ACT-Wazalendo na CHADEMA, achananeni na dhana ya ukuu/ukubwa miongoni mwa vyama vya upinzani nchini

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,986
144,313
Siku chache zilizopita, niliongelea swala la kuwataka CHADEMA kujiepusha na matumizi ya neno "chama kikuu" cha upinzani nchini kwasababu mbalimbali mojawapo ni katika kuimarisha upinzani nchini na kuondoa inferiority complex miongoni mwa vyama vingine vya upinzani.


Katika dhana hiyo hiyo ya kutafuta ukubwa/ ukuu miongoni mwa vyama vya upinzani nchini, leo hii ACT-Wazalendo wameamua kujiita "chama kiongozi wa upinzani nchini". Hii inadhihirisha kile nilichokisema kuwa maneno haya ya "ukuu" yanaathiri umoja na mshikamano miongoni mwa vyama vya upinzani.

Teyari baadhi ya makamanda wameanza kuhoji uhalali wa ACT kujiita ni chama kiongozi wa upinzani nchini jambo ambalo si jema sana.

Najua si vyama vyote vinavyoitwa vyama vya upinzani ni kweli vyama hivyo ni vya upinzani, bali baaidhi ni vyama mapandikizi kwa lengo la kuvuruga upinzani ila bado ukweli huu hauondoi athari ya vyama vingine kuwa na ukuu dhidi ya vyama vingine.

Wasomeni hapa ACT katika taarifa yao hii ndio mjue huu ukuu sio jambo jema miongoni mwa vyama vya upinzani.

Screenshot_20210816-172916_Twitter.jpg
 
Ni nani aliekwambia kuwa wapinzan wa nchi hii wanashaurika? Na ni nani aliewahi kutoa ushauri wake kwa wapinzan, akaeleweka na ushaure wake kufanyiwa kazi?

Mwaka 2015, tulishauri kuhusu Chadema na Ukawa kwa ujumla kuacha kuingia katika mtego uliotegwa mahususi na CCM, ili kuuangamiza upinzan na kuuwa kabisa matumaini ya wale tuliokuwa tunahitaji mabadiliko ya kweli kupitia Ukawa.

Ushauri wetu ulipuuzwa baada ya wenyeviti kurubuniwa na viela kidogo kutoka kwa fisadi kuu na genge lao na matokeo yake kila mtu aliyaona baada ya uchaguzi. Wao wanachoangalia ni jinsi gani watatumia siasa kama njia ya kujaza matumbo yao na vyoo vyao.
 
Siku chache zilizopita, niliongelea swala la kuwataka CHADEMA kujiepusha na matumizi ya neno "chama kikuu" cha upinzani nchini kwasababu mbalimbali mojawapo ni katika kuimarisha upinzani nchini na kuondoa inferiority complex miongoni mwa vyama vingine vya upinzani.


Katika dhana hiyo hiyo ya kutafuta ukubwa/ ukuu miongoni mwa vyama vya upinzani nchini, leo hii ACT-Wazalendo wameamua kujiita "chama kiongozi wa upinzani nchini". Hii inadhihirisha kile nilichokisema kuwa maneno haya ya "ukuu" yanaathiri umoja na mshikamano miongoni mwa vyama vya upinzani.

Teyari baadhi ya makamanda wameanza kuhoji uhalali wa ACT kujiita ni chama kiongozi wa upinzani nchini jambo ambalo si jema sana.

Najua si vyama vyote vinavyoitwa vyama vya upinzani ni kweli vyama hivyo ni vya upinzani, bali baaidhi ni vyama mapandikizi kwa lengo la kuvuruga upinzani ila bado ukweli huu hauondoi athari ya vyama vingine kuwa na ukuu dhidi ya vyama vingine.

Wasomeni hapa ACT katika taarifa yao hii ndio mjue huu ukuu sio jambo jema miongoni mwa vyama vya upinzani.

View attachment 1894679
Naunga mkono hoja.
Chama kikuu cha Upinzani nchini Tanzania ni ACT Wazalendo, kwasababu kina wabunge Bara na Visiwani, pia kina wawakilishi ndani ya Baraza la Wawakilishi.
Chama Kikuu cha Upinzani, Tanzania Bara ni Chadema. Kina mbunge mmoja bara, hakina mbunge Zanzibar wala mwakilishi.
Chama Kikuu cha Upinzani Zanzibar ni ACT Wazalendo, kina wabunge na wawakilishi.

Ili Upinzani ufanikiwe lazima wapinzani washirikiane.

Baada ya Upinzani kushinda Zambia, najua kuna Watanzania wengi na haswa wapinzani na wapenda mabadiliko, watafurahia matokeo ya Zambia kwa imani na matumaini kuwa hiki kilichotokea Zambia, "if it can happen in Zambia, then one day it can also happen in Tanzania". Hivyo na Tanzania kuna siku Upinzani utashinda, uchaguzi, kutangazwa na kuongoza nchi. Naomba niwaandae kisaikolojia, "Zambia is Zambia na Tanzania ni Tanzania" Kwa Tanzania, sisi bado sana, maana ni kama hatuna any serious opposition ya kuikabidhi ikulu yetu, hivyo CCM itatawala mile...!, naomba nisimalizie- Pasco.

P
 
Naunga mkono hoja.
Chama kikuu cha Upinzani nchini Tanzania ni ACT Wazalendo, kwasababu kina wabunge Bara na Visiwani, pia kina wawakilishi ndani ya Baraza la Wawakilishi.
Chama Kikuu cha Upinzani, Tanzania Bara ni Chadema. Kina mbunge mmoja bara, hakina mbunge Zanzibar wala mwakilishi.
Chama Kikuu cha Upinzani Zanzibar ni ACT Wazalendo, kina wabunge na wawakilishi.

Ili Upinzani ufanikiwe lazima wapinzani washirikiane.

Baada ya Upinzani kushinda Zambia, najua kuna Watanzania wengi na haswa wapinzani na wapenda mabadiliko, watafurahia matokeo ya Zambia kwa imani na matumaini kuwa hiki kilichotokea Zambia, "if it can happen in Zambia, then one day it can also happen in Tanzania". Hivyo na Tanzania kuna siku Upinzani utashinda, uchaguzi, kutangazwa na kuongoza nchi. Naomba niwaandae kisaikolojia, "Zambia is Zambia na Tanzania ni Tanzania" Kwa Tanzania, sisi bado sana, maana ni kama hatuna any serious opposition ya kuikabidhi ikulu yetu, hivyo CCM itatawala mile...!, naomba nisimalizie- Pasco.

P
Idadi ya wabunge sio uthibitisho wa kukubalika kwa chama ( Marekani kuna majimbo mengi tu ambako Democrats wanapata kura nyingi kuliko Republicans lakini wanapata viti vichache kuliko wenzao).

Hata katika uchaguzi uliopita ulioacha maswali mengi Chadema kilipata kura nyingi kuliko vyama vingine vyote vya upinzani. Wangekubaliana na matokeo ya uchaguzi Chadema ingekuwa na wabunge 20 bungeni. Aidha, ukiangalia nguvu ambazo chama tawala kinatumia kupambana na Chadema ni dhahiri kuwa wanakiona kuwa ni tishio kwao. Ni Chadema peke yake ambao hata uvaaji wa fulana zao unaweza kukusababisha ukae mahabusu. Ni hiki ndicho kinachofanya wengi tukione kuwa ni chama kikuu cha upinzani.
Ushirikiano wa vyama hauwezi kulazimishwa hasa kwa sababu kila chama kina sera zake. Na ushirikiano wa kulazimisha hapo mbeleni unaleta changamoto za kugawana viti na kama watashinda, madaraka.

Kama kweli watanzania watakuwa wameichoka CCM wataamua wenyewe nani awe mrithi wake. Anaweza kuwa Chadema, ACT-WAZALENDO, NCCR-MAGEUZI CUF, hata TLP.
Hizi sifa za kipi ni chama kikuu au chama kiongozi hakitabadilisha msimamo wao.

Mimi nawashangaa wale wanaosema kuwa hamna serious opposition wakati kila kukicha tunaona juhudi zinavyofanywa kuwakosesha pumzi. Kama hamna serious opposition pangekuwa hamna haja ya kuzuia mikutano ya hadhara, makongamano, maandamano, watu kuombewa, uvaaji wa t-shirt, ubebaji wa mabango n.k. Tusingeona utitiri wa watu kuswekwa mahabusu na kufunguliwa kesi ambazo hazina mbele wala nyuma. Tusingeona mitandao inabanwa maana chama tawala wangejua hamna chama ambacho kinaweza kuchukua nafasi yao kwa kuzingatia jinsi kinavyokubalika.

Hauwezi kuwafunga watu mikono na kuwaziba macho yao halafu ukatamba kuwa hauoni wa kukushinda kwenye mbio za steeple chase!

Amandla...
 
Naunga mkono hoja.
Chama kikuu cha Upinzani nchini Tanzania ni ACT Wazalendo, kwasababu kina wabunge Bara na Visiwani, pia kina wawakilishi ndani ya Baraza la Wawakilishi.
Chama Kikuu cha Upinzani, Tanzania Bara ni Chadema. Kina mbunge mmoja bara, hakina mbunge Zanzibar wala mwakilishi.
Chama Kikuu cha Upinzani Zanzibar ni ACT Wazalendo, kina wabunge na wawakilishi.

Ili Upinzani ufanikiwe lazima wapinzani washirikiane.

Baada ya Upinzani kushinda Zambia, najua kuna Watanzania wengi na haswa wapinzani na wapenda mabadiliko, watafurahia matokeo ya Zambia kwa imani na matumaini kuwa hiki kilichotokea Zambia, "if it can happen in Zambia, then one day it can also happen in Tanzania". Hivyo na Tanzania kuna siku Upinzani utashinda, uchaguzi, kutangazwa na kuongoza nchi. Naomba niwaandae kisaikolojia, "Zambia is Zambia na Tanzania ni Tanzania" Kwa Tanzania, sisi bado sana, maana ni kama hatuna any serious opposition ya kuikabidhi ikulu yetu, hivyo CCM itatawala mile...!, naomba nisimalizie- Pasco.

P
Acheni wananchi waamue kama kweli hakuna upinzani serious na si kutumia dola kudhibiti upinzani.

Simple like that.
 
Naunga mkono hoja.
Chama kikuu cha Upinzani nchini Tanzania ni ACT Wazalendo, kwasababu kina wabunge Bara na Visiwani, pia kina wawakilishi ndani ya Baraza la Wawakilishi.
Chama Kikuu cha Upinzani, Tanzania Bara ni Chadema. Kina mbunge mmoja bara, hakina mbunge Zanzibar wala mwakilishi.
Chama Kikuu cha Upinzani Zanzibar ni ACT Wazalendo, kina wabunge na wawakilishi.

Ili Upinzani ufanikiwe lazima wapinzani washirikiane.

Baada ya Upinzani kushinda Zambia, najua kuna Watanzania wengi na haswa wapinzani na wapenda mabadiliko, watafurahia matokeo ya Zambia kwa imani na matumaini kuwa hiki kilichotokea Zambia, "if it can happen in Zambia, then one day it can also happen in Tanzania". Hivyo na Tanzania kuna siku Upinzani utashinda, uchaguzi, kutangazwa na kuongoza nchi. Naomba niwaandae kisaikolojia, "Zambia is Zambia na Tanzania ni Tanzania" Kwa Tanzania, sisi bado sana, maana ni kama hatuna any serious opposition ya kuikabidhi ikulu yetu, hivyo CCM itatawala mile...!, naomba nisimalizie- Pasco.

P
P- hivi kule Zambia unakumbukumbu za kuandikwa kwa katiba mpya?
 
Kampeni za 2020 zilituonyesha mapenzi makubwa ya Watanzania nchi nzima kwa umati uliokuwa ukivutiwa kwenye kampeni zao ukilinganisha ná chama cha Ayatollah Zitto. Kabla ya hapo Chadema ilikuwa na viti vingi Bungeni kuliko chama cha ayatollah. Maccm hayakiogopi hata chembe chama cha ayatollah ukilinganisha na wanavyoihofia Chadema. Mitandaoni kote habari ni Chadema hata wanachama na Viongozi wa Chadema wanakamatwa sana, kuteswa na kubambikiwa kesi kuliko wale wa chama cha ayatollah. Hivyo kwa ushahidi huo chama kikuu cha upinzani nchini kitaendelea kuwa Chadema na hakuna sababu yoyote ile ya kuacha kujitambulisha hivyo. Zitto ni MSALITI tu na mchumia tumbo.

Siku chache zilizopita, niliongelea swala la kuwataka CHADEMA kujiepusha na matumizi ya neno "chama kikuu" cha upinzani nchini kwasababu mbalimbali mojawapo ni katika kuimarisha upinzani nchini na kuondoa inferiority complex miongoni mwa vyama vingine vya upinzani.



Katika dhana hiyo hiyo ya kutafuta ukubwa/ ukuu miongoni mwa vyama vya upinzani nchini, leo hii ACT-Wazalendo wameamua kujiita "chama kiongozi wa upinzani nchini". Hii inadhihirisha kile nilichokisema kuwa maneno haya ya "ukuu" yanaathiri umoja na mshikamano miongoni mwa vyama vya upinzani.

Teyari baadhi ya makamanda wameanza kuhoji uhalali wa ACT kujiita ni chama kiongozi wa upinzani nchini jambo ambalo si jema sana.

Najua si vyama vyote vinavyoitwa vyama vya upinzani ni kweli vyama hivyo ni vya upinzani, bali baaidhi ni vyama mapandikizi kwa lengo la kuvuruga upinzani ila bado ukweli huu hauondoi athari ya vyama vingine kuwa na ukuu dhidi ya vyama vingine.

Wasomeni hapa ACT katika taarifa yao hii ndio mjue huu ukuu sio jambo jema miongoni mwa vyama vya upinzani.

View attachment 1894679
 
Hiyo dhana nadhani inasababishwa na nature ya kiongozi wa upande mmoja, kuondoka kwake Chadema alikuwa na nia ya kuhakikisha anaenda kuifuta Chadema kwenye ramani za siasa Tanzania, hata ikibidi kwa msaada toka CCM, hili limeshindikana.

Hii ni kutokana na namna alivyoondoshwa, hakupenda kuondoka, ni kama ana kinyongo, japo kwa kumuangalia usoni anaonesha yuko ok hasa kwa uhusiano wake na viongozi wa Chadema (kumtembelea Lissu Belgium, na Mbowe mahakamani), pamoja na hayo sio mtu wa kumuamini 100%.
 
Hiyo dhana nadhani inasababishwa na nature ya kiongozi wa upande mmoja, kuondoka kwake Chadema alikuwa na nia ya kuhakikisha anaenda kuifuta Chadema kwenye ramani za siasa Tanzania, hata ikibidi kwa msaada toka CCM, hili limeshindikana.

Hii ni kutokana na namna alivyoondoshwa, hakupenda kuondoka, ni kama ana kinyongo, japo kwa kumuangalia usoni anaonesha yuko ok hasa kwa uhusiano wake na viongozi wa Chadema (kumtembelea Lissu Belgium, na Mbowe mahakamani), pamoja na hayo sio mtu wa kumuamini 100%.
Huyo kiongozi wa upande mmoja aliondoka ili kuepuka kukutana na yale yaliyomkuta Chacha Wangwe. Maana mazingira ya case zao yalikuwa yanafanana, wote walihoji au kuutaka uenyekiti wa chama ndio yakawakuta yaliowakuta. RIP Chacha Wangwe... Hakika Mungu anamuadhibu yule aliekatisha uhai wako.
 
Naunga mkono hoja.
Chama kikuu cha Upinzani nchini Tanzania ni ACT Wazalendo, kwasababu kina wabunge Bara na Visiwani, pia kina wawakilishi ndani ya Baraza la Wawakilishi.
Chama Kikuu cha Upinzani, Tanzania Bara ni Chadema. Kina mbunge mmoja bara, hakina mbunge Zanzibar wala mwakilishi.
Chama Kikuu cha Upinzani Zanzibar ni ACT Wazalendo, kina wabunge na wawakilishi.

Ili Upinzani ufanikiwe lazima wapinzani washirikiane.

Baada ya Upinzani kushinda Zambia, najua kuna Watanzania wengi na haswa wapinzani na wapenda mabadiliko, watafurahia matokeo ya Zambia kwa imani na matumaini kuwa hiki kilichotokea Zambia, "if it can happen in Zambia, then one day it can also happen in Tanzania". Hivyo na Tanzania kuna siku Upinzani utashinda, uchaguzi, kutangazwa na kuongoza nchi. Naomba niwaandae kisaikolojia, "Zambia is Zambia na Tanzania ni Tanzania" Kwa Tanzania, sisi bado sana, maana ni kama hatuna any serious opposition ya kuikabidhi ikulu yetu, hivyo CCM itatawala mile...!, naomba nisimalizie- Pasco.

P
Hatuna serous opposition pia hatuna serious chama tawala
Sasa wewe pasco,unaona 75*% ya media huru zinaandika habari za cdm, hata wewe unaandika zaidi nabari za cdm kuliko ccm,
Polisi, mahakama, tiss wako bize na cdm

Shaka, chongolo, Samia, siro, mutungi kila saa wanaiwaxa cdml,

Alafu unasema hatuna serious opposition ?
Myonge myonge haki yake mpenzi
Cdm ni chama makini kuliko hata ccm
 
Back
Top Bottom