ACT Wazalendo
JF-Expert Member
- May 5, 2014
- 602
- 1,526
Tumepokea Taarifa kuwa Jeshi la Polisi limevamia Ukumbi wa Msimbazi Center, Dar es salaam na kuzuia kikao Cha Kamati Kuu ya Chama cha NCCR Mageuzi kisifanyike kwa kisingizio cha tahadhari ya ugonjwa wa Uviko 19.
Chama kinalaani vikali hatua hii ya Jeshi la Polisi ambayo ni kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheria ya Vyama vya Siasa.
Ni jambo linalosikitisha kuwa wakati Jeshi la Polisi likizuia shughuli halali za Vyama vya Siasa vya Upinzani kwa sababu mbalimbali ikiwemo Uviko 19, Matamasha ya Michezo Nchini yanaendeleaje pomoja na CCM kufanya shughuli zao ikiwemo vikao vya ndani na mikutano ya hadhara bila ya kuzuiwa utadhani wao ni malaika wasioweza kuugua wala kuambikiza Uviko 19.
WITO WETU:
Chama kinalaani vikali hatua hii ya Jeshi la Polisi ambayo ni kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheria ya Vyama vya Siasa.
Ni jambo linalosikitisha kuwa wakati Jeshi la Polisi likizuia shughuli halali za Vyama vya Siasa vya Upinzani kwa sababu mbalimbali ikiwemo Uviko 19, Matamasha ya Michezo Nchini yanaendeleaje pomoja na CCM kufanya shughuli zao ikiwemo vikao vya ndani na mikutano ya hadhara bila ya kuzuiwa utadhani wao ni malaika wasioweza kuugua wala kuambikiza Uviko 19.
WITO WETU:
Jeshi la Polisi lifanye kazi zake kwa weledi, haki na usawa. Jeshi liache kutumika kisiasa kwa kuipendelea CCM na kuvikandamiza.