Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,349
- 6,476
Jamani tujaribu kuwaelezea vizuri marafiki, ndugu na jamaa wa karibu kuhusu ukombozi kupitia Dr. Slaa. Juzi nilikuwa shamba nikaongea na mlinzi wangu mpaka akakubali kumchagua Dr. Slaa na maongezi yalikuwa hivi:
Mimi: Mwaka huu utapiga kura?
Mlinzi: Ndio, lazima.
Mimi: Kwa kusema ukweli wewe utachagua chama au mtu?
Mlinzi: Udiwani Chadema, Ubunge CCM, na Urais CCM
Mimi: Kwa nini Udiwani Chadema
Mlinzi: sina sababu
Mimi: Kwa nini ubunge na urais CCM?
Mlinzi: kwa sababu ni chama kikongwe
Mimi: Kwa muda wote huo wa chama hiki kikongwe hali yako kimaisha inazidi kuwa mbaya au nzuri?
Mlinzi: La! mbaya kweli kweli.
Mimi: Sasa kwa nini usichague atakayekusaidia kwenye elimu ya wanao na kuachana na yule anayesema hatakusaidia?
Mlinzi: ni kweli
Mimi: Ukimchagua ambaye hataboresha hata maisha yangu mimi, mshahara wako hautapanda, unalionaje hili?
Mlinzi: Hapo kweli umesema
Mimi: Sasa toa nafasi kwa maamuzi ya juu yaani kumchagua Mbunge - Mnyika na Rais - Dr. Slaa kwani wana uwezo bila kuangalia chama
Mlinzi: Mzee hii ni kweli
Mimi: Hivi si hata chakula huwa tunabadilisha - dagaa, maharage, ndizi, ugali, wali? Kwa nini isiwe kwenye uongozi?
Mlinzi: Mzee hapo nimekupata - Kura yangu sasa kuanzia udiwani mpaka urais Chadema!
Mimi: hapana usichague chama, yaani utachagua Maganga kwenye udiwani; chagua Mnyika kwenye ubunge, na Dr. Slaa kwenye Urais
Mlinzi: Mzee nashukuru.
Mimi: siku njema.
Du! wapiga kura bila kuwaelewesha bado ni wazito!
Mimi: Mwaka huu utapiga kura?
Mlinzi: Ndio, lazima.
Mimi: Kwa kusema ukweli wewe utachagua chama au mtu?
Mlinzi: Udiwani Chadema, Ubunge CCM, na Urais CCM
Mimi: Kwa nini Udiwani Chadema
Mlinzi: sina sababu
Mimi: Kwa nini ubunge na urais CCM?
Mlinzi: kwa sababu ni chama kikongwe
Mimi: Kwa muda wote huo wa chama hiki kikongwe hali yako kimaisha inazidi kuwa mbaya au nzuri?
Mlinzi: La! mbaya kweli kweli.
Mimi: Sasa kwa nini usichague atakayekusaidia kwenye elimu ya wanao na kuachana na yule anayesema hatakusaidia?
Mlinzi: ni kweli
Mimi: Ukimchagua ambaye hataboresha hata maisha yangu mimi, mshahara wako hautapanda, unalionaje hili?
Mlinzi: Hapo kweli umesema
Mimi: Sasa toa nafasi kwa maamuzi ya juu yaani kumchagua Mbunge - Mnyika na Rais - Dr. Slaa kwani wana uwezo bila kuangalia chama
Mlinzi: Mzee hii ni kweli
Mimi: Hivi si hata chakula huwa tunabadilisha - dagaa, maharage, ndizi, ugali, wali? Kwa nini isiwe kwenye uongozi?
Mlinzi: Mzee hapo nimekupata - Kura yangu sasa kuanzia udiwani mpaka urais Chadema!
Mimi: hapana usichague chama, yaani utachagua Maganga kwenye udiwani; chagua Mnyika kwenye ubunge, na Dr. Slaa kwenye Urais
Mlinzi: Mzee nashukuru.
Mimi: siku njema.
Du! wapiga kura bila kuwaelewesha bado ni wazito!