Abromovich wa Chelsea atua nchini kupanda Kilimanjaro!

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,800
30,725
Mmliki wa klabu ya soka ya Chalsea FC Roman Abromovich ametua mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya kupanda mlima Kilimanjaro.

Bwana Abromovich alitua jana jioni saa 1 akiwa na watu sita na amefikia katikaHotel ya River Trees Country iliyoko eneo la USA River nje kidogo ya Mji wa Arusha .
 
ni kweli hizi taarifa nilizipata 1 month ago lakini nilikuwa sijui atakuja lini huko
 
licha ya kuwa na utajili wa kutisha lakini anaonekana mtu wa kawaida sana
 
To be honest i am very interested on this man's bness atitude.
 
Huyu jamaa ni mbaguzi sana kwanini amechagua kwenda Arusha na Kilimanjaro badala ya Kigoma au pemba ?.Bwa ha ha ha ha .
 
Huyu jamaa ni mbaguzi sana kwanini amechagua kwenda Arusha na Kilimanjaro badala ya Kigoma au pemba ?.Bwa ha ha ha ha .
Kigoma kufanya nini aisee!!!?????????????????????????????????? kwani hiv kuna hata uwanja wa ndege kule? hivi wewe ukihamishiwa kikazi kule utaenda???
 
According to a Time magazine article last December, Mr Abramovich spent $200m (£120.2m) to $300m of his own money to build everything from hotels and cinemas to supermarkets.

Such largesse has aroused suspicions from Mr Abramovich's critics, who think he is using Chukotka as a springboard for higher political office. But he told Time: "It's a new endeavour for me. I've never run a territory. I've never talked publicly to people. I've got to try it just to see whether I like it."

He even brought staff from Sibneft to run the province. Despite all his efforts, the region was recently declared bankrupt and public sector salaries went unpaid for months.

Thats him!
 
Kigoma kufanya nini aisee!!!?????????????????????????????????? kwani hiv kuna hata uwanja wa ndege kule? hivi wewe ukihamishiwa kikazi kule utaenda???

Mkuu Nyani kwanini serekali haijengi uwanja wa ndege ili Abromovich aende Kigoma.Lawama zinatakiwa ziende serekali kwa uzembe wa maksudi.

Kile chuo kikuu cha Nelson Mandela kulikuwa na kampeni kubwa hapa jamvini kijengwe pemba au Kigoma badala ya Arusha.Nadhani baadhi ya wanajamvi mtaanza kuelewa ni kwanini chuo kinajengwa Arusha badala ya miji iliyolala kama Kigoma na Pemba.
 
Mkuu Nyani kwanini serekali haijengi uwanja wa ndege ili Abromovich aende Kigoma.Lawama zinatakiwa ziende serekali kwa uzembe wa maksudi.

Kile chuo kikuu cha Nelson Mandela kulikuwa na kampeni kubwa hapa jamvini kijengwe pemba au Kigoma badala ya Arusha.Nadhani baadhi ya wanajamvi mtaanza kuelewa ni kwanini chuo kinajengwa Arusha badala ya miji iliyolala kama Kigoma na Pemba.

Nyie mnahangaika nini??? labda wenyewe hawataki kwani serikalini hakuna viongozi wa juu kutoka pemba au kigoma???? je katika ile thread Zito kutoka kigoma alikuja akasema kuwa aliomba chuo kijengwe kula wakamkatalia na je kama walimkatalia walimpa sababu gani??? na hata kama watajenga nani wataenda kusoma kwenye hicho chuo?ok!! then dk.Sheini naye hawezi kushawishi chuo kijengwe visiwani? na kama hawezi ana faida gani sasa kwa watu wa visiwani??samahani najua hii mada haiendani na hi thread
 
Mkuu Nyani kwanini serekali haijengi uwanja wa ndege ili Abromovich aende Kigoma.Lawama zinatakiwa ziende serekali kwa uzembe wa maksudi.

Kile chuo kikuu cha Nelson Mandela kulikuwa na kampeni kubwa hapa jamvini kijengwe pemba au Kigoma badala ya Arusha.Nadhani baadhi ya wanajamvi mtaanza kuelewa ni kwanini chuo kinajengwa Arusha badala ya miji iliyolala kama Kigoma na Pemba.
Nyie mnahangaika nini??? labda wenyewe hawataki kwani serikalini hakuna viongozi wa juu kutoka pemba au kigoma???? je katika ile thread Zito kutoka kigoma alikuja akasema kuwa aliomba chuo kijengwe kula wakamkatalia na je kama walimkatalia walimpa sababu gani??? na hata kama watajenga nani wataenda kusoma kwenye hicho chuo?ok!! then dk.Sheini naye hawezi kushawishi chuo kijengwe visiwani? na kama hawezi ana faida gani sasa kwa watu wa visiwani??samahani najua hii mada haiendani na hi thread
 
Wakuu heshima mbele

Hivi kweli utalii wa Tanzania tunatumiaje ujio wa Tajiri Abramovich kufaidika katika kujitangaza kwenye soko la utalii duniani!!!!!!!

Hivi kweli tutashindwa kweli hata kusema sasa basi kwamba Kilimanjaro ipo Tanzania na sio Kenya kwa ushahidi wa tajiri huyu kutua ndani ya ardhi yetu na anapandia Tanzania!!!!

Kama haya hayajaonekana basi sisi ni vilaza wa kila kitu na wizara nafikiri inahitaji kuangaliwa upya.
 
Mmliki wa klabu ya soka ya Chalsea FC Roman Abromovich ametua mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya kupanda mlima Kilimanjaro.

Bwana Abromovich alitua jana jioni saa 1 akiwa na watu sita na amefikia katikaHotel ya River Trees Country iliyoko eneo la USA River nje kidogo ya Mji wa Arusha .

Acknowledge please! Did you write this piece or you just lifted it from somewhere, probably a newspaper? The chance is high that you lifted it from a daily newspaper, right? Do you know that you have committed a serious offense? Who told you life's that easy? Copying and pasting, uh!
 
Acheni mambo ya kigoma pemba,mpanda na maeneo mengine nahisi itafika wakati watu wataanza kusema kwanini hajafikia nyumbani kwangu?
 
Acheni mambo ya kigoma pemba,mpanda na maeneo mengine nahisi itafika wakati watu wataanza kusema kwanini hajafikia nyumbani kwangu?

ni kweli kabisa Mvina

Ila sasa ninachojiuliza kwanini serikali haitumii nafasi kama hii kuutangaza utalii wetu kupitia watu mashuhuri kama hawa au ndio mazezeta wapo wengi maana kusoma hawajui mpk kuangalia picha napo kunawashinda

Mtu kama huyu angetengenezewa mazingira mazuri huwezi amini hata Chelsea ungeshangaa wangekuja Tanzania lakini mijitu ipo ipo tuu ila nasubiria nione kama mijitu ya Wizara itakuwa imefanya initiatives zozote kwenye issue ya promotion kupita nafasi hii finyu ya ujio wa TAJIRI LA RUSSIA/ STANFORD BRIDGE
 
ni kweli kabisa Mvina

Ila sasa ninachojiuliza kwanini serikali haitumii nafasi kama hii kuutangaza utalii wetu kupitia watu mashuhuri kama hawa au ndio mazezeta wapo wengi maana kusoma hawajui mpk kuangalia picha napo kunawashinda

Mtu kama huyu angetengenezewa mazingira mazuri huwezi amini hata Chelsea ungeshangaa wangekuja Tanzania lakini mijitu ipo ipo tuu ila nasubiria nione kama mijitu ya Wizara itakuwa imefanya initiatives zozote kwenye issue ya promotion kupita nafasi hii finyu ya ujio wa TAJIRI LA RUSSIA/ STANFORD BRIDGE

I think you get it wrong. Uh, hold on! Chukulia wewe ni "mjitu" wa wizarani, ungefanya "initiative gani kwenye issue ya promotion kupita [kupitia] nafasi hii finyu ya ujio wa TAJIRI LA RUSSIA/STANFORD [STAMFORD] BRIDGE"? Ni nani atamlipa huyu tajiri kama atatumika kwenye "promotion" (if this is a right word to use) - kuitangaza Tanzania? Is he that cheap? Do you think he has time for that? Do you think he has that damn good reputation? Na kama kila tajiri akiitembelea nchi yetu atatumika kufanya "promotion" (whatever it means!), then what's the whole deal of them rich visiting our country?

Anyway, ningeomba kufahamu ni namna gani huyu jamaa (na wengine wengi wanaotembelea Tanzania without your knowledge) anaweza kutumika kufanya "promotion"? I don't get it!
 
HUKU bilionea wa Urusi, Roman Abramovich, ambaye ni mmiliki wa klabu ya Chelsea akitarajiwa kushuka leo kutoka kilele cha Mlima Kilimanjaro, safari aliyoianza Septemba 3, juhudi za mashabiki wa timu kuonana na bilionea huyo zimekwama.

Kikwazo ni viongozi wa mashabiki hao kushindwa kuonana na wakala wa kampuni iliyomleta bilionea huyo ya African Environment, hivyo kuwa vigumu kutokana na kuwapo ulinzi mkali dhidi ya bilionea huyo.

Awali, mashabiki hao walipanga kuonana na bilionea huyo aliyetua nchini Septemba 2 na kuanza kupanda Mlima Kilimanjaro siku iliyofuata, ambaye anatarajiwa kushuka leo kabla ya kuondoka nchini kesho.

Kwa mujibu wa mratibu wa mashabiki hao, Stive Munguto ‘Ticha' alisema pamoja na nia yao njema ya kutaka kuonana na bilionea huyo, wamekwama baada ya kushindwa kuonana na viongozi wa African Environment.

"Tumefanya kila linalowezekana ili kuona ni njia gani itakayowezesha kuonana na Abramovich, lakini tumekwama kukutana na viongozi wa Kampuni ya African Environment," alisema Munguto.

Hata hivyo, alisema bado wanaendelea na jitihada zao za mwisho ili kuweza kuzungumza naye baada ya kushuka leo, baada ya kufanikiwa kufika eneo la barafu, umbali wa mita 4,800 kutoka usawa wa bahari.

Bilionea huyo wa Kirusi anashuka leo kutoka Mlima Kilimanjaro akipitia lango la Mweka, kabla ya kufanya ziara ya siku moja katika Chuo cha Hifadhi ya Wanyamapori Mweka.

Source Tanzania daima
 
Acknowledge please! Did you write this piece or you just lifted it from somewhere, probably a newspaper? The chance is high that you lifted it from a daily newspaper, right? Do you know that you have committed a serious offense? Who told you life's that easy? Copying and pasting, uh!

Mkuu Zungu nina rafiki yangu anafanyakazi Africa Enviroment ndiye aliyenitonya.Pia kazi ninayoifanya ina mahusiana makubwa na hawa jamaa wa sector ya utalii.Kwa mfano wiki mbili zilizopita mtoto wa Ghadafi alikuwa anafanya kufuru kubwa Grumeti reserves.

Ningeamua kuileta habari za mtoto wa Ghadafi nayo ungesema ni copy & paste.
 
I think you get it wrong. Uh, hold on! Chukulia wewe ni "mjitu" wa wizarani, ungefanya "initiative gani kwenye issue ya promotion kupita [kupitia] nafasi hii finyu ya ujio wa TAJIRI LA RUSSIA/STANFORD [STAMFORD] BRIDGE"? Ni nani atamlipa huyu tajiri kama atatumika kwenye "promotion" (if this is a right word to use) - kuitangaza Tanzania? Is he that cheap? Do you think he has time for that? Do you think he has that damn good reputation? Na kama kila tajiri akiitembelea nchi yetu atatumika kufanya "promotion" (whatever it means!), then what's the whole deal of them rich visiting our country?

Anyway, ningeomba kufahamu ni namna gani huyu jamaa (na wengine wengi wanaotembelea Tanzania without your knowledge) anaweza kutumika kufanya "promotion"? I don't get it!

Mazee, Hapo ndipo watazania tunapotoka Ziro! Wakati mwingine ni suala la Ubunifu na pengine huna hata haja ya kuongea na Abrahimovich mwenyewe! Nina hakika kuwa Mheshimiwa huyo angekuwa amekwenda kupanda Mlima Kenya basi magazeti Yote, Blog Zote za wakenya na hata Shirika lao la ndege lingetafuta namna fulani ya kutangaza ujio wa mheshimiwa huyo na jinsi mlima/nchi yao ilivyo nzuri kiasi cha mtu kama Abrahmovich kutoka huko atokako kuja kuiona/kuupanda!
Ni lazima huyu mtu atakuwa na kundi kubwa la wafuasi ulimwenguni ambao watapenda kujua nchi/mlima aliotembelea na kupanda una nini cha ajabu na kama nao wana swenti za kutosha wanaweza nao kufunga safari kuja kujionea kile alichofanya Idol wao! Narudia, Ni suala la Ubunifu tu ambalo sadly, hatuna!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom