Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
Kwanza nianze kwakupongeza uamuzi wa busara wa Maalim Seif na wanamageuzi wote toka CUF walioporwa chama chao na CCM kwakushirikiana na Dola kujiunga na ACT kuendeleza mapambano. Ukomavu huu umewaacha hoi ccm wasiamini matokeo haya kwa kazi kubwa waliyoifanya kwa miaka minne ambapo inahitimishwa kwakiimarisha upinzani nchini badala ya kuubomoa.
Kwa zaidi ya masaa 24 sasa nimeona maoni ya jumla ya wadau wa siasa na wengine wasomi wazuri wakihitimisha kuwa sasa 2020 ACT kitakuwa ndio chama kikuu cha Upinzani nchini. Nimestaajabu sana huu muono unatako wapi? Nikajaribu kufuatilia kwa undani, nikajiridhisha ni propaganda iliyobuniwa na walioratibu kifo cha CUF, kwakuwa lengo lao ilikuwa ni kuua upinzani na upinzani wa kweli kwao ilikuwa ni CHADEMA.
Hii sio busara ya kiuchambuzi kubeba maoni ya mtaani nakufanya ndio tafakuri tanzu ya kisiasa, Mimi kama mwanasiasa mwanamajumui, nakubaliana kwamba ujio mpya wa Maalim Seif utazaa siasa mpya Bara, lakini naamini kwa dhati ya moyo na akili, Zanzibar itabaki ileile ya Maalim Seif ya 1995 hadi 2020. Hapa aliyeliwa ni CCM, Hesabu zao zimebuma na katika hili chama cha maoinduzi na dola yao wamepoteza pesa na muda kutwanga maji kwenye kinu.
Kwamba Maalim kuhamia ACT basi hii nihitimisho kwamba ACT kitakuwa chama kikuu cha upinzani 2020, huu ni upungufu wa ufikiri, Maalim alikuwa CUF, Je CUF kilikuwa chama kikuu cha upinzani? Chama cha ACT uchaguzi wa 2015 kilipata asilimia 0.2, je hii ni tafsiri kwamba Maalim kujiunga kitakuwa chama kikuu cha Upinzani? Majibu haya hoja hizo hayajibiwi kisiasa bali kwa namba na sayansi ya siasa.
Hatuzungumzi haya kwa kuhisia tu bali siasa ni namba, tukirejea takwimu za uchaguzi mkuu Tanzania 2015, matokeo ya jumla tunaona wazi ya kwamba uchaguzi wa mwaka huo uliohusisha majimbo 258 kati ya 262, CCM ilishinda ubunge katika majimbo 188, CUF 35, Chadema 34, NCCR–Mageuzi kiti kimoja. NLD haikupata kiti wakati ACT – Wazalendo ilipata kiti kimoja.
Kwamsingi huo, CCM ilipata viti maalumu 64, Chadema 36 na CUF 10. Kwa hesabu hiyo, Chadema ilifikisha wabunge 70 kutoka 48 wa mwaka 2010, CUF ilifikisha wabunge 45 kutoka 36 wa mwaka 2010 wakati NCCR-Mageuzi ilishuka kutoka wabunge wanne wa 2010 hadi mmoja na kufanya idadi ya wabunge wa Ukawa kuwa jumla 116. CCM ilifikisha wabunge 252.
Sasa turejee idadi ya wabunge 45 wa CUF, Wabunge 3 wamejivua uanachama na kujiunga CCM, nakufanya wabaki 39 tu. Na kati ya hao 39, wabunge 27 wa majimbo kati yao 22 kutoka Zanzibar, Wabunge 3 wa bara na Mbunge 1 wa viti maalumu hawa wanamuunga mkono Maalim Seif yaani hawa wamehamia ACT. Huku wabunge 4 wa majimbo na 9 wa viti maalumu hawa wako na Lipumba.
Sasa ili chama kiwe chama kikuu cha Upinzani ni lazima kiwe na idadi kubwa ya wabunge wa upinzani katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Na katika kutilia mkazo hilo, katiba ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na kanuni za baraza la wawakilishi Zanzibar zimeweka utaratibu mzuri wa uwakilishi kutoka Zanzibar.
Kifungu cha 142 (1) cha Kanuni za Baraza la wawakilishi Zanzibar kimeeleza kuwa kutakuwa na wajumbe watano watakaochaguliwa na Baraza, kwa mujibu
wa masharti ya 66(1) (c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuliwakilisha Baraza katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwanadharia hiyo, utaratibu wakuwapata wajumbe hao watano kwa Zanzibar umeelezwa katika katiba ya zanzibar, na kwa desturi utaratibu umekuwa ukitoa wajumbe wawili kutoka CUF na watatu kutoka CCM. Nakudanya idadi ya wawakilishi watano kutimia kutoka visiwani humo.
Sasa tukirejea kwenye namba tunapata kuona kwa tafsiri ya kawaida hadi dakika hii uchaguzi ungefanyika na wabunge walewale toka CUF wakashinda na kuwa wabunge toka ACT, Hii inamaana ACT itakuwa na wabunge 27 na Zitto 1 ambapo inakuwa 28. Viti maalumu wanaweza kupata 18, Sasa Jumla kuu wanakuwa na 38. Je hii inaweza kukiondoa CHADEMA chenye wabunge 70, kilichopata 36% ya kura uchaguzi 2015? Utoto huo. Zingatia ACT ilipata kura 0.2% tu.
Tutumie njia mbadala, tufanye wabunge 15 wa Chadema hawatarejea Bungeni, hivyo kufanya Chadema ipate wabunge 55 tu, na tufanye ACT itaongeza idadi ya Wabunge 15 hivi nakufikisha 53. Je itawezaje kuwa Chama kikuu cha upinzani kwa wabunge 53 tu dhidi ya Chadema yenye wabunge 55 baada ya kuporwa majimbo 15? Labda tunaishi katika fikra ndogo na kuogopa kufikiri kikubwa. Kuwa chama kikuu cha Upinzani Zanzibar au kuwa Chama Tawala Zanzibar hakukupi tiketi ya mojakwamoja kuwa chama kikuu cha upinzani Tanzania.
Hapa tathimini inafanyika huku Chama kizima cha Chadema kiko mahakamani, yaani viongozi wote na wanachama wake wote wenye ushawishi wako mahakamani kwa miaka minne mfululizo, Viongozi wakuu washakaa gerezani kwa zaidi ya miezi mitatu, Mikutano ya kisiasa imefungwa isipokuwa kwa ccm tu, Uhuru wa kutoa maoni umefungwa isipokuwa kwaccm tu. Bado Chadema itaendelea kuwa Chama kikui cha upinzani kama sikuwa chama Tawala 2020, na ikiwa kutakuwa na umoja katika upinzani, ni dhahiri kuwa kwa 99.9 CCM itaondoka madarakani ama itahitaji serikali ya mseto ili kuongoza nchi. Bunge litaamuliwa na upinzani.
Nimalize kwakuwatakia safari njema wale wanaohitaji kuhama vyama vyao, muda uliosalia ni mchache, kwani sheri ya vyama vya siasa ikishasainiwa mlazimika kubaki katika vyama vyenu hadi 2022.
Kama hujawahi kushuhudia uchaguzi mgumu na wahatari zaidi duniani, basi 2020 jiandae kushuhudia Rais Magufuli akikabidhi ofisi kwa njia ya amani kuipisha Chadema chini ya Rais Tundu Antipas Lissu. Hutaki unaacha!
Na Yericko Nyerere
Kwa zaidi ya masaa 24 sasa nimeona maoni ya jumla ya wadau wa siasa na wengine wasomi wazuri wakihitimisha kuwa sasa 2020 ACT kitakuwa ndio chama kikuu cha Upinzani nchini. Nimestaajabu sana huu muono unatako wapi? Nikajaribu kufuatilia kwa undani, nikajiridhisha ni propaganda iliyobuniwa na walioratibu kifo cha CUF, kwakuwa lengo lao ilikuwa ni kuua upinzani na upinzani wa kweli kwao ilikuwa ni CHADEMA.
Hii sio busara ya kiuchambuzi kubeba maoni ya mtaani nakufanya ndio tafakuri tanzu ya kisiasa, Mimi kama mwanasiasa mwanamajumui, nakubaliana kwamba ujio mpya wa Maalim Seif utazaa siasa mpya Bara, lakini naamini kwa dhati ya moyo na akili, Zanzibar itabaki ileile ya Maalim Seif ya 1995 hadi 2020. Hapa aliyeliwa ni CCM, Hesabu zao zimebuma na katika hili chama cha maoinduzi na dola yao wamepoteza pesa na muda kutwanga maji kwenye kinu.
Kwamba Maalim kuhamia ACT basi hii nihitimisho kwamba ACT kitakuwa chama kikuu cha upinzani 2020, huu ni upungufu wa ufikiri, Maalim alikuwa CUF, Je CUF kilikuwa chama kikuu cha upinzani? Chama cha ACT uchaguzi wa 2015 kilipata asilimia 0.2, je hii ni tafsiri kwamba Maalim kujiunga kitakuwa chama kikuu cha Upinzani? Majibu haya hoja hizo hayajibiwi kisiasa bali kwa namba na sayansi ya siasa.
Hatuzungumzi haya kwa kuhisia tu bali siasa ni namba, tukirejea takwimu za uchaguzi mkuu Tanzania 2015, matokeo ya jumla tunaona wazi ya kwamba uchaguzi wa mwaka huo uliohusisha majimbo 258 kati ya 262, CCM ilishinda ubunge katika majimbo 188, CUF 35, Chadema 34, NCCR–Mageuzi kiti kimoja. NLD haikupata kiti wakati ACT – Wazalendo ilipata kiti kimoja.
Kwamsingi huo, CCM ilipata viti maalumu 64, Chadema 36 na CUF 10. Kwa hesabu hiyo, Chadema ilifikisha wabunge 70 kutoka 48 wa mwaka 2010, CUF ilifikisha wabunge 45 kutoka 36 wa mwaka 2010 wakati NCCR-Mageuzi ilishuka kutoka wabunge wanne wa 2010 hadi mmoja na kufanya idadi ya wabunge wa Ukawa kuwa jumla 116. CCM ilifikisha wabunge 252.
Sasa turejee idadi ya wabunge 45 wa CUF, Wabunge 3 wamejivua uanachama na kujiunga CCM, nakufanya wabaki 39 tu. Na kati ya hao 39, wabunge 27 wa majimbo kati yao 22 kutoka Zanzibar, Wabunge 3 wa bara na Mbunge 1 wa viti maalumu hawa wanamuunga mkono Maalim Seif yaani hawa wamehamia ACT. Huku wabunge 4 wa majimbo na 9 wa viti maalumu hawa wako na Lipumba.
Sasa ili chama kiwe chama kikuu cha Upinzani ni lazima kiwe na idadi kubwa ya wabunge wa upinzani katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Na katika kutilia mkazo hilo, katiba ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na kanuni za baraza la wawakilishi Zanzibar zimeweka utaratibu mzuri wa uwakilishi kutoka Zanzibar.
Kifungu cha 142 (1) cha Kanuni za Baraza la wawakilishi Zanzibar kimeeleza kuwa kutakuwa na wajumbe watano watakaochaguliwa na Baraza, kwa mujibu
wa masharti ya 66(1) (c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuliwakilisha Baraza katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwanadharia hiyo, utaratibu wakuwapata wajumbe hao watano kwa Zanzibar umeelezwa katika katiba ya zanzibar, na kwa desturi utaratibu umekuwa ukitoa wajumbe wawili kutoka CUF na watatu kutoka CCM. Nakudanya idadi ya wawakilishi watano kutimia kutoka visiwani humo.
Sasa tukirejea kwenye namba tunapata kuona kwa tafsiri ya kawaida hadi dakika hii uchaguzi ungefanyika na wabunge walewale toka CUF wakashinda na kuwa wabunge toka ACT, Hii inamaana ACT itakuwa na wabunge 27 na Zitto 1 ambapo inakuwa 28. Viti maalumu wanaweza kupata 18, Sasa Jumla kuu wanakuwa na 38. Je hii inaweza kukiondoa CHADEMA chenye wabunge 70, kilichopata 36% ya kura uchaguzi 2015? Utoto huo. Zingatia ACT ilipata kura 0.2% tu.
Tutumie njia mbadala, tufanye wabunge 15 wa Chadema hawatarejea Bungeni, hivyo kufanya Chadema ipate wabunge 55 tu, na tufanye ACT itaongeza idadi ya Wabunge 15 hivi nakufikisha 53. Je itawezaje kuwa Chama kikuu cha upinzani kwa wabunge 53 tu dhidi ya Chadema yenye wabunge 55 baada ya kuporwa majimbo 15? Labda tunaishi katika fikra ndogo na kuogopa kufikiri kikubwa. Kuwa chama kikuu cha Upinzani Zanzibar au kuwa Chama Tawala Zanzibar hakukupi tiketi ya mojakwamoja kuwa chama kikuu cha upinzani Tanzania.
Hapa tathimini inafanyika huku Chama kizima cha Chadema kiko mahakamani, yaani viongozi wote na wanachama wake wote wenye ushawishi wako mahakamani kwa miaka minne mfululizo, Viongozi wakuu washakaa gerezani kwa zaidi ya miezi mitatu, Mikutano ya kisiasa imefungwa isipokuwa kwa ccm tu, Uhuru wa kutoa maoni umefungwa isipokuwa kwaccm tu. Bado Chadema itaendelea kuwa Chama kikui cha upinzani kama sikuwa chama Tawala 2020, na ikiwa kutakuwa na umoja katika upinzani, ni dhahiri kuwa kwa 99.9 CCM itaondoka madarakani ama itahitaji serikali ya mseto ili kuongoza nchi. Bunge litaamuliwa na upinzani.
Nimalize kwakuwatakia safari njema wale wanaohitaji kuhama vyama vyao, muda uliosalia ni mchache, kwani sheri ya vyama vya siasa ikishasainiwa mlazimika kubaki katika vyama vyenu hadi 2022.
Kama hujawahi kushuhudia uchaguzi mgumu na wahatari zaidi duniani, basi 2020 jiandae kushuhudia Rais Magufuli akikabidhi ofisi kwa njia ya amani kuipisha Chadema chini ya Rais Tundu Antipas Lissu. Hutaki unaacha!
Na Yericko Nyerere