Accounts jobs zinakuwa replaced na technology kila siku, wahasibu tumejiandaaje? Next 10 yrs hatutahitajika tena

FRESHMAN

JF-Expert Member
Sep 29, 2011
8,819
33,449
Habari wadau..

Binafsi ni mhasibu kwa taaluma..

Nimesoma research ya PWC, research ya Oxford university, research ya kpmg, na research nyingi za vyuo tofauti..

Zinaonesha kwamba IT technology aka robot accountant ndio watafanya kazi za uhasibu zote kuondoa human error na ku cut cost... sababu uhasibu ni jobs zinazofata principles.. so ni sahihi na rahisi kuweka principles kwenye software au erp, yenyewe ikatengeneza Financial statement na kila report hadi hesabu za kodi bila makosa kuliko kuendelea kutumia binadamu.

Wanahisi miaka inayokuja mahitaji ya wahasibu yatapungua sana na kufikia 10 yrs to 20 ijayo ndio hatutahitajika tenaa.

Na hii itaendana na taaluma zote ambazo zinafata principles kufanya kazi.. eg. bank tellers watakuwa replaced na ATM zinazo deposit hela na kutoa hela na cashless payment inayo grow kwa kasi

Link ya PWC hii hapa

Accounting jobs most at risk from automation, warns PwC | Accountants Daily

Oxford university link

47% of Jobs Will Disappear in the next 25 Years, Says Oxford University

Na dalili zimeanza kuonekana Tanzania mtu una CPA ila mwajiri anaringa anakwambia mshahara mdogo sana na kama hutaki acha kazi... sababu anajua hatuna umuhimu kama zamani sababu ya technology....
 
Hata kazi zako zikiwa automated kiasi gani, bado nafasi ya binadamu iko pale pale. Tayari zipo accounting packages kibao zenye uwezo wa kufanya mengi ikiwemo hayo ya kuandaa hizo financial statements, na mengineyo, lakini uangalizi wa binadamu lazima uwepo. Systems zita automate na record nyingine zitaendelea kuingizwa manually kwenye vitabu. Katika mambo sensitive kama rekodi za kiuhasibu huwezi kutegemea automated systems pekee, lazima kuwe na dual data/record keeping.
 
huko ni kujidanganya.. IT huwa haitaki wafanyakazi wengi.. mfano hai angalia ofisini kwenu IT dept ina watu wangapi..

whatsapp , facebook au google ni apps zinazohudumia dunia nzima.. ila ofisi ni staffs wachache sana kulinganisha na wateja wao kibao..

kampuni hata iwe kubwa vipi kila ilipo duniani lazima iwe na mhasibu... aka accounts dept.. lakini kampuni za IT kina google hazina hiyo changamoto..

system adminstrator mmoja anahudumia hata nchi nzima... ila kiuhasibu haiwezekani


Mkuu, ni shift of economy.

Demand ya accountants inapungua huku demand ya professionals wa hizo teknolojia ikiongezeka.
 
hizo ni research za waliotuletea huo uhasibu,,, hao ndio waliotunga a, e, i, o, na u, ndio waliotunga namba,, na kila taaluma ndio wanaosema hivyo... kama wewe mtanzania unabishana nao sawa... ila tujiandae wazungu na computer hazijawai kumuacha mtu salama.

binadamu sio kama haitajiki.. ila mahitaji ya binadamu ndio yanapungua.. badala ya kuwa na binadamu 100 kama zamani kufanya kazi... anakuwa mmoja tu ambaye anaisapoti technology

Hata kazi zako zikiwa automated kiasi gani, bado nafasi ya binadamu iko pale pale. Tayari zipo accounting packages kibao zenye uwezo wa kufanya mengi ikiwemo hayo ya kuandaa hizo financial statements, na mengineyo, lakini uangalizi wa binadamu lazima uwepo. Systems zita automate na record nyingine zitaendelea kuingizwa manually kwenye vitabu. Katika mambo sensitive kama rekodi za kiuhasibu huwezi kutegemea automated systems pekee, lazima kuwe na dual data/record keeping.
 
Binaadam bado muhimu kuliko robot, waishie huko huko sisi huku tunataka binaadamu bado.
 
Artificial intelligence

Google hilo neno la kizungu ndio utaona raha!

Zinaundwa meli zitakazokuwa hazina mabaharia.

Magari yanayojiendesha (tena wana mpango haya magari yasimilikiwe na mtu binafsi) unaingia linakupeleka unakotaka unashuka linachukua ustaarabu wake.

Operation hospitali kufanywa na robots (zina error margin ndogo saaana ukilinganisha na binadamu wanakupasua kichwa badala ya mguu)

Imeazimiwa "artificial intelligence" ipigwe marufuku kwenye silaha na mapigano ya vita.

Heri yao waliotangulia mbele za haki.
 
huko ni kujidanganya.. IT huwa haitaki wafanyakazi wengi.. mfano hai angalia ofisini kwenu IT dept ina watu wangapi..

whatsapp , facebook au google ni apps zinazohudumia dunia nzima.. ila ofisi ni staffs wachache sana kulinganisha na wateja wao kibao..

kampuni hata iwe kubwa vipi kila ilipo duniani lazima iwe na mhasibu... aka accounts dept.. lakini kampuni za IT kina google hazina hiyo changamoto..

system adminstrator mmoja anahudumia hata nchi nzima... ila kiuhasibu haiwezekani
Mkuu, mimi sikumaanisha demand ya IT professionals kwenye maofisi itapanda sana.

Internal IT departments hazina uwezo wa kutengeneza hizi automation systems. Kwa hilo huwa wanaoutsource kwa purely technoloy companies.

Sasa basi, hao tech providers wanaobuild hizi solutions ndio watakaoajiri IT professionals kwa wingi mno. Hili soko zamani halikuwepo.

Nadhani umenielewa sasa.
 
Kazi ya mhasibu sio kuhesabu hela na kutengeneza fs tu. Mhasibu ni kiini mhimu katika kutengeneza plan na sera za kifedha ktk kampuni. Kwa hiyo hayo maroboti si dhani kama yananafasi hiyo
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom