kindikwili
JF-Expert Member
- Oct 5, 2016
- 1,862
- 2,871
Habari iwe kwenu wakuu!
Leo nilikuwa nimepanda gari kwenda kazini (huwa napanda magari 2 hadi kufika kazini) cha kushangaza kwenye gari la kwanza mpaka nashuka nilihesabu watu wasio na barakoa wakafika 15 na kuna wakati gari ilikuwa na jumla ya watu 28 huku watu 15 wakiwa hawana barakoa kabisa. Njiani kuna wengine walikuwa wanashuka na wengine kupanda ila hata hao waliokuwa wanapanda wengine hawakuwa na barakoa kabisa.
Kwenye gari la pili ambalo huchukua watu wengi zaidi (kivukoni -tegeta) watu kama 6 hawakuwa na barakoa na wengine walikuwa wamevishikilia tu mikononi badala ya kuvaa. Inasikitisha kwamba hayo yanatokea hapa Dar es Salaam ambako matangazo ya corona yamejaa maeneo mbali mbali huku Radio zikitangaza sana juu ya corona. Hata pale ferry kwenye kuvuka baadhi ya watu hawanawi na siku hizi wale walinzi wa SUMA waliokuwa wanasimamia hawasimamii tena wakati mwingine maana si kwamba kila saa niko hapo ila hili nimelishuhudia wakati wa kuvuka wengine hawanawi tena.Kama hali hii ya watu kuzembea kuvaa barakoa wakiwa kwenye usafiri wa umma, kama watu watazembea kunawa mikono na kama wananchi hawatajua kwa uhakika kama ugonjwa bado upo au haupo basi huenda wakati nchi nyingine wanamalizana na tatizo hili sisi tutakuwa ndiyo kwanza tuko kwenye peak.
Ushauri!
1. Kwa wananchi wenzangu jua tu kwamba ikitokea umeugua huu ugonjwa ni wewe na familia yako ndiyo mtahangaika na ikitokea umefariki au umefiwa ni wewe ndiye umefiwa, hivyo tuvae barakoa na kunawa bila kusubiri kushurutishwa.
2. Kwa abiria wengine kukaa kimya wakati mtu wa jirani yako kwenye gari hajavaa barakoa ni kuhatarisha maisha yako. Mwambie bila kumuogopa kuwa avae barakoa hata akinuna wewe mwambie.
3. Tunapoendelea na kampeni ya kufukiza (kwa wanaojifukiza) tusisahau pia kuwasisitiza watu waendelee kuvaa barakoa, kunawa na kukwepa kukaa kwenye vikundi vya watu
4. Kwa jeshi la polisi na mamlaka endeleeni kukagua magari ya abiria na kama mtu atakutwa hana barakoa ashurutishwe kuvaa kwa nguvu
5. Bila taarifa za uhakika na za kuaminika tena ndani ya muda sahihi wananchi wataendelea kuzembea na ugonjwa unaweza ukaenea zaidi
Information is power wapendwa
Kindikwili
Leo nilikuwa nimepanda gari kwenda kazini (huwa napanda magari 2 hadi kufika kazini) cha kushangaza kwenye gari la kwanza mpaka nashuka nilihesabu watu wasio na barakoa wakafika 15 na kuna wakati gari ilikuwa na jumla ya watu 28 huku watu 15 wakiwa hawana barakoa kabisa. Njiani kuna wengine walikuwa wanashuka na wengine kupanda ila hata hao waliokuwa wanapanda wengine hawakuwa na barakoa kabisa.
Kwenye gari la pili ambalo huchukua watu wengi zaidi (kivukoni -tegeta) watu kama 6 hawakuwa na barakoa na wengine walikuwa wamevishikilia tu mikononi badala ya kuvaa. Inasikitisha kwamba hayo yanatokea hapa Dar es Salaam ambako matangazo ya corona yamejaa maeneo mbali mbali huku Radio zikitangaza sana juu ya corona. Hata pale ferry kwenye kuvuka baadhi ya watu hawanawi na siku hizi wale walinzi wa SUMA waliokuwa wanasimamia hawasimamii tena wakati mwingine maana si kwamba kila saa niko hapo ila hili nimelishuhudia wakati wa kuvuka wengine hawanawi tena.Kama hali hii ya watu kuzembea kuvaa barakoa wakiwa kwenye usafiri wa umma, kama watu watazembea kunawa mikono na kama wananchi hawatajua kwa uhakika kama ugonjwa bado upo au haupo basi huenda wakati nchi nyingine wanamalizana na tatizo hili sisi tutakuwa ndiyo kwanza tuko kwenye peak.
Ushauri!
1. Kwa wananchi wenzangu jua tu kwamba ikitokea umeugua huu ugonjwa ni wewe na familia yako ndiyo mtahangaika na ikitokea umefariki au umefiwa ni wewe ndiye umefiwa, hivyo tuvae barakoa na kunawa bila kusubiri kushurutishwa.
2. Kwa abiria wengine kukaa kimya wakati mtu wa jirani yako kwenye gari hajavaa barakoa ni kuhatarisha maisha yako. Mwambie bila kumuogopa kuwa avae barakoa hata akinuna wewe mwambie.
3. Tunapoendelea na kampeni ya kufukiza (kwa wanaojifukiza) tusisahau pia kuwasisitiza watu waendelee kuvaa barakoa, kunawa na kukwepa kukaa kwenye vikundi vya watu
4. Kwa jeshi la polisi na mamlaka endeleeni kukagua magari ya abiria na kama mtu atakutwa hana barakoa ashurutishwe kuvaa kwa nguvu
5. Bila taarifa za uhakika na za kuaminika tena ndani ya muda sahihi wananchi wataendelea kuzembea na ugonjwa unaweza ukaenea zaidi
Information is power wapendwa
Kindikwili