hp4510
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 6,446
- 6,308
Nimefuatilia na kuziangalia picha ambazo Mh. Membe - Mgombea urais kupitia ACT amepigwa akiwa JNIA zinaleta maswali mengi kuliko majbiu.
1. Nani alimpiga hizo picha?
2. Kwa nini apigwe picha bila hata ridhaa yake?
3. Kwa nini ziwekwe kwenye mitandao ya kijamii na wengine hasa viongozi wa kisiasa kuzitolea matamko?
Ni kweli watu hupiga picha wakiwa Airport lakini ukiangalia makini na hasa picha ya pili, inaonesha kabisa ni CCTV camera ya Airport ndiyo ilitumika.
Sasa swali nani aliruhusu zitoke/downloaded kutoka harddisk au server ya Security System ya Airport na kwa minajili gani?
Huyo aliyeruhusu zitoke sio mtu mdogo lazima atakuwa na mamlaka pale Uwanjani, je hili si kosa kisheria?
Kuna jambo hapo la kufikirika hapo!
View attachment 1566302
View attachment 1566303
Na mm Nashangaa shida ni nn, kwamba ukiwa mgombea wa urais unakuwa huna mamlaka ya kusafiri Inje ya inchi au ni nn?
What if anaenda Leo na kurudi J2 na j3 akaendelea na majukumu yake