Acheni kupotosha alichokuwa amesema Tundu Lissu kuhusu Acacia na MIGA

Naikumbuka hiyo kesi, ilifunguliwa na Acacia. Tusisahau tangia mwanzo Acacia walionekana kupinga moja kwa moja madai ya serikali huku parent company, Barrick ikiweka mbele suala la majadiliano na serikali!!

So, few months ago baada ya Barrick kuonesha wazi kwamba wanataka "kulimaliza" hili suala kwa majadiliano kutokana na makubaliano ya awali waliyokuwa wameafikiana na serikali, hapo hapakuwa na namna zaidi ya Acacia kufuta kesi kesi ili hatimae Barrick warudi mezani!

Kwa mfano, habari ya Reuters kuhusu Acacia kuachana na kesi ni hii hapa:-
Unaona hapo hiyo habari imeripotiwa July 17, 2019.

Makubaliano ya Awali kati ya Serikali na Barrick Gold ni haya hapa:-
View attachment 1239915

Unaona hapo makubaliano yanaonekana ni July 19, 2019... yaani siku 2 tu baada ya Acacia kutangaza kuachana na kesi!!!

Kwahiyo ndo tunarudi pale pale... kwenye makubaliano ya awali tayari Barrick alishafahamu watatakiwa kulipa ile USD 300 Million TU, tena kwa masharti kwamba, hatimae makinikia yataruhusiwa kusafirishwa!!

Hiyo kwao ilikuwa ni advantage ndio maana Acacia wakafuta kesi! Na hapa hapa JF nilishawahi kuongea kwamba Acacia watajifanya kuendelea ku-press hard ili kuitisha serikali na hatimae wakubaliane na suala la "Kishuka Uchumba" tu, na ndicho kilichotokea!!

Sasa kama Kabudi anahisi anastahili pongezi kwa Acacia "kufuta" kesi kutokana na ushawishi wake, then we've long way to go! Kama ni kutokana na ushawishi wake, kwanini Acacia wafute kesi baada ya kuona makubaliano yameshafikiwa na badala ya kulipa yale matrilioni, hivi sasa watalipa tu mabilioni na makinikia yanaruhusiwa kusafirishwa!!
Huwa nashangaa sana watu wanaoiona ACACIA kuwa ni tofauti na BARRICK GOLD. ni Barrick walioanzisha kampuni tanzu ya ACACIA ikiwa ni namna ya kushughulika na nchi zetu za kimagumashi, na viongozi magumashi. Nyerere mwenye akili aliwaambia kabisa mapema kwamba subirini kwanza, tujipange kama nchi. uroho wa Mkapa ukatuingiza kichwa kichwa. PAPARA ZA MAGUFULI NAZO ZIKATUTOA MATAKO MATAKO.
Barrick anaonesha kidole kwa ACACIA kwamba ndiyo mtoto mkorofi, wakati yeye ni msikivu na mtiifu!!! Barrick ni wazoefu sana wa kupora mali kama hizi kwa miaka nenda miaka rudi.
Hata hii habari ya kampuni ya pamoja na hisa 16%, subiri kwanza uone je tutapata kitu? nina mashaka sana tutaambulia propaganda tu.
 
Naona unazungumzia mambo kinadharia zaidi,
Alichoshauri Lissu ni kwamba kama serikali inataka kupambana na ACACIA bila kuburuzwa katika mahakama za kimataifa na kushindwa kesi(kunyolewa kwa chupa) basi hawana budi awali ya yote, kujitoa katika hivyo vyombo kama MIGA,hakuna sehemu aliyosema serikali itishie kujitoa.

Halafu unaposema kuwa serikali imeambulia pesa kiduchu sana (kishika uchumba tu) kwa kuzingatia deni ambalo serikari ilisema inawadai jamaa,
Je unafahumu lengo kuu la serikali lilikuwa ni lipi tangu mwanzoni kabisa mwa hilo sakata?


Imeshatokea kichwani mwako ukajiuliza kuwa pengine serikali ilikuwa na lengo lake lingine kabisa nyuma ya pazia tangu kusimamisha usafirishaji wa makinikia mpaka kuundwa kwa hizo tume na mwishowe kutangaza hilo deni lao la matrilion ya tshiling?

Vp kama lengo lao lilitimia kama walivyotaka wao na hicho kishika uchumba ni BONUS tu?
Kuna mahali niliposema Lissu alisema serikali itishie kujitoa?! Halafu acheni porojo za kwamba eti serikali ilikuwa na lengo fulani ndo maana ikakubali kuchukua USD 300M.... hizo ni POROJO! In short, serikali ilichemka, na hawakuwa na namna zaidi ya kuchukua hizo 300M!
 
Wafuasi wa Lumumba ama kwa ile kukosa uelewa, au kwa makusudi tu, since Day 1 wamekuwa wakipotosha ambacho Tundu Lissu aliongea kuhusu MIGA! Au wakati mwingine inawezekana ni kutokana na tabia yetu Watanzania ya kutotafuta ukweli!

Binafsi nimekuwa nikilijadili suala la makinikia since Day 1, na kwavile nilikuwa nafuatilia sana nakumbuka vyema nini Tundu Lissu aliongea, na ninamnukuu hapa chini:-
Hiyo ndiyo hoja ya Lissu... kwamba, kama kweli Serikali ya Magufuli ilikusudia kupambana na Acacia, basi walitakiwa kwanza wajitoe kwenye mkataba wa MIGA!

Ushauri sawa na huo wa TL ulikuja tena kutolewa na Dr. Rugemeleza Nshala mbele ya Wabunge walipokuwa wanatafuta maoni ya wadai wakati wa utungwaji wa sheria mpya ya madini.

Gazeti la the Citizen linatujuza:pia the Citizen wanatukumbusha kwamba, Dr. Nshala ni Mtanzania wa pili kutoa ushauri kama huo huku wa kwanza akiwa ni TL:-Kwa maajabu ya wale waliofuatilia suala la umakini, watu wakapotosha na kudai TL amesema tukipambana na Acacia, watatupeleka MIGA, na huu ndo umekuwa wimbo wa wana-CCM na wafuasi wa serikali!

Busara ya TL kushauri kujitoa MIGA unaweza kuiona kupitia tovuti ya MIGA, hivi ndivyo wanasema:-Hapo wanaongea wazi ni namna gani pamoja na mambo mengine, wana jukumu la kulinda uwekezaji dhidi ya maamuzi ya serikali!

Sasa basi, hoja ya TL ilikuwa ni kwamba, tukishavurugana na Acacia ,watakachofanya wao ni kile ambacho kinafanywa na kampuni zingine... yaani kukimbilia Mahakamani, au MIGA!

Lakini kama kweli umeamua kupambana na hawa jamaa, unachotakiwa ni kuchomoa betri kwa kujitoa MIGA ili wasiwe na kwa kukimbilia zaidi ya kwenda kwenye mahakama zetu wenyewe... yaani mahakama zile zile zinazoamua ma-DED wanastahili kusimamia uchaguzi ambao mmoja wa washiriki ni mwajiriwa wake mwenyewe!!!

Kwa maana nyingine, ukishajitoa MIGA maana yake ni kwamba unakuwa huzitambui mahakama zao! Ni kama United States asivyoitambua International Criminal Court, matokeo yake pamoja na uhalifu wote wa kivita wanaoufanya duniani kote, huwezi kumpeleka Mmarekani ICC .

Maajabu makubwa zaidi ya taifa hili, badala ya kuiangalia hoja ya TL Critically, watu wale wale wanaojiona ndio wazalendo zaidi, wakaona mtu kama TL anastahli kuuawa mara moja... na wafuasi wa CCM na serikali yake wamekuwa wakiirudia kauli hii mara kwa mara!!!!

Je, kumpuuza TL kumetugharimu kama taifa?!

Serikali na watetezi wataendelea kujitekenya wenyewe na kucheka wenyewe lakini ukweli ni kwamba imetugharimu kama taifa!

Sote tumeshuhudia danadana za Acacia... watetezi wa serikali wasichofahamu ni kwamba, danadana zote zile ni kwa sababu walifahamu maji yakiwazidi shingo, wangekimbilia mahakamani ambako katu tusingetoka.

Na kwa Mtanzania yeyote anayekejeli kauli hiyo ya TL, kwa hakika anatakiwa kujitafakari mara mbili... anatakiwa kujitafakari kwa sababu sisi ni victim wa hizi mahakama, hususani kupitia IPTL!

Sote sisi tunakumbuka kushikiliwa kwa Bombardier kwa wiki kadhaa kule Canada kutokana na maamuzi yaliyotolewa na mahakama za aina hii!!

Hivyo basi, ili kujilinda tusipelekwe kwenye mahakama kama hizi ambazo kuchomoka ni nadra sana, ndipo TL akasema ukitaka kupambana na hawa watu, basi jitoe MIGA lakini sio kwamba tukipamba na Acacia, wanatupeleka mahakamani!!!

Je, kwanini Acacia Hawajatupeleka MIGA?

Kwa kifupi ni kwamba, Acacia hawakuwa na sababu ya kutupeleka MIGA kwa sababu serikali imepita njia ambayo ni nafuu maradufu kwa Acacia!

Kuweka kumbukumbu sawa, wakati Profesa Orosso akiwakilisha Ripoti ya Pili, alitoa takwimu ya pesa ambayo serikali ilipoteza kama mapato! Prof. Orosso na timu yake waliweka makadirioo ya kiwango cha chini kabisa ambacho serikali ilipoteza, na kiwango cha juu kabisa!

Tuachane na kiwango cha juu kabisa, Profesa Orosso anatujuza, na ripoti kamili inapatikana tovuti ya Ikulu:-Hicho ndicho kiwango cha chini kabisa... na ukichanganya na adhabu (ya kuchelewesha kulipa kodi), jumla ndo ile figure maarufu ya TRilioni 450!!

Sasa hebu tujiulize... Uchunguzi uliofanywa na akina Prof Mruma na mwenzake Prof Orosso (pamoja na timu ya watu wa TRA), ilionesha Acacia wamekwepa kulipa Sh. 68 kwa miaka 17. Leo hii serikali imekubali kulipwa Sh. 700 Billion... sasa hata kama wewe ndo ungekuwa Acacia, ungeenda MIGA kufanya nini?!

Na kama ilivyo kwa mahakama zingine, kesi za MIGA zinachukua miaka na miaka!! Sasa kwanini ukae miaka yote hayo huku biashara ikiendelea kuathirika kwa kushindwa kusafirisha makinikia?!

Sasa wakati Wafuasi wa CCM na serikali yake wakiendelea kumkejeli TL kwamba mbona hao Acacia hawajaenda MIGA, jibu ndo hilo hapo! Hawajaenda kwa sababu sisi ndio tumeliwa! Tumekubali kuchukua Sh. 700 Billion out of 68 Trillion!!!!

NOTE: Moderator punguzeni kasi ya kuunganisha threads bila sababu za msingi eti kisa tu kuna baadhi ya keywords zinafanana!!! Kuandika haya mambo it takes time... so, it sucks mtu unapoteza saa moja na ushee kuandika thread, unakuja next time, huoni kwa sababu imeunganishwa na thread nyingine!
Rubbish
 
Lakini tukijitoa huko MIGA siyo kwamba ndo tunawafukuza hao wawekezaji....


Ni nani yuko tayari kupeleka mtaji wake sehemu ambayo hata uhakika wa kuuchukua haupo...!

Tatizo la msingi katika nchi yetu sio ubovu wa wawekezaji bali ubovu wetu watanzania kwa kutanguliza maslahi binafsi dhidi ya taifa, Harvard hata sisi tumepeleka watu wetu lakini mbona hawafanyi makubwa, jibu wanarudi wanafikia kwenye mikono michafu ya wanasiasa matokeo yake wanageuka mazimwi manyonya damu .
 
Huwa nashangaa sana watu wanaoiona ACACIA kuwa ni tofauti na BARRICK GOLD. ni Barrick walioanzisha kampuni tanzu ya ACACIA ikiwa ni namna ya kushughulika na nchi zetu za kimagumashi, na viongozi magumashi. Nyerere mwenye akili aliwaambia kabisa mapema kwamba subirini kwanza, tujipange kama nchi. uroho wa Mkapa ukatuingiza kichwa kichwa. PAPARA ZA MAGUFULI NAZO ZIKATUTOA MATAKO MATAKO.
Barrick anaonesha kidole kwa ACACIA kwamba ndiyo mtoto mkorofi, wakati yeye ni msikivu na mtiifu!!! Barrick ni wazoefu sana wa kupora mali kama hizi kwa miaka nenda miaka rudi.
Hata hii habari ya kampuni ya pamoja na hisa 16%, subiri kwanza uone je tutapata kitu? nina mashaka sana tutaambulia propaganda tu.
Yaani hilo la kwamba Acacia zamani ilikuwa inaitwa African Barrick Gold... baadae wakabadili jina ndo wakaitwa Acacia lakini ni wale wale tu... nishasema sana hapa!! Ajabu, kuna watu wanaamini Acacia ni shetani na Barrick ni malaika!!
 
..alishauri tusitaifishe.

..serikali haikutaifisha.

..alisema madai ya usd 191 na ripoti za kina Prof.Mruma na Prof.Ossoro zina kasoro kubwa.

..serikali imeachana na madai ya 191 billion badala yake ime-negotiate, pia imeachana na ripoti za maprofesa.

..alisema tutashtakiwa miga. Kweli tulishtakiwa na kesi iliondolewa baada ya Tz kukubali "kishika uchumba" na minority shareholders wa accacia kununuliwa kwa bei waliyoridhia.

..alisema kama tunaona miga wanatuonea basi serikali ijitoe miga na migogoro yote kati ya Tz na wawekezaji wa nje iamuliwe na mahakama za ndani.

..serikali imepeleka bungeni sheria kwamba mashauri na migogoro ya uwekezaji itaamuliwa na mahakama za Tz.

..hili la kujitoa miga, Lissu alikuwa akishauri kwa mikataba mipya, siyo mikataba ya zamani.

..mwenye uelewa walikuwa wanajua kuwa anachoshauri Tundu Lissu ni sahihi.


Ngoja nikwambie kitu mkuu,
Unajua kwamba mtu anaweza akawa anazo HOJA za msingi kabisa katika jambo fulani lakini tatizo kubwa likawa ni jinsi gani huyo mtu anawasilisha hizo hoja zake kwa wahusika?

Ni sawa tu na mtu anayo story nzuri yenye mafunzo mengi/vichekesho vingi,lakini tatizo lake hajui jinsi ya kuiwasilisha kwa ufasaha hiyo story mbele ya hadhira yake ili watu wajifunze kweli/wacheke kweli kweli kama alivyotaka yeye.


Utaona kwamba jamaa alishindwa hapo hata kama alikuwa nazo kweli hoja zilizokuja kufanyiwa kazi mbeleni,
Mtu mwerevu anajua jinsi ya kuwasilisha hoja zake smartly na lengo lake kutimia bila kuleta mambo ya sijui rubbish na majigambo mengine ya kijinga tu,ambayo yatawafanya wengine wakuone mpuuzi tu hata kama kweli unazo hoja za msingi.
 
Lakini tukijitoa huko MIGA siyo kwamba ndo tunawafukuza hao wawekezaji....


Ni nani yuko tayari kupeleka mtaji wake sehemu ambayo hata uhakika wa kuuchukua haupo...!

Tatizo la msingi katika nchi yetu sio ubovu wa wawekezaji bali ubovu wetu watanzania kwa kutanguliza maslahi binafsi dhidi ya taifa, Harvard hata sisi tumepeleka watu wetu lakini mbona hawafanyi makubwa, jibu wanarudi wanafikia kwenye mikono michafu ya wanasiasa matokeo yake wanageuka mazimwi manyonya damu .
Watu wanapeleka mitaji maeneo ya vita, ije kuwa nchi ambayo imejitoa MIGA! Na haya mambo muhimu kwa wawekezaji sio hii mikataba ya MIGA bali uongozi uliopo madarakani!!

Nchi inaweza isiwe mwanachama wa MIGA sio kwa sababu ya kutaka ukorofi dhidi ya wawekezaji bali kwa kuona mkataba hauna maslahi kwake! Na pasipo na MIGA, taifa husika linaweza kuwa na mifumo yake yenyewe ya uwazi na huru; na hivyo kutokuwa tishio kwa wawekezaji!!!

But on top of that, hata kama ingekuwa kujitoa, Tanzania isingekuwa ya kwanza! Back 2007, Bolivia baada ya kuona wanaibiwa sana kwenye mafuta yao, hiki ndicho kilifuata:-
Bolivia.png

Mwaka 2012 nao, Venezuela nao wakachomoa betri!

Kisha soma hapa:-
Contrary to the perception that ICSID mechanism has been accepted in the majority of American hemisphere, many states of this region continue to be extremely distant from ICSID : Canada, Cuba, México and Dominican Republic have not ratified ICSID Convention. In the case of Mexico, this attitude is rated by a Mexican author as “wise and rebellious”.
All in all, hiyo sio hoja. Hoja ni upotoshaji wa kile alichosema TL. Akina Mataga wanaacha maelezo ya awali ya TL na kuchukua kipengelea kwamba "TL alisema serikali ikiwabughudhi Acacia basi watatupeleka mahakamani"

Na kimsingi sio alisema Tz ijitoe, bali kama serikali haijaanza kupambana na hawa akina Acacia, ijitoe kwanza ili kuwanyima pumzi Acacia!!
 
Bila misaada na mikopo kutoka kwa mabeberu nchi hii haitawaliki. Tunapata misaada na mikopo katika kufanikisha bajeti ya serikali kuu. Bila hiyo hata mishahara serikali ingeshindwa kulipa. Pia tunapata misaada na mikopo kufanikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo kama ujenzi wa miundombinu ya barabara, reli, maji, umeme, meli nk. Hata baadhi ya semina na makongamano ya serikali yanafadhiliwa na fedha za mabeberu.

Hivyo puuzia kabisa majigambo ya kiongozi wetu eti nchi hii inaweza kuwa donor country badala yake ni matonya country!
Hahaha nilitaka kuelewa, mikopo ndiyo inaitwa misaada au ni vitu viwili tofauti?!
Maana serikali inatumia mapato ya ndani, na mnasema tunapata misaada, yenyewe inatumika wapi na lini na nani anaitoa?!
Je, huwa tunakopa lini ikiwa inaonekaka pesa za ndani zinatosha na mnasema misaada tuna pata?!
Nani anatumia misaada hii, au inatumika wapi, lini na kwanini?!
 
Utaona kwamba jamaa alishindwa hapo hata kama alikuwa nazo kweli hoja zilizokuja kufanyiwa kazi mbeleni,
Mtu mwerevu anajua jinsi ya kuwasilisha hoja zake smartly na lengo lake kutimia bila kuleta mambo ya sijui rubbish na majigambo mengine ya kijinga tu,ambayo yatawafanya wengine wakuone mpuuzi tu hata kama kweli unazo hoja za msingi.
TL aliwasilisha hoja yake vizuri tu bali watu walipotosha! Waliacha yoooooooooooooote aliyoongea waka-exaggerate kipengele kimoja wapo na kudai alisema "...serikali ikiwasumbua Acacia basi Acacia itatupeleka mahakamani!" Hicho sicho alichosema TL
 
Naikumbuka hiyo kesi, ilifunguliwa na Acacia. Tusisahau tangia mwanzo Acacia walionekana kupinga moja kwa moja madai ya serikali huku parent company, Barrick ikiweka mbele suala la majadiliano na serikali!!

So, few months ago baada ya Barrick kuonesha wazi kwamba wanataka "kulimaliza" hili suala kwa majadiliano kutokana na makubaliano ya awali waliyokuwa wameafikiana na serikali, hapo hapakuwa na namna zaidi ya Acacia kufuta kesi kesi ili hatimae Barrick warudi mezani!

Kwa mfano, habari ya Reuters kuhusu Acacia kuachana na kesi ni hii hapa:-
Unaona hapo hiyo habari imeripotiwa July 17, 2019.

Makubaliano ya Awali kati ya Serikali na Barrick Gold ni haya hapa:-
View attachment 1239915

Unaona hapo makubaliano yanaonekana ni July 19, 2019... yaani siku 2 tu baada ya Acacia kutangaza kuachana na kesi!!!

Kwahiyo ndo tunarudi pale pale... kwenye makubaliano ya awali tayari Barrick alishafahamu watatakiwa kulipa ile USD 300 Million TU, tena kwa masharti kwamba, hatimae makinikia yataruhusiwa kusafirishwa!!

Hiyo kwao ilikuwa ni advantage ndio maana Acacia wakafuta kesi! Na hapa hapa JF nilishawahi kuongea kwamba Acacia watajifanya kuendelea ku-press hard ili kuitisha serikali na hatimae wakubaliane na suala la "Kishuka Uchumba" tu, na ndicho kilichotokea!!

Sasa kama Kabudi anahisi anastahili pongezi kwa Acacia "kufuta" kesi kutokana na ushawishi wake, then we've long way to go! Kama ni kutokana na ushawishi wake, kwanini Acacia wafute kesi baada ya kuona makubaliano yameshafikiwa na badala ya kulipa yale matrilioni, hivi sasa watalipa tu mabilioni na makinikia yanaruhusiwa kusafirishwa!!
Leo nimeona hii Barrick to Restart Gold Mining in Tanzania
Huko wallstreet journal, tuwekee kwenye lugha ya SADC mkuu. Imeelezea yoote ya nyuma kwa kizungu, sasa sisi huku SADC tunaweza kupitwa na huondo motomoto wa leo.
 
CCM ni wasanii hatari, leo wanataka kujitoa kwamba eti hawakushiriki ku sign hii mikataba ya kilaghai ya madini na maliasili nyingine nyingi...yaani wanatakiwa wawaombe radhi watanzania... tumeibiwa mno sababu ya CCM.

Leo hii wanataka kuwageuzia kibao watetezi wa mali asili zetu miaka nenda rudi kama kina Lissu na wengineo kwamba si wazalendo bali eti ni watetezi wa mabeberu.

CCM hebu muogopeni Muumba mbingu na nchi.....anawaona mnayoyafanya...!!
 
huwezi ukawa msaliti alafu uendelee kuishi, kama kuna mwingine anataka yampate ya kumpata bas afanye usaliti kwa nchi. wamesomeshwa kwa pesa za serikali wazazi wao walikua masikini wa kutupwa, wakulima waliochoka 'strong and tired peasants' leo wanakashifu na kuisaliti nchi kwa kitu so called democracy. endeleeni kuzusha ila sio usaliti... you will kiss your @ss
 
CCM ni wasanii hatari, leo wanataka kujitoa kwamba eti hawakushiriki ku sign hii mikataba ya kilaghai ya madini na maliasili nyingine nyingi...yaani wanatakiwa wawaombe radhi watanzania... tumeibiwa mno sababu ya CCM.

Leo hii wanataka kuwageuzia kibao watetezi wa mali asili zetu miaka nenda rudi kama kina Lissu na wengineo kwamba si wazalendo bali eti ni watetezi wa mabeberu.

CCM hebu muogopeni Muumba mbingu na nchi.....anawaona mnayoyafanya...!!
Yaani ni mchezo unachezwa ili kufuta uzalendo wa Tundu Lissu toka enzi na enzi, pale alipokuwa akipambana na ULOFA wa Mkapa na kuwatetea wananchi mamia walioswekwa ndani kwa kesi za kubambikiza. Leo CCM wale wale wamebadili ngozi toka mbwa mwitu kuwa kondoo, wakijifanya watetezi. Kumbe ni kambi ya majizi watupu. hebu waulize ule mgao wa pesa za Escrow zile za kigeni, kuna hata mmoja amewajibishwa???
 
Back
Top Bottom