Yussufhaji
Member
- Sep 9, 2018
- 35
- 28
Abiy Ahmed ana njia moja tu kuitoa Ethiopia katika mzozo wa vita ya wenyewe kwa wenyewe
04/11/2021
Novemba 6 mwaka jana, Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed alitangaza operesheni za Kijeshi katika mji wa Tigray dhidi ya vikosi vya T.P.L.F, kufuatia madai ya Serikali ya Ethiopia kuwa T.P.L.F ilivamia kambi ya jeshi la taifa hilo,
Huko nyuma, tayari kulikuwepo na sintofahamu ya kisiasa baina ya Serikali kuu ya Ethiopia iliyopo Adis Ababa na ile ya Mkoa wa Tigray kufuatia Serikali ya Mkoa wa Tigray kukaidi agizo la kutofanya uchaguzi wakati wa janga la Uviko-19 na kupelelea Adis Ababa kukatisha udhamini wa kibajeti kwa Mkoa wa Tigray,
Hakuna asiyejua nguvu kubwa waliyonayo T.P.L.F na udhibiti wake wa siasa za Ethiopia kwa miongo kadhaa, T.P.L.F ni kikundi kilichoshiriki kuunda Serikali Kuu ya Ethiopia kwa miongo mitatu mfululizo,
Pamoja na harakati za propaganda za Serikali ya Abiy Ahmed kuwa inaenda kushinda mzozo huu wa kivita, lakini inasemekana hali ni tofauti kabisa na picha inayo ionesha Adis Ababa kwa jamii ya kimataifa,
Kwa mujibu wa Mtandao wa New York times katika makala yake yenye kichwa cha habari "Kwanini Ethiopia ipo katika vita yenyewe kwa yenyewe?" inaeleza kuwa zaidi ya watu milioni 1.7 wameyahama makaazi yao kutokana na mzozo huu wa kivita, na zaidi ya 63,000 wamekimbilia nchi jirani ya Sudan huku watu zaidi ya 350,000 wakikumbwa na janga la njaa,
Huku T.P.L.F wakisemekana wakipata nguvu siku baada ya siku pamoja na uwezo mkubwa wa Jeshi la Ethiopia na mshirika wake katika vita hiyo, Eritrea!
Siku chache zilizopita Abiy Ahmed alitumia mtandao wa kijamii wa Facebook kuwataka raia wa nchi hiyo kuchukua silaha kupambana na waasi wa T.P.L.F aliyo waita ni magaidi, ikiwa ni dalili ya wazi kabisa ya kuzidiwa kwa Adis Ababa katika vita hiyo,
Waswahili wanasema, mtu mzima akivuliwa nguo huchutama!
Mwaka 2009, Abiy Ahmed alishinda tunzo ya amani ya Nobel baada ya kufanikiwa kusuluhisha mgogoro wa mpaka baina ya nchi yake Ethiopia na Eritrea kwa njia ya mazungumzo,
Iweje Abiy Ahmed aweze kupatana na jirani yake kwa njia ya mazungumzo ashindwe kupatana na ndugu zake kwa njia ya mazungumzo????
Tuseme Abiy Ahmed hazijui nguvu zilizokita mizizi za T.P.L.F katika siasa za Ethiopia kwa miongo zaidi ya mitatu? kwa maana aliamua kucheza na moto kwa kutumia mikono yake miwili???
Kwa uoni wangu njia pekee ya kutatua mzozo huu wa vita ya wenyewe kwa wenyewe ili isienee zaidi na kuleta madhara zaidi kwa Ethiopia ni mazungumzo!
Abiy Ahmed asijisahau kuwa tayari ana jalada jengine la kesi katika uwanja wa kimataifa kufuatia ujenzi wa bwawa la kufua umeme linalojengwa na Ethiopia katika mto Nile na kuzua mtafaruku na vuta nkuvute na jirani zake Misri na Sudan,
Abiy Ahmed aelewe kuwa, wakati huu Ethiopia inahitaji kuwa tulivu kuliko wakati wowote ule katika historia yake.
@Mtoto_wa_Mkulima
Karibu!
Yussuf H. Khatib
Email: hajjyussuf2@gmail.com
WhatsApp: Jaa WhatsAppissa
Sent from my SHV40 using JamiiForums mobile app
04/11/2021
Novemba 6 mwaka jana, Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed alitangaza operesheni za Kijeshi katika mji wa Tigray dhidi ya vikosi vya T.P.L.F, kufuatia madai ya Serikali ya Ethiopia kuwa T.P.L.F ilivamia kambi ya jeshi la taifa hilo,
Huko nyuma, tayari kulikuwepo na sintofahamu ya kisiasa baina ya Serikali kuu ya Ethiopia iliyopo Adis Ababa na ile ya Mkoa wa Tigray kufuatia Serikali ya Mkoa wa Tigray kukaidi agizo la kutofanya uchaguzi wakati wa janga la Uviko-19 na kupelelea Adis Ababa kukatisha udhamini wa kibajeti kwa Mkoa wa Tigray,
Hakuna asiyejua nguvu kubwa waliyonayo T.P.L.F na udhibiti wake wa siasa za Ethiopia kwa miongo kadhaa, T.P.L.F ni kikundi kilichoshiriki kuunda Serikali Kuu ya Ethiopia kwa miongo mitatu mfululizo,
Pamoja na harakati za propaganda za Serikali ya Abiy Ahmed kuwa inaenda kushinda mzozo huu wa kivita, lakini inasemekana hali ni tofauti kabisa na picha inayo ionesha Adis Ababa kwa jamii ya kimataifa,
Kwa mujibu wa Mtandao wa New York times katika makala yake yenye kichwa cha habari "Kwanini Ethiopia ipo katika vita yenyewe kwa yenyewe?" inaeleza kuwa zaidi ya watu milioni 1.7 wameyahama makaazi yao kutokana na mzozo huu wa kivita, na zaidi ya 63,000 wamekimbilia nchi jirani ya Sudan huku watu zaidi ya 350,000 wakikumbwa na janga la njaa,
Huku T.P.L.F wakisemekana wakipata nguvu siku baada ya siku pamoja na uwezo mkubwa wa Jeshi la Ethiopia na mshirika wake katika vita hiyo, Eritrea!
Siku chache zilizopita Abiy Ahmed alitumia mtandao wa kijamii wa Facebook kuwataka raia wa nchi hiyo kuchukua silaha kupambana na waasi wa T.P.L.F aliyo waita ni magaidi, ikiwa ni dalili ya wazi kabisa ya kuzidiwa kwa Adis Ababa katika vita hiyo,
Waswahili wanasema, mtu mzima akivuliwa nguo huchutama!
Mwaka 2009, Abiy Ahmed alishinda tunzo ya amani ya Nobel baada ya kufanikiwa kusuluhisha mgogoro wa mpaka baina ya nchi yake Ethiopia na Eritrea kwa njia ya mazungumzo,
Iweje Abiy Ahmed aweze kupatana na jirani yake kwa njia ya mazungumzo ashindwe kupatana na ndugu zake kwa njia ya mazungumzo????
Tuseme Abiy Ahmed hazijui nguvu zilizokita mizizi za T.P.L.F katika siasa za Ethiopia kwa miongo zaidi ya mitatu? kwa maana aliamua kucheza na moto kwa kutumia mikono yake miwili???
Kwa uoni wangu njia pekee ya kutatua mzozo huu wa vita ya wenyewe kwa wenyewe ili isienee zaidi na kuleta madhara zaidi kwa Ethiopia ni mazungumzo!
Abiy Ahmed asijisahau kuwa tayari ana jalada jengine la kesi katika uwanja wa kimataifa kufuatia ujenzi wa bwawa la kufua umeme linalojengwa na Ethiopia katika mto Nile na kuzua mtafaruku na vuta nkuvute na jirani zake Misri na Sudan,
Abiy Ahmed aelewe kuwa, wakati huu Ethiopia inahitaji kuwa tulivu kuliko wakati wowote ule katika historia yake.
@Mtoto_wa_Mkulima
Karibu!
Yussuf H. Khatib
Email: hajjyussuf2@gmail.com
WhatsApp: Jaa WhatsAppissa
Sent from my SHV40 using JamiiForums mobile app