Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,480
- 9,241
Kampuni ya AAR Healthcare (T) Ltd imetangaza kuuza vifaa vyote vilivyopo kwenye kliniki zake saba nchini vilivyokuwa vikitumika kutoa huduma za afya.
Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya kampuni hiyo kutangaza kufunga kliniki zake zote zilizokuwa zinatoa huduma kwa wagonjwa wa nje kote nchini kwa sababu kampuni hiyo sasa imefilisiwa.
Aprili 28, 2021 wafanyakazi wa kampuni hiyo waliandamana katika ofisi za kampuni hiyo jijini Dar es Salaam wakidai kulipwa stahiki zao baada ya kupata taarifa kwamba kampuni hiyo ilikuwa imefiliwa.
Kwa mujibu wa tangazo katika gazeti la Mwananchi leo Mei 7, 2021 kampuni ya AAR imetangaza kuuza vifaa vyote vilivyokuwa vinatumika katika kliniki saba nchini zilizopo mkoani Dar es Salaam, Mwanza na Arusha.
AAR ina kliniki tano Dar es Salaam; Posta (City Centre Clinic na New Chato Clinic), Mbagala, Tabata na Tegeta wakati Mwanza iko moja eneo la Mlango Mmoja na Arusha moja eneo la Philips.
Tangazo hilo limebainisha vifaa vinavyouzwa kuwa ni kompyuta pamoja na vifaa vyake kama vile printa, UPS, server na kompyuta mpakato. Vingine ni vifaa vya kieletroniki kama vile friji, projekta, mifumo ya CCTV na vifaa vya kuunganishia mtandao wa intaneti.
Vilevile, AAR inauza vifaatiba kama vile stendi za dripu, vipimo cha mkojo (urine analyzers) na kitanda cha magurudumu kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza au wale wanaopokelewa kutoka kwenye gari la wagonjwa (collapsible stretcher trolley).
Kampuni hiyo pia inauza vifaa vya maabara kama vile mashine ya X-Ray, mashine ya oksijeni, mashine ya kupima shinikizo la damu na kipimio cha meno (dental unit).
Mbali na vifaa hivyo, kampuni ya AAR pia inauza samani mbalimbali kama vile meza na viti vya ofisini, stendi za TV, mashefu, makabati pamoja na mabenchi.
“Kliniki hizo ziko katika viwango vinavyohitajika katika tasnia na viko tayari kutumika. Vifaa vya kudumu vinapatikana kwa ajili ya watua huduma za afya,” linaeleza tangazo hilo huku likibainisha kwamba watakaohitaji vifaa watume maombi kabla ya Mei 17,2021.
Chanzo: Mwananchi
Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya kampuni hiyo kutangaza kufunga kliniki zake zote zilizokuwa zinatoa huduma kwa wagonjwa wa nje kote nchini kwa sababu kampuni hiyo sasa imefilisiwa.
Aprili 28, 2021 wafanyakazi wa kampuni hiyo waliandamana katika ofisi za kampuni hiyo jijini Dar es Salaam wakidai kulipwa stahiki zao baada ya kupata taarifa kwamba kampuni hiyo ilikuwa imefiliwa.
Kwa mujibu wa tangazo katika gazeti la Mwananchi leo Mei 7, 2021 kampuni ya AAR imetangaza kuuza vifaa vyote vilivyokuwa vinatumika katika kliniki saba nchini zilizopo mkoani Dar es Salaam, Mwanza na Arusha.
AAR ina kliniki tano Dar es Salaam; Posta (City Centre Clinic na New Chato Clinic), Mbagala, Tabata na Tegeta wakati Mwanza iko moja eneo la Mlango Mmoja na Arusha moja eneo la Philips.
Tangazo hilo limebainisha vifaa vinavyouzwa kuwa ni kompyuta pamoja na vifaa vyake kama vile printa, UPS, server na kompyuta mpakato. Vingine ni vifaa vya kieletroniki kama vile friji, projekta, mifumo ya CCTV na vifaa vya kuunganishia mtandao wa intaneti.
Vilevile, AAR inauza vifaatiba kama vile stendi za dripu, vipimo cha mkojo (urine analyzers) na kitanda cha magurudumu kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza au wale wanaopokelewa kutoka kwenye gari la wagonjwa (collapsible stretcher trolley).
Kampuni hiyo pia inauza vifaa vya maabara kama vile mashine ya X-Ray, mashine ya oksijeni, mashine ya kupima shinikizo la damu na kipimio cha meno (dental unit).
Mbali na vifaa hivyo, kampuni ya AAR pia inauza samani mbalimbali kama vile meza na viti vya ofisini, stendi za TV, mashefu, makabati pamoja na mabenchi.
“Kliniki hizo ziko katika viwango vinavyohitajika katika tasnia na viko tayari kutumika. Vifaa vya kudumu vinapatikana kwa ajili ya watua huduma za afya,” linaeleza tangazo hilo huku likibainisha kwamba watakaohitaji vifaa watume maombi kabla ya Mei 17,2021.
Chanzo: Mwananchi