Acknowlegment kutoka kwa waandaji wa old skool bash

Binti Maringo

JF-Expert Member
Jul 4, 2007
2,804
87
Kwa wanajumuiya wote wa Kitanzania,
salaaam!!

Tunapenda kutumia nafasi hii kuwaomba radhi jamii ya Watanzania wote waliojitokeza kwa mamia yao kwenye sherehe ya "OldSchool" mjini Columbus tarehe 5/7/2008.

Hakuna kina cha maneno au upambaji wa hoja unaoweza kuelezea masikitiko yetu kwa kushindwa kufanya siku hiyo kuwa ya kukumbukwa kwa uzuri wake, burudani yake na zaidi ya yote muziki wake mzuri, muziki wa zamani ambao wengi waliutarajia.

Licha ya maandalizi yetu yote tunaweza kukiri kwamba jukumu la kuandaa shughuli hiyo lilizidi mara nyingi sana uwezo wetu kama waandaji na hilo peke yake limekuwa funzo kubwa kwetu. Funzo la kwamba, tukitaka kuandaa kitu kizuri kwa Watanzania wenzetu hatuna budi kufanya na zaidi ya kufanya maandalizi yetu kuwa ya hali ya juu, bora, na ambayo yanaendana na viwango vya kimataifa.

Tulishindwa katika kuwapatia burudani ya muziki ambao wengi waliutarajia. Licha ya kwamba nyimbo zenyewe zilikuwa ni zile zilizopendwa miaka "ile" tatizo la uwezo mdogo wa nguvu ya umeme katika jengo tulilofanyia tafrija ilisababisha vyombo vilivyotumika kutumia nguvu nyingi ya umeme na hivyo kusababisha muziki kukatika katika. Hii ilikuwa ni kero ya dhahiri na jambo ambalo liliongeza kero zilizotangulia.


Kuna mengine mengi ambayo tungeweza kuyaeleza na kuwaomba radhi kwayo lakini kwa kifupi ni kuwa kama waandaji tunabeba mzigo wote wa kuwajibika kwa kushindwa kufanikisha kwa kiwango cha kuridhisha na zaidi ya kuridhisha yaani kuzikosha roho zenu pale Columbus siku ile ya Jumamosi. Funzo tulilolipata ni kubwa, na kwa pamoja na mmoja mmoja tunakubali makosa na mapungufu yote na ni sisi tu wenye kustahili kubeba lawama hizo zote.


Tunawashukuru kwa moyo wenu wa ukarimu na ukaribu, na zaidi ya yote kuchukiliana nasi katika mapungufu hayo. Tunawashukuru zaidi kwa kuja kwenu na kuweza kujumuika na kukutana na watanzania wengine katika mkusanyiko huu. Tunawashukuru wale wote waliojaribu kwa namna yao kutengeneza kilichoharibika. Mapungufu ya muziki yaliyojitokeza si kosa la Ma DJ tuliowaalika bali ni makosa ambayo hata wao yalikuwa nje ya uwezo wao, na kwa niaba yao tunawaombeni radhi ninyi nyote.

Tunaahidi kuwa kabla ya kuandaa kitu kingine kama hiki tutakaa chini na kujifunza (take a course) na kuhakikisha kuwa katika uchanga wa shughuli zetu hizi tutaweza muda si mrefu ujao kufanya tafrija ambayo siyo tu itakidhi matarajio ya wageni wetu bali itapita kila njozi yao na kufanya ndoto zao za tafrija zote kutimia. Tunahakikisha tunapata mawazo ya watu wengine waliobobea katika mambo kama haya.

Hilo tunawaahidi na mapungufu ya safari hii tunaomba mtuchukilie kama uchanga wa shughuli hizi kubwa lakini pia msisite kutupa nafasi inayostahili tutakapoweza kuwathibitishia pasipo shaka kuwa tumekomaa kufanya shughuli kama hizi.

Tunatanguliza Shukrani Zetu za dhati kwa uwezo wenu mkubwa wa kuelewa suala hili kwani Kufanya Kosa Sio kosa bali kurudia kosa ndio kosa.


Aksanteni nyote

Waandaji, (Tina Lupembe, Phanuel Ligate, Peter Kirigit, Lucas Mukami)
 
haya sasa maneno. Let me think about forgiving... najua itachukua muda kidogo I have to factor kukosa mechi ya simba na yanga, bbq, muziki wa kukatikakatika n.k na kupata parking ticket!...
 
Haya sasa maneno...
Duh, ebu niitazame picha upya!..Phanuel wangu, Peter wangu kazi kweli kweli kutoa kile kilicho rohoni laa sivyo niongeomba mjiuzuru!
Vizuri sana kama mmeweza kutambua mapungufu yenu....na pengine hizi apologies mngezitanguliza pale kiwanjani na ukumbini maanake sioo wote wanaoingia hapoa kijiweni.. bado mnahitaji support ya Watanzania..
Next time niiteni gwiji, muzee wa starehe niwakomboe ktk maandalizi!..haaa haaa.
 
In other words,this was daylight robbery at its worst,hii columbine massacre ooops sorry,,,,yaani hii columbus massacre,whereas people were mugged of their hard earned dollars inanikumbusha mbali,kwa sisi watu wa west lake lile basi la BIJAMPOLA lilivvyotapeli watu enzi zile
 
.... nawapongeza kwa prompt acknowledgment ya baadhi ya michemsho iliyotokea.

.... ni hard lesson, waandaaji walipaswa kuomba ideas kutoka kwa watu mbalimbali, hata siye wengine ambao tulijua fika kuwa hatutamudu kuhudhuria. one or two ideas from steved or kadampinzani wouldn't have hurt anybody, but could've been useful.... mwamba ngomba ngozi huivutia kwake..... nisiseme mengi.

....Hata hivyo, HONGERENI SANA kwa yote mliyofanikisha.

SteveD.
 
Poleni waandaaji..mimi kama mtu ambaye nimesha tayarisha vitu kama hivi naelewa jinsi gani mlivyo jisikia....lakini chukueni hii kitu kama mfano and take lesseons learned very seriously kwani Watanzania ni forgiving people.. I am sure mtabounce back stronger than ever. But all in all we had fun haswa kukutana na watu wengi..Amani
 
Mimi naona wadau muwasamehe bure najua wengi mtakuwa na ghadhabu kwa kupata music yenye kikohozi ni furaha kubwa kukutana wadau na kufahamiana.

Na nyie "mapromota" next time ombeni ushauri kwa wakongwe wa kuandaa haya makitu... inaonekana kuna kaharufu ka ufisadi mlifanya....
 
Basi na kale kafaida ka vijisenti walikokapata baada ya kuwawekesha watu kwenye gereji chafu na yenye joto iliyokuwa na choo kimoja kichafu na watoe kafara hapa JF. Invisible mkuu; hakikisha kunaingia vijisenti mkobani, na utupe uthibitisho maana walikitumia hiki kijiwe sana kukonvinsi watu kwenda.
Na vili vile......siendelei, natema mate chini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom