ya Kinondoni na Siha kwa kuwa sababu zilizowafanya wasusie uchaguzi mdogo uliopita, bado hazijafanyiwa kazi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 21, 2018 Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho-Bara, Msafiri Mtemelwa amesema changamoto walizozilalamikia katika uchaguzi wa Januari 13 katika majimbo ya Singida Kaskazini, Songea Mjini na Longido bado hazijafanyiwa kazi.

Amesema bado chama hicho kitaendelea kushinikiza Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufanya mageuzi katika mchakato wa uchaguzi.

Amesema malalamiko ya chama hicho kwa NEC ni matumizi ya nguvu ya vyombo vya dola dhidi ya vyama vya upinzani kwa lengo la kukisaidia chama tawala CCM.

Uchaguzi wa Siha na Kinondoni unafanyika baada ya waliokuwa wabunge wa majimbo hayo kuhamia CCM Desemba mwaka jana.
Chanzo: MCL
 
ACT wana akili kuliko vyama vyote ndo maana yule jamaa alitumia njia zake kukiua hiki chama
 
Chama cha ACT-Wazalendo kimesema hakitashiriki uchaguzi katika majimbo ya Kinondoni na Siha kwa kuwa sababu zilizowafanya wasusie uchaguzi mdogo uliopita, bado hazijafanyiwa kazi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 21, 2018 Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho-Bara, Msafiri Mtemelwa amesema changamoto walizozilalamikia katika uchaguzi wa Januari 13 katika majimbo ya Singida Kaskazini, Songea Mjini na Longido bado hazijafanyiwa kazi.

Amesema bado chama hicho kitaendelea kushinikiza Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufanya mageuzi katika mchakato wa uchaguzi.

Amesema malalamiko ya chama hicho kwa NEC ni matumizi ya nguvu ya vyombo vya dola dhidi ya vyama vya upinzani kwa lengo la kukisaidia chama tawala CCM.

Uchaguzi wa Siha na Kinondoni unafanyika baada ya waliokuwa wabunge wa majimbo hayo kuhamia CCM Desemba mwaka jana.
Chanzo: MCL
We Mzee acha kujipendekeza...nenda Lumumba mkasovu issue zenu

Musiba ni Msiba!
 
Wangewasiliana na chadema, maana inashiriki, inawezekana changamoto walizopigia kelele tume imezifanyia Kazi.

Ni imani yangu kwenye chaguzi hizi mbili ,za Kinondoni na Siha, chadema ikitokea wakashindwa, watakua wameshindwa kihalali na hakutakua na visingizio vyovyote vile, kwani wameingia wakiamini kila kitu tume ya uchaguzi imekifanyia kazi
 
Demokrasia....Ila Chama babalao la demokrasia halitakaa kususia uchaguzi kamwe
 
Wangewasiliana na chadema, maana inashiriki, inawezekana changamoto walizopigia kelele tume imezifanyia Kazi.

Ni imani yangu kwenye chaguzi hizi mbili ,za Kinondoni na Siha, chadema ikitokea wakashindwa, watakua wameshindwa kihalali na hakutakua na visingizio vyovyote vile, kwani wameingia wakiamini kila kitu tume ya uchaguzi imekifanyia kazi
Hawana hela, trust me. Hawana hela na chama kimepukutishwa sana. Wanarudi kujipanga upya. Hata hivyo majimbo ya Dar sio priority yao. Ingekuwa ni moja ya majimbo ya Kigoma Zitto angewakopesha pesa na Magari yake. Mimi nipo ACT kimaslahi ingawa moyoni ni CDM Damu, niamini, ACT Wamefulia
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom