Uchaguzi 2020 Abdul Nondo atia nia ubunge Kigoma Mjini

Hata chato?
Chato hata Geita mgombea yeyote asiye Musukuma atashinda kwa urahisi maana Wasukuma wamechoka na usanii unaofanywa Kanda ya Ziwa. Sifiasifia na kuunga mkono tunaosikia kila siku toka sehemu mbalimbali nchini huwezi kusikia toka Geita au Chato labda toka kwa watafuta teuzi kama wakina Pascal Mayalla ambaye naye sasa haumi wala kupuliza baada ya kurudishiwa Press Card yake. Njaa haina adabu!
 
Nondo anataka ubunge kwani wale makaburu aka "wazalendo uchwara" walishamrudishia uraia wake!?
 
Watia nia ubunge kigoma mjini mpaka sasa kupitia ACT-WAZALENDO ni Abdul Nondo, Baba Levo. Bado najiuliza Zitto Kabwe atahama jimbo tena au atagombea nao kura za maoni, au hatagombea mwaka huu?
Nimepata taarifa kuwa Zitto anagombea uraisi
 
Zitto anajua kuseti mipango. Anajua vizuri hatashindana na CCM bali mkurugenzi na ffu!

Ameamua kuwapanga vijana wake nchi nzima wamsakie "asilimia ya kura za urais" ili apate ruzuku na hatimaye aweze kujilipa mshahara mzuri akisubiria baba jeska asitaafu ndipo aanze harakati tena
ACT haijulikani popote zaidi ya kigoma,hiyo asilimia tano ya kura ataipata Gungu?
 
Uraisi atagombea Membe, na hii itapelekea viti vingi vya ubunge huko kusini kuhamia ACT ,hasa vilivyokuwa CUF. Ndio maana Zitto anang'ang'ania Membe .Akikusanya viti vya Pemba,akakusanya vya kusini,akakusanya vya Kigoma hata viwili/vitatu atakuwa kapiga hatua na ruzuku itaongezeka, naona mwaka huu Zitto yupo kimkakati zaidi wakukuza chama. Lakini yote hayo yatatokea kama tume ikijaribu kufanya fair japo kidogo.

Baadaye ikiffanya FEA msije mkasema POLICMM ni sehemu ya ZITTTO..
 
Ni jambo jema,CCM lazima wabanwe mbavu kila kona na upinzani,Kila jimbo wawekwe watu wenye ushawishi.
Watakatwa wote hao, kama walivyokatwa kwenye serikali za mitaa. Kama wagombea wao wa serikali za mitaa walikatwa, wao madiwani na wabunge ni akina nani hadi wasikatwe, kwani wale wakataji wamestaafu? Watakatwa madiwani na wabunge wote , baada ya tarehe 5 August mtajionea
 
Back
Top Bottom