ACT-Wazalendo na CHADEMA, achananeni na dhana ya ukuu/ukubwa miongoni mwa vyama vya upinzani nchini

Idadi ya wabunge sio uthibitisho wa kukubalika kwa chama ( Marekani kuna majimbo mengi tu ambako Democrats wanapata kura nyingi kuliko Republicans lakini wanapata viti vichache kuliko wenzao).

Hata katika uchaguzi uliopita ulioacha maswali mengi Chadema kilipata kura nyingi kuliko vyama vingine vyote vya upinzani. Wangekubaliana na matokeo ya uchaguzi Chadema ingekuwa na wabunge 20 bungeni. Aidha, ukiangalia nguvu ambazo chama tawala kinatumia kupambana na Chadema ni dhahiri kuwa wanakiona kuwa ni tishio kwao. Ni Chadema peke yake ambao hata uvaaji wa fulana zao unaweza kukusababisha ukae mahabusu. Ni hiki ndicho kinachofanya wengi tukione kuwa ni chama kikuu cha upinzani.
Ushirikiano wa vyama hauwezi kulazimishwa hasa kwa sababu kila chama kina sera zake. Na ushirikiano wa kulazimisha hapo mbeleni unaleta changamoto za kugawana viti na kama watashinda, madaraka.

Kama kweli watanzania watakuwa wameichoka CCM wataamua wenyewe nani awe mrithi wake. Anaweza kuwa Chadema, ACT-WAZALENDO, NCCR-MAGEUZI CUF, hata TLP.
Hizi sifa za kipi ni chama kikuu au chama kiongozi hakitabadilisha msimamo wao.

Mimi nawashangaa wale wanaosema kuwa hamna serious opposition wakati kila kukicha tunaona juhudi zinavyofanywa kuwakosesha pumzi. Kama hamna serious opposition pangekuwa hamna haja ya kuzuia mikutano ya hadhara, makongamano, maandamano, watu kuombewa, uvaaji wa t-shirt, ubebaji wa mabango n.k. Tusingeona utitiri wa watu kuswekwa mahabusu na kufunguliwa kesi ambazo hazina mbele wala nyuma. Tusingeona mitandao inabanwa maana chama tawala wangejua hamna chama ambacho kinaweza kuchukua nafasi yao kwa kuzingatia jinsi kinavyokubalika.

Hauwezi kuwafunga watu mikono na kuwaziba macho yao halafu ukatamba kuwa hauoni wa kukushinda kwenye mbio za steeple chase!

Amandla...
Asante sana
 
26A235F7-590D-45A2-A785-BFDD0EA8F1A4.jpeg

Siku chache zilizopita, niliongelea swala la kuwataka CHADEMA kujiepusha na matumizi ya neno "chama kikuu" cha upinzani nchini kwasababu mbalimbali mojawapo ni katika kuimarisha upinzani nchini na kuondoa inferiority complex miongoni mwa vyama vingine vya upinzani.



Katika dhana hiyo hiyo ya kutafuta ukubwa/ ukuu miongoni mwa vyama vya upinzani nchini, leo hii ACT-Wazalendo wameamua kujiita "chama kiongozi wa upinzani nchini". Hii inadhihirisha kile nilichokisema kuwa maneno haya ya "ukuu" yanaathiri umoja na mshikamano miongoni mwa vyama vya upinzani.

Teyari baadhi ya makamanda wameanza kuhoji uhalali wa ACT kujiita ni chama kiongozi wa upinzani nchini jambo ambalo si jema sana.

Najua si vyama vyote vinavyoitwa vyama vya upinzani ni kweli vyama hivyo ni vya upinzani, bali baaidhi ni vyama mapandikizi kwa lengo la kuvuruga upinzani ila bado ukweli huu hauondoi athari ya vyama vingine kuwa na ukuu dhidi ya vyama vingine.

Wasomeni hapa ACT katika taarifa yao hii ndio mjue huu ukuu sio jambo jema miongoni mwa vyama vya upinzani.

View attachment 1894679
 
Back
Top Bottom