Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,603
- 29,743
TEMESA wanaoendesha mradi wa kuvusha abiria, magari na mizigo Kivuko cha Kigamboni, wamefanya upanuzi wa eneo la abiria upande wa Kigamboni.
Sambamba na upanuzi huo, wamejenga vyoo vya abiria eneo la banda la kusubiria kivuko.
Ujenzi bado unaendelea kukamilisha maeneo yaliyosalia lakini TEMESA wameruhusu sehemu hiyo kuanza kutumika. Tangu wameruhusu hadi sasa haijapita hata miezi miwili, lakini kwa aibu yetu watumiaji wa vyoo wamejitahidi kuharibu vyoo na mabomba ya maji kwenye sinki za kunawia mikono.
Hebu tujiulize, mtu unaenda haja ndogo kisha unakolokochoa pee pit sijui unafikiria mkojo unasukumwa kama.kimba au? Hali hii imesababisha maji na mikojo kusambaa chini eneo la.choo.
pee pit kilichoharibiwa na abiria..
Hali hii pia utaikuta upande wa pili kwenye vyoo jirani na kituo cha mwendokasi. Hapo uharibifu ni wa kudumu maana ni mwaka wa tatu sasa yale mabomba ya chooni yameharibiwa bila kurekebishwa
Kuna wakati inabidi kamera ziwepo ili kujua nani anaharibu mali ya umma awapo mawalitoni.
Sitaki kuamini kwamba mpaka leo kuna waMikoani ambao wanashindwa kuelewa matumizi ya maliwato kistaarabu
Sambamba na upanuzi huo, wamejenga vyoo vya abiria eneo la banda la kusubiria kivuko.
Ujenzi bado unaendelea kukamilisha maeneo yaliyosalia lakini TEMESA wameruhusu sehemu hiyo kuanza kutumika. Tangu wameruhusu hadi sasa haijapita hata miezi miwili, lakini kwa aibu yetu watumiaji wa vyoo wamejitahidi kuharibu vyoo na mabomba ya maji kwenye sinki za kunawia mikono.
Hebu tujiulize, mtu unaenda haja ndogo kisha unakolokochoa pee pit sijui unafikiria mkojo unasukumwa kama.kimba au? Hali hii imesababisha maji na mikojo kusambaa chini eneo la.choo.
Hali hii pia utaikuta upande wa pili kwenye vyoo jirani na kituo cha mwendokasi. Hapo uharibifu ni wa kudumu maana ni mwaka wa tatu sasa yale mabomba ya chooni yameharibiwa bila kurekebishwa
Kuna wakati inabidi kamera ziwepo ili kujua nani anaharibu mali ya umma awapo mawalitoni.
Sitaki kuamini kwamba mpaka leo kuna waMikoani ambao wanashindwa kuelewa matumizi ya maliwato kistaarabu