Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,172
- 7,428
Kwa sasa kama ilivyo kwa vyama vingine vya upinzani, ACT nao wanakimbizana na matukio. Hatuwalaumu sana kwa hilo kwa sababu mbalimbali lakini kuna tatizo kubwa Zaidi ambalo sasa linajitokeza. Changamoto kubwa zaidi ni kwamba; baadhi ya viongozi wa ACT wamekuwa na utaratibu wa kukimbilia kuwa 'wakwanza' kuripoti matukio yenye utata kwa habari wanazozipata mtandaoni.
Tunawashauri kama watashawishika na kuona hoja tutakazozitoa hapa zina uzito,basi hata kama wamechagua kukimbizana na matukio; angalau wajiepushe kukimbilia kuwa wakwanza kuripoti matukio yanayojitokeza mitandaoni na hasa ambayo ni 'negative'. Hii ni kwa sababu zifuatazo;-
Tunawashauri kama watashawishika na kuona hoja tutakazozitoa hapa zina uzito,basi hata kama wamechagua kukimbizana na matukio; angalau wajiepushe kukimbilia kuwa wakwanza kuripoti matukio yanayojitokeza mitandaoni na hasa ambayo ni 'negative'. Hii ni kwa sababu zifuatazo;-
- Asilimia fulani ya taarifa zinazoanzia mitandaoni juu ya matukio tata zinakuwa za uongo.
- Viongozi wakubwa wa vyama wanaposema kitu halafu kikawa si sahihi, namna ya kurudishia na kuendelea kuaminika inakuwa ngumu kidogo. Kwa hiyo kwa mfano, kama taarifa imetolewa na viongozi wa chama na baadae kubainika ni uongo, ni tatizo kubwa.na
- Viongozi wakubwa wanatakiwa kujiepusha na ishu ndogo ndogo ili kupata muda wa kutosha kutafakari na kushughulikia ishu kubwa.