ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,649
Ilikuwa ni mtiti mkubwa sikuwahi kuona. Ustaadhi mmoja maeneo ya dodoma alimkoromea mtoto wa jirani -mtoto wa mpangaji mwenzake-kisa kwanini yule mtoto aliyatia kidole maji yalokuwa yametengwa kwenye jiko la jirani huyo. Ilianza kama mzaha wakati ustaadhi akitoka nje kwenda kuoga huku mkewe akiwa na ndoo tayari kuyapooza maji ili mumewe akaoge. Ghafla ustaadhi akamuona jirani akipima joto la maji ili ayaipue jikoni ili apashe moto mboga.
Baada ya kuona kitendo hicho ustaadhi 'alimkoromea' sana huyo jamaa na aligoma kwenda kuyaoga hayo maji. Na kweli mkewe ilibidi amtengee maji mengine mumewe.
Binafsi sikuelewa kabisa kosa la yule jirani ya ustaadhi, hivyo naomba mnieleweshe wanajf, hivi tatizo ni nini kwa kitendo kile? Je kuna uhusiano gani na Mungu kwa kitendo kile maana kuna wakati jamaa alikuwa ana 'link' kutiwa kwa maji kidole na mambo ya kidini, ingawa hakuwa muwazi sana.
Nijuzeni waungwana maana sometime huwa nabaki kucheka tu kwa jinsi nilivyoichukulia lile jambo na maisha yetu waswahili ya kila siku.
Baada ya kuona kitendo hicho ustaadhi 'alimkoromea' sana huyo jamaa na aligoma kwenda kuyaoga hayo maji. Na kweli mkewe ilibidi amtengee maji mengine mumewe.
Binafsi sikuelewa kabisa kosa la yule jirani ya ustaadhi, hivyo naomba mnieleweshe wanajf, hivi tatizo ni nini kwa kitendo kile? Je kuna uhusiano gani na Mungu kwa kitendo kile maana kuna wakati jamaa alikuwa ana 'link' kutiwa kwa maji kidole na mambo ya kidini, ingawa hakuwa muwazi sana.
Nijuzeni waungwana maana sometime huwa nabaki kucheka tu kwa jinsi nilivyoichukulia lile jambo na maisha yetu waswahili ya kila siku.